Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nisaidien wana jf nna nyumba natumia kama dhamana nipate mkopo wa mil.6 wapi ni bank nzuri,naweza pata huu mkopo mapema kwa mashart nafuu.
Nyumba zenye hati ya makazi au title yaani ya kudumu nilisikia wanapata mikopo ya ujenzi au ukarabati, hivyo ndugu utaiweka kama dhamana kutoka Azania bank. ila nao naona itabidi uwaridhishe jinsi gani unarudisha mkopo wao kwa either salary pay slip au biashara leseni/ tin. Mkopo huu sidhani kama ni wa dharura itawachukua muda upate jaribu kuwatembelea.
Habari mkuu, kwanza napenda kukujuza kuwa, kwenye uombaji mikopo mara nyingi wanaangalia shughuli unayoifanya ambayo ndio inayokuingizia kipato (uwe umeajiriwa ama umejiajiri), na kiasi unachoweza kupewa kinategemea na dhumuni la mkopo, kipato chako, historia yako ya ukopaji, kumbukumbu zako na dhamana zako. Ila si kwamba ukiwa na dhamana yenye thamani kubwa peke yake ndio kwamba utaweza kupata mkopo. Na masharti nafuu ya mikopo ni pamoja na riba ndogo, muda wezeshi kwa mteja kuweza kulipa, uhakika na uharaka wa huduma bora za utoaji mikopo. Hivyo nakushauri upitie Bank na taasisi mbalimbali za mikopo kuangalia vitu hivyo ili uweze kujua ipi ni nafuu kwako.
Recommended: FINCA, Advans Bank, Akiba Commercial Bank.
Kama tayari una biashara nenda Access Bank Au Akiba Commercial Bank pia Stanbic kariakoo. Kwa kiasi unachotaka huko utapata, kama ndo unataka kuanza biashara sio rahisi kupata mkopo bank ukafungulie biashara wanataka biashara uwe umeshafanya angalau kwa miezi sita bank statement watahitaji.