NSSF na Infrastructure Investment: Kigamboni Bridge, IPP, Road Construction.. ???

NImeanza kuangalia hapa (ndani ya siku hizi chache zilizopita) na ninaanza kuona tatizo mahali fulani; japo kwa juu inaonekana vizuri sana lakini naanza kuhofia na ninashindwa kuelewa kwanini NSSF inawekeza fedha za wafanyakazi wake kwenye miradi hii mikubwa ya Umeme, Ujenzi wa Madaraja na sasa Ujenzi wa Barabara.

Kuna kitu hakiko sahihi; nia yaweza kuwa nzuri lakini kuna kitu hakiko sahihi... sijui ni kitu gani bado.. lakini something is very very wrong somewhere..

Miradi mingine wanayobuni NSSF ni mizuri lakini kama watategemea kwa asilimia 100% serikali katika uwekezaji wake ...ikishindwa kuwalipa basi pesa za wafanyakazi zitakuwa hatarini..mfano mashirika haya yamewekeza sana UDOM ni jukumu la serikali kuhakikisha kuwa inayalipa haya mashirika marejesho kwa wakati...

Nashauri miradi ya barabara ...ie interchanges ,flyovers etc...NSSF Wakishirikiana na mashirika mengine yafanye hivi....
- Yapewe na wizara ya ardhi maeno makubwa ..amabayo watayaendeleza kama satelite cities....na hizo bara bara wajenge kuhakikisha maeneo watakayowekeza kwa makazi na viwanda....yana miondo mbinu ya uhakika.....wakaazi watakao chagua kuishi kwenye maeno hayo ..they have to pay road toll...au watakaopenda kutumia .....ni biashara ya uhakika...lakini kujenga na kuwapa serikali itakuwa haina impact.....we need have TOLL ROAD AUTHORITY...
-Njia nyingine ni kuwekeza kwenye highways ...mfano tumegundua we have only one road exit in north from dar..and another ipo south[kilwa road]...tutakuwa na nyingine bagamoyo karibuni.......that has to be under toll road ---PPP.
NSSF wanaweza kujenga njia nyingine alternative ya kutoka AIRPORT hadi MBEZI....HADI chalinze ..inayojitegemea hiyo iwe EXPRESS CARRIAGE HIGHWAY....mtu ambaye ana pesa yake na anaona njia ya ubungo inamchelewesha kuingia au kutoka dar.....simply anaingia kwenye NSSF carriage way...analipa anaambaa zake ..simple....

Mradi wa umeme hauwafai NSSF ...kwani sheria bado inaweka wazi muendeshaji ni TANESCO ...isitoshe hao TANESCO walipewa 100 bilioni..syndicate loans na mabenki na wakashindwa kulipa...so ni risk kuingiza pesa za wafanyakazi kwenye mradi wa umeme ..pia sababu kubwa ni kuwa NSSF Ni wazuri kwenye uwekezaji wa properties na ndio maana hata barabara wakiwekeza kwa mfumo huo hakuna neno....kujipeleka kwenye umeme ni kwenda mbali sana nje ya uwekezaji wao wa kawaida ...hawana uzoefu..kabisa!!..na sio vizuri kwenda nje sana na uzoefu kwenye biashara!!
 
Ni kwa kiasi gani?

a. NSSF Inawekeza katika senior housing?
b. NSSF Inawekeza katika huduma ya afya ya wanachama wake?
c. Binafsi ninapenda miradi ambayo ni ya NSSF yenyewe kuliko ile ya kiserikali; kwa mfano, wakijenga nyumba za makazi au maofisi ambayo ni "yao' ni rahisi fuatilia na kuwajibishana. Kwenye hiyo ya PPP nadhani haina tatizo sana isipokuwa kama inapangwa vizuri.
d. Miradi hii mikubwa mitatu tu (au minne ukiongeza na Kiwira) kwa wakati mmoja inapresume mambo mengi sana kuwa yako constant.
 
you are catching up faster...

Unahangaika na NSSF tu au na mifuko mingine ya pension pia? (just curious)

Kwa taarifa yako Tanzania kuna mifuko sita yenye sifa kama NSSF na zenye pesa nyingi pia (hufahmu au unajidai hufahamu?)

Nikutajie PPF, LAPF, GEPF, PSPF, NHIF...

Kama kuongelea tuongelea zote kwa kuangalia wana Invest wapi? na kwa faida ya nani?
 
Unahangaika na NSSF tu au na mifuko mingine ya pension pia? (just curious)

Kwa taarifa yako Tanzania kuna mifuko sita yenye sifa kama NSSF na zenye pesa nyingi pia (hufahmu au unajidai hufahamu?)

Nikutajie PPF, LAPF, GEPF, PSPF, NHIF...

Kama kuongelea tuongelea zote kwa kuangalia wana Invest wapi? na kwa faida ya nani?

ukisoma vizuri utaona inauhusiana na uwekezaji kwenye maeneo fulani; kama na weewe unaona mashirika mengine nayo yanahitaji kuangaliwa uwekezaji wake, unatakia kutoa mchango wako na kuhoji usisubiri mtu mwingine afanye halafu uje "mbona na kule hamuangalii" kwanini wewe huna chembe za Ubongo?
 
ukisoma vizuri utaona inauhusiana na uwekezaji kwenye maeneo fulani; kama na weewe unaona mashirika mengine nayo yanahitaji kuangaliwa uwekezaji wake, unatakia kutoa mchango wako na kuhoji usisubiri mtu mwingine afanye halafu uje "mbona na kule hamuangalii" kwanini wewe huna chembe za Ubongo?

Ubongo wako ndio unakufanya ujadili mambo kiaina huku unaficha nia halisi...(???) usituzuke hapa...ingekuwa

objectives ungechukau "holistic approach" mifuko ya pension Tanzania?? zina invest kwa interst ya nani?

Tatizo lako kule kuliko na wenzako unajifanya mbogo..pole...we know your aim???
 
NImeanza kuangalia hapa (ndani ya siku hizi chache zilizopita) na ninaanza kuona tatizo mahali fulani; japo kwa juu inaonekana vizuri sana lakini naanza kuhofia na ninashindwa kuelewa kwanini NSSF inawekeza fedha za wafanyakazi wake kwenye miradi hii mikubwa ya Umeme, Ujenzi wa Madaraja na sasa Ujenzi wa Barabara.

Kuna kitu hakiko sahihi; nia yaweza kuwa nzuri lakini kuna kitu hakiko sahihi... sijui ni kitu gani bado.. lakini something is very very wrong somewhere..

Labda ungelitusaidia wewe mtazamo wako ni upi hapo? Kuna ubaya gani NSSF kuwekeza kwenye madaraja, barabara, Ujenzi na Umeme?
Lipi ni bora zaidi kuwekeza katika maendeleo au kuacha ziliwe kama anavyofanya Urio kule PPF?
 
naanza kuhofia na ninashindwa kuelewa kwanini NSSF inawekeza fedha za wafanyakazi wake kwenye miradi hii mikubwa ya Umeme, Ujenzi wa Madaraja na sasa Ujenzi wa Barabara.

mmmh! Hapo kwenye barabara na madaraja wanawekeza au wanasaidia jamii!
Nashindwa kuelewa watatengeneza vipi faida.
Au serikali ipo kwenye mkakati wa kupanga bei kwenye huduma hizo.

Investment kwenye umeme nasupport ingawa risk yake ni kubwa lakini high risk high returns.
 
mmmh! Hapo kwenye barabara na madaraja wanawekeza au wanasaidia jamii!
Nashindwa kuelewa watatengeneza vipi faida.
Au serikali ipo kwenye mkakati wa kupanga bei kwenye huduma hizo.

Investment kwenye umeme nasupport ingawa risk yake ni kubwa lakini high risk high returns.

Katika barabara na madaraja faida ipo kwenye interest charged to the government. Nssf sio wajinga waende tu kujenga barabara ni makubaliano kati ya serikali na NSSF. Makubaliano hayo ni kwamba NSSF inajenga daraja kwa mkopo na serikali inawalipa kidogo kidogo mpaka mkopo unaisha. Ni akili nzuri sana na binafsi wanaunga mkono 100%.

Umeme pia ni uwekezaji wenye faida kwani kuna monopoly katika sekta. Huo ndio ubepari halisia sasa sioni tatizo hapo ndio maana namuuliza Mzee Mwanakijiji shida ipo wapi?
 
Nimeongeza viambatanishi kadhaa kusaidia mjadala maana wengine kwa kuogopa kugonganisha vichwa kwenye mambo muhimu kama haya watakuja na hoja zisizo na uhusiano na mjadala ili kupoteza mwelekeo wa hoja.
 
Kutokana na mambo yalivyo sasa, ukiona kitu kinang'ang'aniwa sana na asasi za umma, ujue hapo kuna ulaji wa kufa mtu. Tulipofikishana sasa pako wazi kabisa....hakuna kitu kinachofanyika bila maslahi binafsi.
Hii miradi ambayo Nssf inataka kuifanya, siamini ni kwa ajiri ya kusaidia watu wa kawaida....ni ya kutengeneza ulaji kama ilivyokuwa ule mradi wa Bot. Time will prove me otherwise but for now that is what I believe. Na kama ningekuwa na uwezo, kuliko hela zangu kuchezewa bila huruma, ningezichukua zote na kuziweka mfukoni mwangu. Bora nikalewe ziishe zote siku moja kuliko kuambiwa uliweka ila mfuko umefilisika nikaishia kuhangaika kama wastaafu wa afrika mashariki
 
Kama mtu hatokuwa na muda wa kusoma viambatanishi vyote napendekeza upitie conclusion ya Pension Watch ambayo inadokeza kwa mbali tu matatizo ambayo ninayaona ya NSSF au Pension fund nyingine yoyote kuwekeza katika miundombinu katika mazingira ya kiuchumi, kisheria na kisiasa ya Tanzania.
 
MS: Kwenye kukopesha wanachama nadhani mtazamo wako sio sawa.
1. Usi-generalize kwamba sisi watanzania hatuna utaratibu wa kulipa tunapokopa. Ni kweli wewe haukopesheki??? Ukikopa huwa haurejeshi??
2. Haya mabenki mbona yameweza kutukopesha tena kwa barua ya mwajiri tu na kasalare slip kako. Hizi foleni unazoziona zinazidi kila siku ni kwa sababu leo hii mtanzania anaweza kupata mkopo wa 10m ndani ya 24hrs.

Hofu yangu kama ilivyo ya wengi ni juu ya ajenda iliyo nyuma ya hii miradi maana hakuna wa kumwamini (siasa kila mahali).
Kama ni swala la miradi Shirika la Maendeleo (NDC) kazi yake nini???
NSSF kama wanahela kibao watukopeshe wanachama kwanza, mfuko ni wa wanachama ambao ni sehemu ndogo sana ya watanzania. Mwenye wajibu wa kujenga hiyo miundo mbinu ni serikali maana pesa wanayo tatizo hakuna wenye kuwaza kizazi cha kesho.

Heshima yako mkuu, Nadhani tunajua kuwa kuna wanachama wanasiasa waliokopeshwa na mpaka sasa wanadaiwa nisingependa kutaja majina hapa ila kwa ufupi pesa zile hazijarejeshwa na kama zimerejeshwa basi hazijamalizika! Kuhusu investments wanazozisimamia NSSF sina tatizo ilimradi tu ziwe na return of investment na pay back period yake isiwe ya miaka mingi naamini umeme ni investment inayolipa kwa barabara nadhani hapo wamechemka ila pia hizo barabara zitachochea ukuaji wa uchumi kwa wanachama pia. Tatizo lililopo linaweza likawa hatuwaamini watanzania wenzetu tunataka tuone wazungu ndio tuwaamini! Tuwape nafasi maana wanasiasa wameshindwa ila tuwape angalizo miradi yao isiingiliwe na siasa!
 
Nimesoma hiyo document ya Pension Watch pekee (kudownload inakula credit). Angalau nimepata point chache.

We do not have policy and regulations for such joint venture between gov and pension funds, do we?
How was the decision that NSSF should invest in these projects reached, transparency, competative bidding, and participation of members?
Has NSSF done analysis of its ability to engage in these risky ventures and do they have ways to mitigate any unforsee and forsee risks?
 
Nimesoma hiyo document ya Pension Watch pekee (kudownload inakula credit). Angalau nimepata point chache.

We do not have policy and regulations for such joint venture between gov and pension funds, do we?
How was the decision that NSSF should invest in these projects reached, transparency, competative bidding, and participation of members?
Has NSSF done analysis of its ability to engage in these risky ventures and do they have ways to mitigate any unforsee and forsee risks?

Now we are talking; kwa sababu kufanikiwa kwa uwekezaji kaam huu unahitaji mabadiliko ya miundo na hata sheria mbalimbali; kunahitaji uwajibika, uwazi, na ushirikishwaji wa wanachama. Lakini vile vile kunahitajika mjadala wa kina wa kuelewa uwekezaji huu utafanyika vipi na utaathiri vipi mafao mbalimbali ya wafanyakazi.
 
Now we are talking; kwa sababu kufanikiwa kwa uwekezaji kaam huu unahitaji mabadiliko ya miundo na hata sheria mbalimbali; kunahitaji uwajibika, uwazi, na ushirikishwaji wa wanachama. Lakini vile vile kunahitajika mjadala wa kina wa kuelewa uwekezaji huu utafanyika vipi na utaathiri vipi mafao mbalimbali ya wafanyakazi.
watu humu ndani wanachekelea tu hii miradi bila kujua kinachofanyika tanzania ni impunity, impunity, impunity! Miradi inabuniwa ili ku-siphon hela za wanachama wa Pension nashangaa hamna watu wanajua hii miradi na wala hamna watu walio na uelewa wa risks za hii miradi na thamani halisi na faida zitokanazo na hii miradi yaani neutral individuals like International consultancies!
 
watu humu ndani wanachekelea tu hii miradi bila kujua kinachofanyika tanzania ni impunity, impunity, impunity! Miradi inabuniwa ili ku-siphon hela za wanachama wa Pension nashangaa hamna watu wanajua hii miradi na wala hamna watu walio na uelewa wa risks za hii miradi na thamani halisi na faida zitokanazo na hii miradi yaani neutral individuals like International consultancies!

Mkuu uzoefu wangu kuhusu hapo kwenye red ni negative sana, saaaana. Hawa watu kazi yao ya kwanza ni kukuwadia nchi zao na kampuni za kwao. pengine kama ningeulizwa maoni yangu kuhusu independent consultant ningesema ni sisi wananchi wenyewe, kati yetu wamo wenye integrity na uzalendo. Watu kama J Ulimwengu, Shivji. watu ambao hawahongeki na misimamo yao haichuji wala kupepesuka. Inawezekana kuna wengine lakini hao wawili pekee ndio mimi nimewapitisha, kwa subjectivity yangu!
 
Mkuu uzoefu wangu kuhusu hapo kwenye red ni negative sana, saaaana. Hawa watu kazi yao ya kwanza ni kukuwadia nchi zao na kampuni za kwao. pengine kama ningeulizwa maoni yangu kuhusu independent consultant ningesema ni sisi wananchi wenyewe, kati yetu wamo wenye integrity na uzalendo. Watu kama J Ulimwengu, Shivji. watu ambao hawahongeki na misimamo yao haichuji wala kupepesuka. Inawezekana kuna wengine lakini hao wawili pekee ndio mimi nimewapitisha, kwa subjectivity yangu!
acha politics za "sisi wananchi" wakati hata haki ya kupiga kura hatujui simple civic rights zinatushinda! halafu miradi ikibuma watashitaki nani? hizo International consultancies zina reputation za kufanya kazi sehemu mbalimbali ila wanapokuja katika nchi za mijizi kama hii inabidi wamtumikie punda yaani kufuata matakwa ya serikali katika wizi la sivyo wanakosa tenda lakini still si consultancies zote bado zipo ambazo ku-maintain good reputation means a lot to them!
 
Mkuu uzoefu wangu kuhusu hapo kwenye red ni negative sana, saaaana. Hawa watu kazi yao ya kwanza ni kukuwadia nchi zao na kampuni za kwao. pengine kama ningeulizwa maoni yangu kuhusu independent consultant ningesema ni sisi wananchi wenyewe, kati yetu wamo wenye integrity na uzalendo. Watu kama J Ulimwengu, Shivji. watu ambao hawahongeki na misimamo yao haichuji wala kupepesuka. Inawezekana kuna wengine lakini hao wawili pekee ndio mimi nimewapitisha, kwa subjectivity yangu!

mkuu..Gurudumu... umetuletea thread kule kwenye Business and Economy halafu umekimbia... rudi nyumba ndogo bana
 
Miradi ya NSSF chini ya Dr Dau inanipa shaka sana kufuatia mosi jinsi Manji alivyoweza kutajirika haraka sana na hili shirika. Vile vile NSSF kutokuwa waangalifu na kusababisha vifo vya watoto kule Tabora kwenye miradi yao na hakuna hata aliyewajibika au kuwajibishwa. Hatuwezi kuwaamini katika makubwa wakati wameshindwa madogo. Ikumbukwe ni hawa hawa NSSF ambao walikuwa wanamipamgo sijui niite ya Bulicheka kwenda ku-invest nje ya nchi wakati miradi midogo inawashinda hapa nyumbani. WAACHENI waendelee lakini hicho ndio kifo cha NSSF.
 
Back
Top Bottom