Nukta za Zitto kuhusu vurugu za wana-uamsho Zanzibar

Jibu lako ni rahisi sana.
Makanisa yamepelekwa zenj na muungo.
Kabla ya muungano zenj haikuwa na utitiri wa mabaa na makanisa.:banghead:

Wewe ndiye huelewi kabisa. Kama wewe ni Muunguja mweusi uwezekano mkubwa mababu zako kubakizwa Zanzibar badala ya kufikishwa kwenye soko la utumwa (India??) ilitokana na jitihada ya Padre Mmisionari aliyekuwa akiwanunua watumwa na kisha kuwaachia huru, na kuwanunulia ardhi kutoka kwa sultani wa Kiarabu na kisha kuwagawia. Makanisa yamekuwepo Zanzibar kwa miaka mingi sana kabla ya Mwungano. Unaelewa lile kanisa la Anglikana la pale mji mkongwe walipokuwa wanacharaziwa watumwa wakati wa kuuzwa lilijengwa mwaka gani?
 
Funga domo lako kama umetumwa nenda kawaambie kanisa lako hoja yako inanuka.Shenzi

Kwa kuwa wameonesha kuwa nia yao ya kutaka kuuvunja mwungano ni kushambulia imani za kidini, hao ni watu wa kuadhibiwa vikali na dola ili wajue kuwa katika Tanzania mambo yote yanaweza kuvumiliwa lakini siyo harakati za kuleta udini na ukabila. Hawa wasionewe huruma hata kidogo. Viongozi wao watakapokuwa jela, jitihada za kuwaelimisha wale waliovutwa kwa mkumbo ziendelee. Kuutaka au kutoutaka mwungano hakuhalalishi uchomaji wa makanisa.

Na katika hili la kuchoma makanisa, ndugu zako Waislam inabidi walijadili sana ili kuona wanaweza kulidhibiti vipi. Sijawahi kusikia Wakristo mahali popote Duniani wakichoma misikiti lakini ni mara nyingi sana kusikia kuwa waislam wamechoma makanisa. Hili halileti picha nzuri kwa uislam katika jamii za watu waliostaarabika na wanaoheshimu uhuru wa kuabudu. Waislam wachache wanaofanya mambo hayo wanaudhalilisha uislam kwa ujumla, na kuufanya uislam uonekane ni imani inayopalilia vurugu na utengano miongoni mwa jamii zenye imani tofauti.
 
Wananchi wengi hawana utamaduni wa kusoma au kufuatilia mambo na ni wajibu wa serikali kuweka mambo yote wazi hasa hasa hili la Muungano. Je wananchi wakijua kwa kina Muungano uko vipi wataweza kupingana na viongozi ambao kila upande unaona unapoteza bora kujitenga? Hili suala limeachwa kwa muda sana na kwa uzembe wa viongozi sasa itakuwa ngumu kudhibiti hali kwani si Muungano tena, bali dini imeingilia kati na ni watu wachache wasiojua dini vizuri wanaleta matatizo. Tatizo kubwa ni uongozi wa sasa kutokubali mawazo hasa hasa ya upinzani, hapa wakishauriwa zuri wanaona watakuwa wamefanyia kazi upinzani bila kujua hili vuguvugu linaletwa na mataifa ya nje kuvuruga nchi za Afrika, Mombasa wameenza majuzi haya haya ya kutaka kujitenga.


Naamini waandishi hawakumwelewa Katibu Mkuu. Mkataba wa Muungano upo. Ni moja ya hati za makabidhiano kwa kila Katibu wa Bunge na Dkt. Slaa amekuwa Mbunge muda mrefu na hawezi kusema walichoandika waandishi. Mkataba wa Muungano ulijadiliwa katika Bunge la Tanganyika na Hansard zipo kila mahala. Mkataba wa Muungano sio jambo la siri hata kidogo na wala haliwezi kuwa jambo la siri.

Ni kweli wananchi hawaujui muungano. Hii ni kutokana na watawala kutotaka tuujue muungano. Lakini kutoujua hakutun yimi haki ya kuujadili muungano na kuamua hatma yake.
 
Jibu lako ni rahisi sana.
Makanisa yamepelekwa zenj na muungo.
Kabla ya muungano zenj haikuwa na utitiri wa mabaa na makanisa.:banghead:

kwa hiyo unamaanisha waliopeleka makanisa huko ndo wameaanzisha mabaa na bangi kwanini nyie watu mna roho za ukatili sijawahi sikia kuwa wakristo wamechoma msikiti sina imani na MUNGU gani mnayemwabudu mnatisha kwa ukatili
 
jeshi litahakikisha linalinda aman na usalama wa raia na mali zao kwa nguvu yeyote ile...MSICHEZEE DOLA NYIE WENYEWE HATA MILION 2 HAMFIKI MNATAKA KUTUSHUGHULISHA SIE TUKO BUSY NA MAMBO YA MSINGI,TUWAZALISHIE UMEME,TUWALISHE,TUWALINDE NA BADO MNALETA FYOKOFYOKO HAPA,TUNAWASOMESHA KUPITIA BODI YA MIKOPO,HAMNA PESA YEYOTE,MNAJENGA HUKU,BADO TUU MNAPOTEZA MUDA KWA VURUGU,ALA

.
Kibaya zaidi ni kwamba amiri jeshi mkuu ndie alieasisi vugu vugu hili la kidini wakati wa kampeni zao urais 2010. Sasa kweli jeshi litamkamata amiri wao?
.
 
SIUNGI MKono kuchomwa kanisa lkn nakumbuka siku kama nne zilizopita kuna padri kaitaka serekali idhibiti UWAMSHO TAASISI YA KIISLAM na wazanzibar 99% ni waislamu .serekali ya muungano imeitika wito wa padri kwa kumkamata shehe musa msikitini zanzibar unategemea nn kitokee kwa wazanzibar kufatwa misikitini na SMT tusitegeme kupanda mgomba tukavuna embe polisi wa smt ndio chanzo
 
Chanzo cha vurugu Zanzibar kinajulikana, ni lile lile dubwana muungano. Hata muwatie ndani wazanzabar wote, mutayastopisha mapambano lkn hamtayaondoa, kwani wameshauliwa weng na wengne kutiwa ndani tokea 64, kwa ajili ya muungano huu ili kuudhbit na kuulinda kwa nguvu zote. Alimradi kizazi cha kizanzibar bdo kpo kinaendelea, mizozo hii kamwe haitosita, mpaka wapewe haki yao
Kwahiyo hayo makanisa yaliyochomwa moto ndo yaliyoleta huo Muungano?. Kuna mtu fulani hapa alishawahi kusema kuwa hakuna hata Mzanzibar mmoja mwenye akili timamu nikamuona kuwa hayupo sahihi ila kwa sasa naweza kuhisi nini alichokuwa anamaanisha.
 
Uwamsho taasisi ya kiislamu imekana kuhusika na kuchoma kanisa na inashutumu kupangwa mpango huo ili kupakwa matope na kubadili mada wanasema wakristu znz ni jamii ndogo na mkanisa yamo kwenye mitaa ya waislamu na hayana ulizi wowote zaidi ya wakazi wa maeneo ambao ni waislamu hili limechomekwa kama kubadilisha mada WAZANZIBAR HATUTAKI MUUNGANOOOO makanisa viwanja tunawauzia wenyeweee kila mtu na dini yake sio mada hapa muunganoo ushakuwa kerooo kwa maslahi yetu
 
  • Thanks
Reactions: dkn
Makanisa hayajaanza kuchomwa huko zanzibar jana. Yamechomwa toka 2010 na kama sikosei hilo la jana litakuwa ni kanisa la tano kuchumwa. Cha ajabu na cha kustajabisha hakuna aliyechuliwa hatua mpaka sasa. Serikali inayojinadi kuwa Tanzania ni kisiwa cha amani imenyamaza na kujifanya kana kwamba hakuna kitu kilichotokea.

Hivi nijaribu kuwauliza kama ni wakristo wangechoma msikiti mmoja tu hata kama ni wa makuti ingekuwa je? Sasa haya mambo yanatufanya tuamini yale yanayosemwa kwamba nchi kwa sasa ina miaka saba ikijiendesha yenyewe bila kuwa na kiongozi mkuu. Na kama yupo hajijui ama hayajui majukumu yake na wala hayajui majukumu ya watendaji wake aliowateua.
 
Hivi hawa mafirauni wametumwa na nani?kama wanataka vita waseme tuzichape mana tumekaa kmya na sasa tuseme imetosha
 
Hapa tatizo si ku distruct mchakato wa katiba.hapa wanataka wanayoyafanya yaingie ktk Katiba au hata katiba iandikwe kukiwa hakuna muuungano.

Serikali ndio ilianzisha mchakato kihuni.Shida ni kwamba wanayafanya vibaya.

-Suala hapa ni udini uliojengeka kama ilivyoelezwa ktk no2 hapo juu ndio unang`aa kuhalalisha chuki juu ya muungano. Na udini umechukua nafasi ya uelewa mdogo wa watu za zanzibar kuhusu muungano na uzembe wa serikali kutoruhusu ama serikali moja ambayo ingedilute watu au hata 3 ili kuleta sense ya mipaka kiutawala. Nimekuwa zanzibar vijijini vijana wengi wanaijua dar ipo km miji ya ulaya, wanaamini kuwa umangani maisha ni rahisi sana na masikini wanaweza jichukulia magari yaliyozagaa mitaani, ila Serikali Kristu ya bara inawazuia hao wamanga kuja.

Vijana wanaamini conspiracy theory kuwa Kanisa Katoliki ndilo linaongoza nchi na akina Kikwete ni vikaragosi na ushahidi ni MOU ktk ya kanisa na serikali.

Hakuna kiongozi serikali na hasa wa Zanzibar kaweza litolea maelezo sahihi na ya kiungwana, kwa sababu linapokuja suala la dini ni gumu kumeza wanatafuta sababu na kuliweka chini ya carpet. Pia viongozi wa Zenji ni wabinafsi na wasaliti kwa watu kiasi ch akushindwa wekeza Zenji zaidi ya dar.

Pamoja na kendekeza ubaguzi bado maelezo kwa watu wao wakiwa zenji ni tofauti sana na wanachokiongoa ktk muungano. Hawana ujasiri au pengine wana hila ktk Muungano. Waislamu wa bara nao hawajawa na nia ya kuupenda muungano.

Na pia wamedhani kuwapa Zanzibar nchi ni kuwapenda na si kuwachukia kwani kinachoendelea pale ni chuki za waislam kwa waislam, waarabu na waswahili ,wapemba na waunguja,na njia pekee ya kuzuia hilo ni kuweka Muungano imara. Pia uelewa mdogo kwa wananchi na viongozi wa kisiasa na kijamiii wa sura nyingi na maslahi mengi ktk zanzibar. -Mbali na uwakilishi sawa ktk Muungano, kuna uwakilishi sawa ktk haya: Dini, jinsia,(unguja v/s pemba). Na wala si suala la uchache kwani hata wao ktk muungano ni wachache ila wana uwakilishi sawa ktk kila kitu.Marais wote hawakuliona hili.

-Pia Zanzibar wanatakaiwa wajue kuwa uhuru wa kuabudu si kwa bara tuu ila ktk Jamhuri ya muungano nzima. Na wajue pia pia watu wanaoamua kuacha dini moja na kuingia ingine wana uhuru .Pamoja na kuwa waislam ni wengi ila wanaweza kuongezeka ama kupungua pia. Na hili lihubiriwe na serikali na liende mbali hadi ktk hiyo mahakama ya kadhi. Wajue kuwa uhuru wa muislam kuuacha uwepo na uhuru muislam kuingia ktk mahakam secular upo pia. Hata km inauma basi wajue cha kufanya kuwaombea dua ili waone njia sahihi. Suala la udini Zanzibar si la kuuliza ,na wala si la wachache, kuanzia moderate hadi kwa islamists, na hili limetokana na mfululizo kwa propaganda kwa miaka mingi.

Na imani kuwa uislam ndio dini pekee sahihi na hakuna tafrsi mbadala. Watu wanaongea mengi wanapendana na baadhi ya wabara ila wanakuwa wamoja linapokuwa suala la muungano. Kuna uanfiki mwingi visiwani kuliko bara.

Huyo Zitto akitaka jua a beep akiwa anachat na wabunge wa visiwani akiwa bara halafu achat nao tena wakiwa viswani mbele ya wazenj wawili watatu ambao hawatoki familia za viongozi. Familia za viongozi wanapenda muungano wakati unawafaidisha, unapowawezesha kukumbia ukweli wa maisha ya Zenj.
 
Zanzibar imechafuka. Serikali itume JWTZ kwa ajili ya kutunza amani. Nasema kutunza amani na siyo kutuliza ghasia kwani naelewa tofauti yake.

Askari wa JWTZ wawepo mitaani wanarandaranda tu na silaha. Wasiwe wa kwanza kupiga. Wasiwanyime waZenji uhuru wa kuzurura. Rules of engagement ni kupiga vibaya sana pale mtu atapothubutu kuchokoza.
 
1 .Vurugu za Zanzibar ni 'unwanted distractions' katika mchakato wa kuandika katiba mpya.

2. Hakuna namna vitendo hivyo vinaweza kuhalalishwa na kutetewa lakini ni matokeo ya muda mrefu ya 'superficial attempts at dealing against groups with ulterior motives.

3. Rais Ali Mohamed Shein aunde kikosi kazi maalum kwa ajili ya kudhibiti vurugu hizo, na kuanza mzungumzo na pande zote. Hiki sio kitendo cha kudharau kabisa

4. Muungano wetu ni sacred na tumetoka mbali kushindwa sasa kuulinda, 'not when we are so close at having an everlasting formula'

5. Waliochoma nyumba za ibada wasakwe na kufikishwa mbele ya sheria mara moja. Tusiruhusu hata kidogo wapuuzi wachache
kutuingiza katika vurugu za kidini ili kufikia malengo yao ya kisiasa.

6. Zanzibar Political leaders and public opinion makers must engage the Zanzibaris into a serious and objective dialogue about the future of Zanzibar within or outside the Union.
hapo nilipo bold-umekosea-huu muungano si lazima udumu-kama ulianzishwa kwa reason "hewa" then ukahang for such long time kwa sababu ya woga wa watu na propaganda za chama-sasa ni wakati umefika wa kila mtu kuangalia na kama kuna haja ya kurenew terms au kama kuna haja ya kuwa na kitu inaitwa muungano-kama hakuna-kila upande uchukue ustarabu wake-
si lazim tuungane na hawa wa zenji-mbona Soviet Union ilikwisha,na ni nchi ngapi za kiafrika zilishawahi kuungana na zikavunja huo muungano wao?kwa nini sisi iwe ngumu kuushika kwa huu wetu kuvunjika
 
New generation(kizazi cha miaka ya 70's and 80's) hatuna cha kujivunia ndani ya muungano,so to hell with it.
 
Watu wanatumia madhaifu ya muungano kutimiza adhima zao binafsi kama kuchoma makanisa,bar na kuwatimua wabara,so what the point kuwa na muungano wa aina hii?
 
Again wisdom na conflict resoultion abilities za hawa viongozi wetu simaanishi akina membe na issue ya libya zinakuwa under test

Namaanisha viongozi wa ndani. Hawa jamaa wakipeleka Jeshi vibaya ktk matukio picture zitakazopatika zitatumiaka km kisingizi cha umwagaji damu na uonevu.

Inabidi waende wanajeshi km dharura na pia kuwepo na watu wenye ushawishi na busara wapite mitaani kupata maoni ya raia wa kawaida ambao hawana ulewa mkubwa wa mambo ila wanawafuata hawa jamaa wenye malengo fulani.

Baada ya maoni TV ya Zanzibar, na redio na magazeti watangaze majibu ya mwaswali na maoni kwa ufasaha.

Na tahadhari yenye sura ya upendo na tahadhari ifuatie kwa uma na kwa vyombo vyote ikiwaleza watu hasara ya kujiingiza ktk vitu visivyo na maslahi ya uma wala binafsi si vyema sana kwao, nakupoteza muda ktk Muungano hakuwasaidii sana km kupambana na viongozi wa sheia zao ili wawaeleze kwanini mahesabu fulani hayako sawa, kwanini wanauza viwanja kwa watu wa nje ya nchi, na pia wajue kuwapiga vita watu wa bara ni kujiweka pasipo sahihi. Pia kuwa na majibu yanayowakatia link na viongozi uchwara wa dini na kisiasa.

Na hapa najua viongozi wa zenj ktk CCM ya leo hawatapenda kwani nao wanakula kotekote ktk hili jambo ili kuepusha kufa kisiasa kule zenj.
 
Sijabahatika hata siku 1 kumuona Zitto msikitini, hata picha 1 ya zitto kusalimiana na viongozi wa dini ya kislam. Ni wazi ni muislam Jina. hana uchungu kabisa na uislam na waislam wa tz. kauli hii ingalitolewa na akina Abdalla safari ningalishtuka, lkn Zitto uislam wake unamashaka. ndio maana hadi leo ndoa yake haiujlikani kama itafungwa kiislam au mahakamani
 
1 .Vurugu za Zanzibar ni 'unwanted distractions' katika mchakato wa kuandika katiba mpya.

2. Hakuna namna vitendo hivyo vinaweza kuhalalishwa na kutetewa lakini ni matokeo ya muda mrefu ya 'superficial attempts at dealing against groups with ulterior motives.

3. Rais Ali Mohamed Shein aunde kikosi kazi maalum kwa ajili ya kudhibiti vurugu hizo, na kuanza mzungumzo na pande zote. Hiki sio kitendo cha kudharau kabisa

4. Muungano wetu ni sacred na tumetoka mbali kushindwa sasa kuulinda, 'not when we are so close at having an everlasting formula'

5. Waliochoma nyumba za ibada wasakwe na kufikishwa mbele ya sheria mara moja. Tusiruhusu hata kidogo wapuuzi wachache
kutuingiza katika vurugu za kidini ili kufikia malengo yao ya kisiasa.

6. Zanzibar Political leaders and public opinion makers must engage the Zanzibaris into a serious and objective dialogue about the future of Zanzibar within or outside the Union.

Kwa bahati siajwahi kuona Picha ya zitto akiwa katika nyumba ya Ibada ya waislam , sijabahatika kuona akisalimiana na viongozi wa dini ya kiislam. Siamini kama zitto ana ushawishi ktk jamii ya kiislam. kwa picha ya mbali zitto nawezza kumuona zitto ni muislam Jina. hata harusi yake hatujui itafungwa kwa madhehebu gani
 
Sijabahatika hata siku 1 kumuona Zitto msikitini, hata picha 1 ya zitto kusalimiana na viongozi wa dini ya kislam. Ni wazi ni muislam Jina. hana uchungu kabisa na uislam na waislam wa tz. kauli hii ingalitolewa na akina Abdalla safari ningalishtuka, lkn Zitto uislam wake unamashaka. ndio maana hadi leo ndoa yake haiujlikani kama itafungwa kiislam au mahakamani
uchungu gani?kwani wamefanyaje?/wamefanywa nini?
 
Sijabahatika hata siku 1 kumuona Zitto msikitini, hata picha 1 ya zitto kusalimiana na viongozi wa dini ya kislam. Ni wazi ni muislam Jina. hana uchungu kabisa na uislam na waislam wa tz. kauli hii ingalitolewa na akina Abdalla safari ningalishtuka, lkn Zitto uislam wake unamashaka. ndio maana hadi leo ndoa yake haiujlikani kama itafungwa kiislam au mahakamani

kaka inahusian vipi na kuwanyima wakritu haki pamoja na kuharibu mali zao?Au kutaka hao waliofanya hivyo kuonja sheria kunahusiana vipi na uislam wa Zitto.Hapa hata Mbwa angesema kuwa kuchoma ni kosa lingekuwa kosa pamoja na kuwa anweza hesabika ktk ni haramu.

Hapa ndipo wanapohitajika waislam kweli wasimame wakemee na washududie hata km ni ngumu kidini.Ila waifany rahisi kwa kutazama haya matendo km yanaharibu na kuchafua dini kuliko faida wanayodhani inakuja.

Ni kipidni waislam waliosoma na kushika nyadhifa, wakashuhudia na kuyafanya maamuzi ya serikali, wanafahamu sheria za nchi wasimame wayaseme ktk makongamano ya kiislam,wayaseme ktk kamati za miskiti, wayaseme ktk familia zao, na wayaseme wanapopokea misaada toka nchi zenye tabia km hizi.

Waseme bila woga kwani bila hivyo ipo siku itabidi waseme wakiwa wamevaa bullet proof, wakiwa mafichoni, wakiwa mawepoteza mali walizotuibia na watoto waliowapata wakitumbua kodi zetu.

Ni kipindi cha waislam kweli na waislam jina kuondoa unafiki na kusema kweli na iliyo kweli na si relative truth.Naamini hata muislam jina km hajaukana bado nimuislam na akifa atazikwa kiislam na km ni vinginevyo kosovo lake ,halituliziki.

Naomba mheshimiwa ujiweke ktk mazingira ya Wakristu halafu jiulize ingekuwa ni MSIKITI UMECHOMWA makanisa mangapi yengungua ndani na nje ya zanzibar, wakristu wangapi wangeuwawa duniani za si Zenji pekee.Hiyo busara ikitumika utaona makosa yanayofanyika pale zenj kizembe.Issue itageuka kuwa ya waislam wote na wakristu wote,ila mbaya zaidi wazenji wengi wataangamia kwani wenye kupataka hawatapenda tena mbegu ya watu waliopo.Na patagawanywa kirahisi kwa matajiri wachache na kuwa kisiwa cha zinaa,uharamia etc.
Take my note.(Wazenjenj ni km watu wa Yemen hawatakiwi na waarabu wala Wazungu ktk maisha ya kawaida).Ila wanahitajika kwa kazi maulumu km hizi zinazotokea.Km umekaa zanzibar na pwani sikia jinsi walio na rangi isiyo nyeusi wanvyopenda jipambanua km waarabu, jinsi wanavyo watazama weusi wasio viongozi, wasio matajiri, wasio na vipaji fulani vya kutumika?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom