Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
kutokana na umuhimu wake katika taifa letu, nimeamua kutundika hotuba iliyotolewa na Mheshimwa Mkuchika Huko Busanda kwenye kampeni za uchaguzi kwenye jimbo hilo. Ni hotuba inayohitaji tafakuri ya kina sana.hotuba hii nimeitoa kwenye gazeti la leo la Nipashe.
Mapema jana asubuhi Mkuchika aliwacharukia waandishi wa habari wanaoripoti habari za vigogo wa CCM kuzomewa. Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Zakaria, Mkuchika alisema CCM ina nguvu na inakubalika ila waandishi ndio wanaifitini.
Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,alifoka Mkuchika.
Mapema jana asubuhi Mkuchika aliwacharukia waandishi wa habari wanaoripoti habari za vigogo wa CCM kuzomewa. Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Zakaria, Mkuchika alisema CCM ina nguvu na inakubalika ila waandishi ndio wanaifitini.
Nyie andikeni mnavyotaka, hata kwenye TV onyesheni, kwanza watu wa huku TV hawana kwa vile hata umeme hawana! Hizo TV zenu watazitazamia wapi. Na nyine wenye magazeti kwanza huku hayafiki na hata yakifika wananchi hawana uwezo wa kuyanunua, watasomea wapi hizo fitina zenu. Hayo mnayoandika yanabakia kuwa yenu na wamiliki wa vyombo vyenu,alifoka Mkuchika.