NMB yaja na Pesa Fasta

PayGod

JF-Expert Member
Mar 4, 2008
1,259
57
BENKI ya NMB imezindua huduma mpya ya Pesa Fasta itakayomuwezesha mteja kuchukua fedha kwenye mashine za NMB popote bila kuwa na kadi wala akaunti.

Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Mark Wiessing amezindua huduma hiyo leo Dar es Salaam na kuongeza kuwa, huduma hiyo ni rahisi , ya haraka na yenye kutoa suluhu la soko la huduma za kibenki.

“Kufikia huduma za fedha ni moja ya changamoto ambayo wasimamizi wakuu kama BoT pamoja na benki nyingine kama NMB wanakabiliana nazo nchini pamoja na nchi nyingine,” alisema Wiessing.

Amesema, kuzinduliwa kwa huduma ya Pesa Fasta itasaidia idadi kubwa ya Watanzania ambao hawakuwa na huduma za benki kupata huduma hizo ambapo kuanzia sasa watakuwa na upeo mkubwa wa kupokea fedha kupitia mashine za ATM za NMB.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano cha NMB, Imani Kajula alisema faida za NMB Pesa Fasta haihitaji kuwa na akaunti, haihitaji kuwa na kadi ya NMB ATM, hakuna makato ya mwezi, mhusika anaweza kuchukua fedha kwenye ATM zaidi ya 400 na huduma hiyo inapatikana kwa saa 24.

Amesema, jinsi ya kutuma fedha kutumia simu yako ya mkononi kwa huduma ya Pesa Fasta ni kupiga *150*66# na kisha kufuata maelekezo zaidi ambapo mteja anaweza kutuma au kupokea hadi Sh 200,000 kwa siku.

Aidha, Kajula amesema, huduma hiyo pia itamwezesha mteja kuangalia salio, kutuma fedha kwenda kwenye akaunti ya NMB, kununua LUKU au muda wa maongezi au kupata taarifa fupi.
 
hizo pesa unatoa vp kama huna akaunt number wala ATM card

ukiwa kwenye atm yoyote ya NMB BONYEZA TOP RIGHT HAND BUTTON, kisha fuata maelekezo, ambayo yatakuhitaji kuingiza namba mbili za siri na na kiasi ulichotumiwa, na utapata fedha yako
 
ukiwa kwenye atm yoyote ya NMB BONYEZA TOP RIGHT HAND BUTTON, kisha fuata maelekezo, ambayo yatakuhitaji kuingiza namba mbili za siri na na kiasi ulichotumiwa, na utapata fedha yako

that means you must register for this service therefore there is nothing new .... just like m-pesa though the cash points are ATM'S ....isn't it ..?
 
NMB PesaFasta Launch


Today NMB has introduced NMB PesaFasta a new money transfer service that enables NMB mobile customers to send money to beneficiaries who don't have bank Account.NMB PesaFasta recipients will be able to withdraw transferred amount from NMB ATM anywhere in Tanzania. The launch of NMB PesaFasta is a continuation of NMB commitment in improving service delivery to customers
2.JPG
NMB CEO Mark Wiessing unveiling NMB PesaFasta, with him (from right) is Financial Sector Deepening Trust (FSDT) Technical Director Sosthenis Kewe and NMB Head of Personal Banking Abdulmajid Nsekela.
Speaking during the launch of NMB PesaFasta that was held in Dar es Salaam, NMB CEO Mark Wiessing said "NMB is delighted to announce the creation of NMB PesaFasta unique service which allows any NMB mobile customers to send money to beneficiaries who do not have yet a bank Account. This will allow these unbanked Tanzanians to start getting access to the normal banking system".
transaction.JPG
















Financial Sector Deepening Trust (FSDT) Technical Director Sosthenis Kewe and NMB Relationship Manager Neema Kassim making transactions through NMB PesaFasta.
Mr. Wiessing added "NMB PesaFasta is designed to be an affordable, reliable and convenient solution for our target market, including the so-called unbanked. A cheaper, better and faster money transfer service that uses NMB's leadership in technology".
Speaking on behalf of NMB partners, Financial Sector Deepening Trust (FSDT) Technical Director Mr. Sosthenis Kewe, congratulated NMB for being a strong partner in bringing financial services to the unbanked.
From now onwards you can access NMB PesaFasta service by dialing *150*66#
 
that means you must register for this service therefore there is nothing new .... just like m-pesa though the cash points are ATM'S ....isn't it ..?

Mtumaji lazima awe mteja wa NMB na ajisajili na nmb mobile ila mpokeaji anachotakiwa awe na simu ya mkononi tu.
 
  • Thanks
Reactions: LAT
Wangeshugulika kwanza na namna ya kupunguza msongamano kwenye benki zao, maana hii huduma kama inakuhitaji uende kwenye benk zao, utakuwa msalaba. kwa wanaojua hii benki wanajua ninachomaanisha. foleni kila mahali hata kujua salio, unakaa foleni masaa wee bila kuhudumiwa.
 
that means you must register for this service therefore there is nothing new .... just like m-pesa though the cash points are ATM'S ....isn't it ..?
Anayetumiwa haitaji kujisajili, ila mtumaji lazima awe na akaunti ya nmb. Inabidi waboreshe atm mashine zao ili hii huduma iwe nzuri!
 
  • Thanks
Reactions: LAT
BENKI ya NMB imezindua huduma mpya ya Pesa Fasta itakayomuwezesha mteja kuchukua fedha kwenye mashine za NMB popote bila kuwa na kadi wala akaunti.

Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Mark Wiessing amezindua huduma hiyo leo Dar es Salaam na kuongeza kuwa, huduma hiyo ni rahisi , ya haraka na yenye kutoa suluhu la soko la huduma za kibenki.

Kufikia huduma za fedha ni moja ya changamoto ambayo wasimamizi wakuu kama BoT pamoja na benki nyingine kama NMB wanakabiliana nazo nchini pamoja na nchi nyingine, alisema Wiessing.

Amesema, kuzinduliwa kwa huduma ya Pesa Fasta itasaidia idadi kubwa ya Watanzania ambao hawakuwa na huduma za benki kupata huduma hizo ambapo kuanzia sasa watakuwa na upeo mkubwa wa kupokea fedha kupitia mashine za ATM za NMB.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Masoko na Mawasiliano cha NMB, Imani Kajula alisema faida za NMB Pesa Fasta haihitaji kuwa na akaunti, haihitaji kuwa na kadi ya NMB ATM, hakuna makato ya mwezi, mhusika anaweza kuchukua fedha kwenye ATM zaidi ya 400 na huduma hiyo inapatikana kwa saa 24.

Amesema, jinsi ya kutuma fedha kutumia simu yako ya mkononi kwa huduma ya Pesa Fasta ni kupiga *150*66# na kisha kufuata maelekezo zaidi ambapo mteja anaweza kutuma au kupokea hadi Sh 200,000 kwa siku.

Aidha, Kajula amesema, huduma hiyo pia itamwezesha mteja kuangalia salio, kutuma fedha kwenda kwenye akaunti ya NMB, kununua LUKU au muda wa maongezi au kupata taarifa fupi.
Mie nlikua nataka munisaidie jinsi ya kujitoa kwenye huduma hii maana unakopa alafu siku za kulipa unapewa kidogo kwakweli ni shida
 
Back
Top Bottom