Cantalisia
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 5,222
- 2,925
- Thread starter
- #61
Uko sahihi kbs happy,ameshalitambua hilo na kwa sasa anasema anapumzika kwanza ajipe mda wa kutosha kujiangalie yeye na kurekebisha mapungufu yake kabla hajajiingiza kwenye uhusiano mpya?Mapenzi ni matamu sana. Hasa ukipata anayeyajulia, mkweli, mwaminifu na muelewa. Inakupasa uwe mwangalifu sana kabla hujajiingiza kwenye mapenzi. Ukikosea wakati wa kuchagua na kuamua elewa hutaweza kukwepa maumivu ya mapenzi siku za mbele. Mueleze huyo shost, afute akilini mwake kama aliwahi kupenda. Ajiandae upya kiakili kujifikiria yeye mwenyewe kwanza yukoje kimapenzi na afikirie ni mpenzi gani atamfaa kulingana na yeye alivyo. Akishajitambua alivyo itakuwa ni rahisi kupata sifa za anayemuhitaji.
Awe mwangalifu wakati wa kumchunguza mpenzi anayemtaka. Asiwe mtu wa makuu sana, aelewe hakuna binadamu aliyekamilika, ila kuna tabia ambazo zinaweza kuvumilika/kuchukulika. Endapo kuna tabia yoyote ambayo anahisi hataweza kuivumilia asikubali kujiingiza kwenye mapenzi akitegemea mtu yule ataiacha au kubadilika.
Aanze kuchagua kulingana na sifa anazozitaka. Mwambie awe mwangalifu sana wakati wa kuchagua, na asiwe na papara. Ajifunze kuutuliza moyo wake, maana wakati mwingine mioyo yetu hutuharakisha kuamua na kujikuta tunajuta.
Atulieze akili zake kwa kufanya mazoezi, kula vizuri, kulala mapema, kufurahi na marafiki na kuhakikisha anachangamka, mapenzi yasimfaye alie na kuwaza hadi akose hamu ya chakula. Hii itampelekea kutokuwa na maamuzi mazuri.