PayGod
JF-Expert Member
- Mar 4, 2008
- 1,259
- 57
BENKI ya NMB imezindua huduma mpya ya Pesa Fasta itakayomuwezesha mteja kuchukua fedha kwenye mashine za NMB popote bila kuwa na kadi wala akaunti.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Mark Wiessing amezindua huduma hiyo leo Dar es Salaam na kuongeza kuwa, huduma hiyo ni rahisi , ya haraka na yenye kutoa suluhu la soko la huduma za kibenki.
Kufikia huduma za fedha ni moja ya changamoto ambayo wasimamizi wakuu kama BoT pamoja na benki nyingine kama NMB wanakabiliana nazo nchini pamoja na nchi nyingine, alisema Wiessing.
Amesema, kuzinduliwa kwa huduma ya Pesa Fasta itasaidia idadi kubwa ya Watanzania ambao hawakuwa na huduma za benki kupata huduma hizo ambapo kuanzia sasa watakuwa na upeo mkubwa wa kupokea fedha kupitia mashine za ATM za NMB.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano cha NMB, Imani Kajula alisema faida za NMB Pesa Fasta haihitaji kuwa na akaunti, haihitaji kuwa na kadi ya NMB ATM, hakuna makato ya mwezi, mhusika anaweza kuchukua fedha kwenye ATM zaidi ya 400 na huduma hiyo inapatikana kwa saa 24.
Amesema, jinsi ya kutuma fedha kutumia simu yako ya mkononi kwa huduma ya Pesa Fasta ni kupiga *150*66# na kisha kufuata maelekezo zaidi ambapo mteja anaweza kutuma au kupokea hadi Sh 200,000 kwa siku.
Aidha, Kajula amesema, huduma hiyo pia itamwezesha mteja kuangalia salio, kutuma fedha kwenda kwenye akaunti ya NMB, kununua LUKU au muda wa maongezi au kupata taarifa fupi.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Mark Wiessing amezindua huduma hiyo leo Dar es Salaam na kuongeza kuwa, huduma hiyo ni rahisi , ya haraka na yenye kutoa suluhu la soko la huduma za kibenki.
Kufikia huduma za fedha ni moja ya changamoto ambayo wasimamizi wakuu kama BoT pamoja na benki nyingine kama NMB wanakabiliana nazo nchini pamoja na nchi nyingine, alisema Wiessing.
Amesema, kuzinduliwa kwa huduma ya Pesa Fasta itasaidia idadi kubwa ya Watanzania ambao hawakuwa na huduma za benki kupata huduma hizo ambapo kuanzia sasa watakuwa na upeo mkubwa wa kupokea fedha kupitia mashine za ATM za NMB.
Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano cha NMB, Imani Kajula alisema faida za NMB Pesa Fasta haihitaji kuwa na akaunti, haihitaji kuwa na kadi ya NMB ATM, hakuna makato ya mwezi, mhusika anaweza kuchukua fedha kwenye ATM zaidi ya 400 na huduma hiyo inapatikana kwa saa 24.
Amesema, jinsi ya kutuma fedha kutumia simu yako ya mkononi kwa huduma ya Pesa Fasta ni kupiga *150*66# na kisha kufuata maelekezo zaidi ambapo mteja anaweza kutuma au kupokea hadi Sh 200,000 kwa siku.
Aidha, Kajula amesema, huduma hiyo pia itamwezesha mteja kuangalia salio, kutuma fedha kwenda kwenye akaunti ya NMB, kununua LUKU au muda wa maongezi au kupata taarifa fupi.