NMB wanaboa

Ambassador

JF-Expert Member
Jun 2, 2008
933
75
Leo shemeji/wifi yenu kaenda tawi moja la NMB jijini kuuliza taratibu za kufungua akaunti kwa ajili ya watoto akaambiwa apeleke fomu toka serikali za mitaa zenye picha ya kila mtoto na mama, pamoja na kopi za vyeti vya kuzaliwa. Wife akahangaika kupata docs na kuziwasilisha NMB akaambiwa vinatakiwa vyeti original pamoja na copy. Aliporudi na hizo original akaambiwa picha yake kwenye fomu masikio hayaonekani akapige nyingine!

Kilichofuata? Wife alikasirika na akaelekea CRDB. Huko akapewa fomu na kuambiwa apate sahihi za wadhamini wawili wenye akaunti CRDB, alete kopi za vyeti vya kuzaliwa na kitambulisho chake na mchezo ukaisha!

La kujiuliza hapa, kwa nini NMB hawakukagua vema hizo fomu na kutambua makosa yote ili wife asirudi mara mbilimbili? Na kwa nini hawakumpa maelezo ya kutosha mwanzoni kwamba waltaka original? Kwa kupoteza wateja watarajiwa wanne kwa wakati mmoja hii kwao sio issue kwa kuwa ni watoto na hawana pesa ya kuweka benki? Ofcourse kama wazazi wanojali tumeamua kuwafungulia akaunti ili kuwawekea akiba itakayowasaidia hapo baadae na lazima akaunti zao ziwe operational.

Kwa ndugu zangu wa NMB, wekeni taratibu zinazoeleweka na rahisi kwa wateja wenu ili kuepuka usumbufu na kujipotezea wateja. Onyesheni kwamba ninyi ni benki ya wananchi kweli. Au ndo mmebweteka? Shauri lenu...!!
 
kwanza hiyo misururu ya wateja wao kila siku umeiona....mimi hata kwa mtutu sifungui account pale
 
Tatizo ni watoa huduma wao, wamejaza form siks liva ambao hawana noleji yoyote ya kastomakea!!!!
Juzi nilikuwa TRA kupata TIN, mhudumu anauliza kwa senior wake "hivi passport nayo ni sawa na kitambulisho cha mpiga kura?!!!!!". Kitambulisho anachokijua yeye ni cha mpiga kura tu na barua ya mwenyekiti wa mtaa!!
 
Tatizo kubwa la Watoa Huduma wengi wa Tanzania ni kwamba wanaona wanakufanyia favor fulani hivi kwa kukupa hiyo huduma husika, potelea mbali kwamba unailipia, na sio kwamba wewe ndio unawafanyia favor kwa kufuata huduma yao wao na kuwaacha wengine!!
 
Tuna matatizo mengi sana kwenye maofisi yetu haya! customer care ni zero, angalia hata ukienda bar, restaurants, hotelini, sehemu nyingi za biashara wana matatizo makubwa kwenye customer care.
NMB wanaboa ile mbaya, NBC bao wanaboa pia, CRDB wako safi. We need to change the way of recruiting employee, siyo kumchukua mfanyakazi bila hata kumpa customer care training mnajidai mko busy matokeo yako hasara, akishaganga njaa basi anakuwa boss badala ya kutafuta namna ya kupata hela kutoka kwa wateja, wanafukuza wateja. Hapo ndo nachoka hapo.
 
Hata hapo CRDB panaboa. Ikiwa serikali ya mtaa imekudhamini, una original goverment document kama vyeti vya kuzaliwa, wadhamini wawili wenye account crdb wa nini?
 
asante sana mkuu kwa kuiweka hii kero wazi,,unajua hiyo ni moja,,mimi nilikuwa nafikiri itakuwa hii ya misururu tu..kumbe kuna mengine!!! hawa jamaa mimi najiuliza hivi sababu ni nini?? kwamba pesa zimejaa?? au sisi wateja hatuna pakukimbilia pengine,jamani ule muda ninaopoteza kwenye fuleni yao huwa naahirisha mambo mengine yote...JAMANI MIMI KUFUNGUA ACCOUNT NMB tena itakuwa ndoto isiyotimia..nasikitika tu sikuzote...mfalme wa biashara siku zote ni mteja,,inakuwaje hawa jamaa!!!!!!!!!!!
 
Hivi hawa wanelewa banking ni nini ? Mtu unawapa hela zako wakuwekee, na hivyo kuwapa hela za kukopesha watu wengine na kupata interest, halafu wanakupa tabu hivi ?

Au ndiyo kusema soko huru na mashindano ya kibiashara Tanzania bado ?
 
jamani mie mwanichoma maana huko ndo wife anakopiga kazi atiiiii
 
Hata hapo CRDB panaboa. Ikiwa serikali ya mtaa imekudhamini, una original goverment document kama vyeti vya kuzaliwa, wadhamini wawili wenye account crdb wa nini?
CRDB hawahitaji udhamini wa serikali za mitaa
 
asante sana mkuu kwa kuiweka hii kero wazi,,unajua hiyo ni moja,,mimi nilikuwa nafikiri itakuwa hii ya misururu tu..kumbe kuna mengine!!! hawa jamaa mimi najiuliza hivi sababu ni nini?? kwamba pesa zimejaa?? au sisi wateja hatuna pakukimbilia pengine,jamani ule muda ninaopoteza kwenye fuleni yao huwa naahirisha mambo mengine yote...JAMANI MIMI KUFUNGUA ACCOUNT NMB tena itakuwa ndoto isiyotimia..nasikitika tu sikuzote...mfalme wa biashara siku zote ni mteja,,inakuwaje hawa jamaa!!!!!!!!!!!
Nadhani inafika time hata hao staff wanachoka na hiyo misururu na kuona bora wateja waondoke tu ili wao wapumzike. Mimi nashangaa hiyo misururu inatokana na huduma mbovu? staff wachache? au nini?
 
Nadhani inafika time hata hao staff wanachoka na hiyo misururu na kuona bora wateja waondoke tu ili wao wapumzike. Mimi nashangaa hiyo misururu inatokana na huduma mbovu? staff wachache? au nini?


NBC na NMB sio bank za mtu kuhifadhi visenti vyako kabisa, hizo ATM zao tu balaa....
 
Jmani NMB wanalinga kwa kuwa katika wilaya nyingine hakuna bank,kwa mfano wiki iliyopita nilikuwa mkoa mpya wa Katavi wilaya ya Mpanda,kule hakuna bank zaidi ya NMB sasa ukienda ina maana huna namna ya kuishi vizuri mpaka uwe na account ya NMB la sivyo uyembee na cash ya kutosha mpaka siku unaondoka.
Ushauri ni kuwa wafungue matawi mengi na waboreshe huduma zao kwa kupunguza masharti yasiyokuwa na maan
 
Hawa jamaa hawafai kabisa, nilikuwa na account NMB nikaacha kuitumia kwa mwaka mmoja, ukafika wakati lazima niwe naye kwa kuwa kuna transaction ambazo lazima zifanyike nje ya DSM kupitia NMB, Nikaagiza wawe wananiwekea hiyo pesa uko ilivyowekwa wakaambiwa account imefngwa.Kilichofuata? Naambiwa , niende kwenye tawi langu nilikofungua hiyo account. Nilivyoenda uko nilichoambiwa kiliniudhi sana, eti lazima nijaze fomu upya kufungua account!!!! Sasa kulikuwa na faida gani ya kunipeleka kwenye tawi langu? kwa nini nisifungue account katika tawi nililoenda?Inaboa.
 
Back
Top Bottom