Nukuu takatifu ya Mkuchika!

kutokana na umuhimu wake katika taifa letu, nimeamua kutundika hotuba iliyotolewa na Mheshimwa Mkuchika Huko Busanda kwenye kampeni za uchaguzi kwenye jimbo hilo. Ni hotuba inayohitaji tafakuri ya kina sana.hotuba hii nimeitoa kwenye gazeti la leo la Nipashe.

Mapema jana asubuhi Mkuchika aliwacharukia waandishi wa habari wanaoripoti habari za vigogo wa CCM kuzomewa. Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Zakaria, Mkuchika alisema CCM ina nguvu na inakubalika ila waandishi ndio wanaifitini.

“Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,”alifoka Mkuchika.

Jamani huyu ndiyo waziri wa habari ambaye moja ya kazi zake ni kuhakikisha wananchi wana uhuru na uwezo wa kupata habari.Kama hayo haliyoyasema ndivyo basi hastahili kuwa waziri wa habari.kukosa umeme,kukosa habari hii nimja ya sababu ambayo imeifanya serikali ya CCM kuwa madarakani kwa muda mrefu.Kama walalahoi ambao idadi kubwa hawapati habari kupitia katika vyombo vya habari mbali mbali wengu hawafahamu madudu yanayofanywa na hao wanaowajihita viongozi.Sasa naanza kuelewa kwanini vyombo vingi vya habari vya serikali Radio Tanzania TBC ,television havina hata website kwani vyombo hivi vemelenga kuwadumaza walalahoi kwa propoganda za CCM na viongozi wao.Habari zao zikiingia katika mtandao na kusomwa au kutizamwa na watanzania wengi waishio nje ya nchi ni wazi watapata challenge kubwa.Kitu kingine ambacho najiuliza hivi hao viongozi wa CCM na serikali uwa wanaandaa hotuba zao au wanakurupuka tu na kuoanda majukwaani!CCM SIKIO LA KUFA ALISIKII DAWA MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Watanzania wanataka ushahidi gani tena? Mwenye dhamana ya habari kumbe anavikandamiza ili wadanganyika wabaki vihiyo sio? Busanda wamepata jibu, ila nasikitika nimeota leo mgombea wa ccm kapita. I hope not
 
Zitto alisha sema kila kitu kwenye hotuba yake, haya sasa bado CCM inadhidi kuji dhihirisha. Wanachi 2010 hiyo kazi kwetu.
 
“Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,”alifoka Mkuchika.

kweli akutukanae hakuchagulii tusi.........CCM wanatudumaza ili waendelee kuchukua vyao mapema......wamefikia hatua ya kutuambia dhahiri eti andikeni, onyesheni luningani (haijalishi maana wa busanda waala hawataona wala kusoma.

Pumbavu, wao si ndo hawajafikisha hiyo miundo mbinu muhimu huko!!!!!! Na lengo lao ndo hilo!

Poleni wenye mbunge wenu.....Mkuchika. amesha kuja huko au anasubiri kujiuza 2010
 
kutokana na umuhimu wake katika taifa letu, nimeamua kutundika hotuba iliyotolewa na Mheshimwa Mkuchika Huko Busanda kwenye kampeni za uchaguzi kwenye jimbo hilo. Ni hotuba inayohitaji tafakuri ya kina sana.hotuba hii nimeitoa kwenye gazeti la leo la Nipashe.

Mapema jana asubuhi Mkuchika aliwacharukia waandishi wa habari wanaoripoti habari za vigogo wa CCM kuzomewa. Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Zakaria, Mkuchika alisema CCM ina nguvu na inakubalika ila waandishi ndio wanaifitini.

“Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,”alifoka Mkuchika.

Thats what, as a minister, he has to say! Shame on him no wonder why he is making unsounding decisions in the ministry! who is the source of all problems he mentioned? Tena awaombe radhi wana Busanda kwa matusi makuu namna hiyo!
 
Maneno ya huyu waziri kilaza yana-potray tabaka la watawala linavyofurahia wananchi wa vijijini kuwa ktk filthy state kiasi cha kushindwa kupata habari na kujua kinachoendelea. Watawala wanajua hawa wananchi ni easy preys, ready to be exploited and deceived.

Nini kingine tutarajie kutoka kwa chama cha watu kama hawa? Ni wazi chama hiki ni adui wa kila mmoja wetu.
 
Very sad kusikia kiongozi anatumia umaskini na ujinga wa wananchi ambao kawasababishie mwenyewe madhara yote hayo na kuwa kama ngao kwake kujipatia cheo na kujilimbikizia mali huku akijua wamamchi hawana uwezo wa kuangalia TV kwa vile umeme hajawapelekea kwa makusudi....tuna safari ndefu kuwang'oa watu hawa.
 
.

“Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,”alifoka Mkuchika.

udhaifu MKUBWA SANA!inaonyesha namna gani CCM wanavyotumia udhaifu wa UMASKINI WA WATANZANIA kujineemesha.

DAMN IT CCM!
 
Ni kauli chafu na ya kutia aibu, au alidhani na sisi wengine huku pia hatutaisoma? Mbona mtanzania mwenzetu umekosa haya na adabu? Hivi ulikuwa sober kweli ukiongea hayo? (Nahisi hukumaanisha bwana ulikua unatania tu.......... mmh)
 
udhaifu MKUBWA SANA!inaonyesha namna gani CCM wanavyotumia udhaifu wa UMASKINI WA WATANZANIA kujineemesha.

DAMN IT CCM!

I wonder why he is still in BUsanda; CCM inabidi wawakane watu wa namna hii hadharani na kuwarudisha Dar Mapema kuonyesha kupinga kauli za ki***** kama hizi

Sijui kakumbwa na nini huyu baba!!!
 
Haya maneno matupu na hasira hayasaidii kitu..

Endapo yangegeuzwa kuwa vitendo naami viongozi wangekuwa wanaheshimu wapigakura.

Lakini kwa sasa bado tumefulia tukiongea kwa matendo hapo ewaaa! Mambo yatakuwa safi ufisadi no.
 
Sio siri, sijapata kuona mtu anayeongozwa na jazba katika maamuzi na matamshi yake kama huyu mzee, sometime unaweza kusema hata Mrema ana afadhali!!
 
".............vile vile ukimwona mtu anazomea jua kakata tamaa,'' alisema Waziri Mkuchika huku akizidi kuzomewa.

Mimi nimeumizwa sana na kauli hii.

Nakumbuka wakati wa uchaguzi 2005 mmoja wa wagombea wa CCM aliniambia " watanzania wanatupa karata ya mwisho ya imani yao kwa utawala, wakikatishwa tamaa baada ya utawala unaokuja (akimaanisha utawala wa Kikwete) basi ndio itakuwa mwisho wa Tanzania tuipendayo".


Miaka kadhaa baadae nikamsikia tena akisema katika mdahalo pale UDSM kuwa "nimeshuhudia jamii nyingi zikiparaganyika hapa afrika na sehemu nyingine ulimwenguni, kinachoendelea leo hapa kwetu kinashabihiana kabisa na kila hatua ambazo mataifa ya wenzetu yalipitia kuelekea mashafuko makubwa"


Inatia machungu sana kumsikia/kusikia Mkuchika akikejeli kukata tamaa kwa watanzania.....


omarilyas
 
Shame on you Mkuchika!! ipo siku sauti hizi zitawafikia hata hao mnaowakandamiza uko vijijini. Hufai kuwa hata house boy...
 
Mkuu

Nilidhani nasoma poem kumbe haya maneni si ya kutunga haya. yametoka mdomoni mwa mtanzania mwenye dhamana dhidi ya watanzania wenzake.

Ah walijisemea wahenga kwamba hofu ya kuku huwa ni desema kipindi cha noeli....

Mkuchika amenikifu
 
Kigarama ahsante sana. Natamani ningetoa photocopy hicho kipande na kumgawia kila mpiga kura wa Busanda ili ajuwe namna ambavyo kura yake ni muhimu kuuondoa huu ukoloni mweusi usiokuwa na huruma kwa wenye nchi. Mkuchika haoni aibu jamani kutamka hayo maneno mbele ya wanageita ambao wana utajiri mkubwa wa madini? Hili limenichafua kupita maelezo. Hawa ndio mawaziri wa jk ambao kigezo c uwezo wa ubongo au uchapa kazi bali ni uanamtandao au uwe former classmate wa kisura full stop. Anyway lakini pia mimi simshangai sana mkuchika kwani ninamjuwa toka akiwa mkuu wa wilaya ya ilala enzi za anbem. MKUCHIKA NI ZERO ya kutosha tu nawezo kuthibitisha hilo.
 
kutokana na umuhimu wake katika taifa letu, nimeamua kutundika hotuba iliyotolewa na Mheshimwa Mkuchika Huko Busanda kwenye kampeni za uchaguzi kwenye jimbo hilo. Ni hotuba inayohitaji tafakuri ya kina sana.hotuba hii nimeitoa kwenye gazeti la leo la Nipashe.

Mapema jana asubuhi Mkuchika aliwacharukia waandishi wa habari wanaoripoti habari za vigogo wa CCM kuzomewa. Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Zakaria, Mkuchika alisema CCM ina nguvu na inakubalika ila waandishi ndio wanaifitini.

"Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,"alifoka Mkuchika.

Mkakati wa CCM ni kuwafanya watu wawe masikini wasifikirie kingine zaidi ya mlo wa leo utatoka wapi?, hiyo ndiyo itawafanya wao waendelee kutawala daima kwani hakuna atakaye angalia uwongo wao, Ila wanasahau kuwa mtu akiwa anazama akiona hata unyoya ataushika akidhani utamuokoa, sasa watanzania wanadhani kuwa solution ni kuzomea na kuwapigia kura wapinzani, hilo Mkuchika hajalifikiria katika karata zake.

"Sooner or Later CCM will be out of power"
 
kutokana na umuhimu wake katika taifa letu, nimeamua kutundika hotuba iliyotolewa na Mheshimwa Mkuchika Huko Busanda kwenye kampeni za uchaguzi kwenye jimbo hilo. Ni hotuba inayohitaji tafakuri ya kina sana.hotuba hii nimeitoa kwenye gazeti la leo la Nipashe.

Mapema jana asubuhi Mkuchika aliwacharukia waandishi wa habari wanaoripoti habari za vigogo wa CCM kuzomewa. Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Zakaria, Mkuchika alisema CCM ina nguvu na inakubalika ila waandishi ndio wanaifitini.

“Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,”alifoka Mkuchika.

aibu kubwa
 
....“Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,”alifoka Mkuchika.
Nakubaliana na Mkuchika kaamua kusema ukweli. kwa kuwa hao watu hawana umeme kutokana na sera mbovu za chama dume tangu uhuru mpaka sasa... Hivyo anasifia sera zao kwa ujuha
 
Back
Top Bottom