No half Revolutions: Resignation or dissolution is not enough; The parliament should go too

Back to square one.
Hatujamwajiri rais wetu. Katiba yetu haituwezeshi sisi kumwajiri rais.Hatuwezi hata kumwondoa, the same system ipo kwenye vyama mbadala, kuna watawala na wengineo ni watwana. Hata ukiamua kugombea nafasi fulani huruhusiwi kwa sababu wewe ni mtwana. Sasa hiyo ndiyo tuiondoe.
Tunapenda kujiaminisha kuwa tumewaajiri hawa wanasiasa ilhali hao ndio wametuajiri tuwafanyie kazi na kuwatajirisha. Dah!! aliyegundua pilau ana akili kuliko Einstein.
Labda una maana hatujaamua kumuondoa! kuweza kumuondoa tunaweza kabisa. Wakati wa kampeni katiba yetu ilielekeza kuwa wagombea waende kwa wananchi waombe ridhaa. Ridhaa maana yake waombe ajira!

Kumbu kumbu zangu zinaonyesha orange revolution kule Ukraine(kama nipo sahihi) ni matokeo ya waajiri kuiweka kando katiba kwanza ili washughulike na tatizo halafu walirudi kutengeneza katiba.
Kuna kitu kinaitwa 'radical therapy' hasa pale 'conventional therapy' inaposhindwa. Je, si wakati sasa wa kuwa na radical therapy!

Tatizo la Watanzania ni kutojiamini na kuamini kuwa hawawezi. Hapo wajanja wanatumia udhaifu wetu kuleta hadithi, ngano na mashairi. Ndiyo maana tunadanganywa na maneno mchakato, linazungumzika, amani na utulivu, wasikivu,wazee wa Dar n.k.
 
Nadhani watu wengine hawajasoma nilichoandika; mimi si muamini wa mapinduzi ya umwagikaji damu naamini katika mapinduzi ya kidemokrasia. Mapinduzi ya kidemokrasia ni mabadiliko ya haraka, ya jumla ya uongozi wa kisiasa kutoka chama kimoja kwenda kingine na kubadilisha kabisa namna ya utawala. Ndio maana nimesema siamini katika 'half a revoution" yaani kwa mfano kulazimisha WM ang'oke au mawaziri au hata baraza la mawaziri kuvunjika; mimi ninaamini katika kusababisha uongozi mzima wa chama kimoja kung'olewa ili kupisha uchaguzi mwingine mapema zaidi. Siamini kama taifa linahitaji kuvumilia hadi 2015!
 
Nadhani watu wengine hawajasoma nilichoandika; mimi si muamini wa mapinduzi ya umwagikaji damu naamini katika mapinduzi ya kidemokrasia. Mapinduzi ya kidemokrasia ni mabadiliko ya haraka, ya jumla ya uongozi wa kisiasa kutoka chama kimoja kwenda kingine na kubadilisha kabisa namna ya utawala. Ndio maana nimesema siamini katika 'half a revoution" yaani kwa mfano kulazimisha WM ang'oke au mawaziri au hata baraza la mawaziri kuvunjika; mimi ninaamini katika kusababisha uongozi mzima wa chama kimoja kung'olewa ili kupisha uchaguzi mwingine mapema zaidi. Siamini kama taifa linahitaji kuvumilia hadi 2015!
Mkuu MM, mara nyingi mapinduzi ya damu yanatokea pale ya kidemokrasia yanapoonekana kutozaa matunda. Baada ya kusema hivyo bado siamini katika mapinduzi ya umwagaji damu asilani.

Mabadiliko ya lazima si mapinduzi ya umwagaji damu. Mapinduzi ya umwagaji damu ni yale ya siri yanayopangwa na kikundi au kundi fulani. Mabadiliko ya lazima ni yale yanayotoa fursa ya majadiliano yakiambatana na shinikizo.

Misri wamesubiri miaka 50 hatimaye wakalazimisha mabadiliko ya lazima. Walitoa fursa kwa Mubarak kuwaachia nchi yao na pale alipoleta ujeuri ndipo 'radical therapy' ikatumika. Radical therapy si nzuri lakini kuna wakati inabidi ili kumsaidia mgonjwa.

Uporaji wa mali ya umma uliokuwepo miaka ya 70,80 na hata 90 si kama tunaoushuhudia. Siku hizi ni halali kupora halafu unastaafishwa ili usimamie miradi yako iliyotokana na pesa zetu kwa utulivu (mwacheni apunzike mzee wa watu).

Kinachotia ghadhabu ni pale kundi la waporaji linapowafanya Watanzania kama mazezeta. Ndiyo ya Pinda kusema atatoa tamko la mali zetu Jumatatu na mwishowe kuishia na hadithi za ushindi wa Simba Algeria.

Kama mapinduzi ya kidemkrasia yanafanya kazi basi tungeona japo dalili.
Tufikirie kuwa Waziri mwenye dhamana ya ulinzi yupo madarakani huku mauaji ya kizembe ya mabomu yametokea. Ok! Japo basi tuambiwe nani alizembea, hilo halikufanyika kama tulivyoachwa gizani na Kagoda, Meremeta, Richmond n.k

Ikifika hapo nasita kuamini kuwa kuna njia ya mkato. Katika historia ya nchi yetu hakuna Rais aliyewahi kuonja hasira za wananchi. Ni kwasababu hiyo, Rais ambaye hupewa 'briefing' za nchi kila asubuhi amefika mahali pa kusema alikuwa ziarani na hajui nini kinaendelea nchi mwake. Dharau ya namna hii haiwezi kukubali mapinduzi ya kidemokrasia. Ni dharau iliyofikia upeo wa juu sana.

Wakati umefika Wananchi bila kujali itikadi zao za kijamii, na bila kubeba jiwe, fimbo au sindano tusimame kwa pamoja na tuwaambie hawa wanaotupora, tunajua wanatupora lakini sasa tumechoka. Tumechoka na tunahitaji mabadiliko.

Tusimame waone nyuso zetu zilivyosawajika kwa uonevu, sinyaa kwa majonzi na zinazofuka moshi wa hasira. Tuwape nafasi ya wao kujitahmini wakiwa wameziangalia nyuso zetu ili waone njia panda tuliyosimama.
 
Mapinduzi kimsingi ni "mabadiliko makubwa, ya haraka na yenye kulazimishwa". Yapo mapinduzi ya kijeshi - ambapo jeshi linaingia kati na kulazimisha mabadiliko na yapo mapinduzi baridi ya wananchi ambapo wananchi wanawatimua watawala wao (tumeona Georgia, Ukraine, Misri n.k) na yapo mapinduzi ya demokrasia ambapo chama kilichoko madarakani kinaondolewa in one clean sweep kwa kutumia sanduku la kura. Ndivyo kilivyoondolewa Chama cha Mapinduzi cha Mexico na chama tawala cha Indonesia. Yanapotokea mabadiliko hayo makubwa kwa njia ya demokrasia basi ndio mapinduzi ya demokrasia.

Ninaamin kabisa sasa hivi TZ ipo kwenye mkesha wa kuamkia siku hiyo kama nilivyoandika kwenye "Unabii Utatimia". Watanzania wataibadilisha CCM mara moja. Tayari tumeona wakiibadili pole pole kila kona ya Tanzania. Pole pole wanaanza kuthubutu kuikataa sema mfumo wetu hauruhusu mabadiliko ya haraka ndio maana naamini kuvunjwa kwa bunge sasa hivi na watu warudi kwa wananchi kutaleta boost nyingine ya kuzidi kuwaondoa watawala hawa walioshindwa.
 
Back
Top Bottom