Nna nyumba nataka mkopo wa biashara bank gan na weza pata mkopo haraka na kwa riba ndogo.

frnk

Senior Member
Jun 19, 2012
160
12
Nisaidien wana jf nna nyumba natumia kama dhamana nipate mkopo wa mil.6 wapi ni bank nzuri,naweza pata huu mkopo mapema kwa mashart nafuu.
 
Asante kwa swali lako ukipata jibu na mimi ntakuwa nimefaidika nina shida kama yyako
 
Nisaidien wana jf nna nyumba natumia kama dhamana nipate mkopo wa mil.6 wapi ni bank nzuri,naweza pata huu mkopo mapema kwa mashart nafuu.

Kama tayari una biashara nenda Access Bank Au Akiba Commercial Bank pia Stanbic kariakoo. Kwa kiasi unachotaka huko utapata, kama ndo unataka kuanza biashara sio rahisi kupata mkopo bank ukafungulie biashara wanataka biashara uwe umeshafanya angalau kwa miezi sita bank statement watahitaji.
 
Habari mkuu, kwanza napenda kukujuza kuwa, kwenye uombaji mikopo mara nyingi wanaangalia shughuli unayoifanya ambayo ndio inayokuingizia kipato (uwe umeajiriwa ama umejiajiri), na kiasi unachoweza kupewa kinategemea na dhumuni la mkopo, kipato chako, historia yako ya ukopaji, kumbukumbu zako na dhamana zako. Ila si kwamba ukiwa na dhamana yenye thamani kubwa peke yake ndio kwamba utaweza kupata mkopo. Na masharti nafuu ya mikopo ni pamoja na riba ndogo, muda wezeshi kwa mteja kuweza kulipa, uhakika na uharaka wa huduma bora za utoaji mikopo. Hivyo nakushauri upitie Bank na taasisi mbalimbali za mikopo kuangalia vitu hivyo ili uweze kujua ipi ni nafuu kwako.
Recommended: FINCA, Advans Bank, Akiba Commercial Bank.
 
Nyumba zenye hati ya makazi au title yaani ya kudumu nilisikia wanapata mikopo ya ujenzi au ukarabati, hivyo ndugu utaiweka kama dhamana kutoka Azania bank. ila nao naona itabidi uwaridhishe jinsi gani unarudisha mkopo wao kwa either salary pay slip au biashara leseni/ tin. Mkopo huu sidhani kama ni wa dharura itawachukua muda upate jaribu kuwatembelea.
 
Nyumba zenye hati ya makazi au title yaani ya kudumu nilisikia wanapata mikopo ya ujenzi au ukarabati, hivyo ndugu utaiweka kama dhamana kutoka Azania bank. ila nao naona itabidi uwaridhishe jinsi gani unarudisha mkopo wao kwa either salary pay slip au biashara leseni/ tin. Mkopo huu sidhani kama ni wa dharura itawachukua muda upate jaribu kuwatembelea.

Nashukuru sana,umenipa mwanga mzuri,.
 
Habari mkuu, kwanza napenda kukujuza kuwa, kwenye uombaji mikopo mara nyingi wanaangalia shughuli unayoifanya ambayo ndio inayokuingizia kipato (uwe umeajiriwa ama umejiajiri), na kiasi unachoweza kupewa kinategemea na dhumuni la mkopo, kipato chako, historia yako ya ukopaji, kumbukumbu zako na dhamana zako. Ila si kwamba ukiwa na dhamana yenye thamani kubwa peke yake ndio kwamba utaweza kupata mkopo. Na masharti nafuu ya mikopo ni pamoja na riba ndogo, muda wezeshi kwa mteja kuweza kulipa, uhakika na uharaka wa huduma bora za utoaji mikopo. Hivyo nakushauri upitie Bank na taasisi mbalimbali za mikopo kuangalia vitu hivyo ili uweze kujua ipi ni nafuu kwako.
Recommended: FINCA, Advans Bank, Akiba Commercial Bank.

Nimekupata mkuu,nashukuru sana kwa maelezo yako yaliyojitosheleza,ngoja niwaone,
 
Kama tayari una biashara nenda Access Bank Au Akiba Commercial Bank pia Stanbic kariakoo. Kwa kiasi unachotaka huko utapata, kama ndo unataka kuanza biashara sio rahisi kupata mkopo bank ukafungulie biashara wanataka biashara uwe umeshafanya angalau kwa miezi sita bank statement watahitaji.

Nashukuru sana,biashara ambayo nafanya nina gar moja(tax) ingawaje ni tax bubu,haijapgwa mkanda,na nimekua niikafanya kwa mda sasa,bia mim ni benefitial wa mfuko wa pspf kama msimamiz wa mirath,hvyo kwa mwaka hua napokea jumla ya mil.3 ambayo nimepanga nikapewa mkopo wa mil.6 nikanunua gar ambayo kwa mwez italeta lak 4.,hvyo ile pensen yangu ya mil.3 itakua kma security ya kupeleka bank yote,then katika lak 4 ya tax nitatoa lak 2 then kwa mwaka itakua ni mil.2.4 plus mil.3 ni kama mil.5.4 ambayo nitaweza ipeleka bank within a year.hvyo kama wakinipa mda wa 2 yrs ,na iman ntakua nimelipa hela bila utata kabisa.mnaonaje hapo wadau.mnisaidiaje mawazo maana mi taaluma yangu ni mwanasheria.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom