Njia hizi za asili zitumiwe na “Nguvu Jamii”kupambana na ufisad ...tafakurii!!!

meddie

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
434
125
Wtz tunatabia yakusahau haraka lkn naamini wote bado tunakumbuka jinsi mwaka juzi tar.24 April 2009 Nd. Reginald Mengi, alivyochukua hatua “ninayoiona ya ujasiri wa pekee” kutaja kwa majina baadhi ya raia na viongozi wa juu nchini kuwa ni ‘mafisadi papa’
Ktk watu hao wakwanza alikuwa Rostam Aziz, mbunge wa Igunga na mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM). Watuhumiwa wengine na wote watz wenye asili ya kieshia ni wafanyabiashara Tanil Somaiya, Yussuf Manji, Jeetu Patel na Subhash Patel.
Mengi alikuwa raia wa pili kujitokeza hadharani na kutuhumu wafanyabiashara na viongozi wa kisiasa kuwa ni “mafisadi.”Wa kwanza akiwa Dk. Willibrod Slaa, aliyekuwa mbunge wa Karatu (CHADEMA), aliyetaja viongozi na wafanyabishara 10 kuwa ndio wala nchi hapo 15 Septemba 2007 kwenye mkutano wa hadhara, uwanja wa Mwembeyanga, Temeke jijini Dar es Salaam.
Nawahesabu watu hawa miongoni mwa watu muhimu nchini waliojitoa kwa ajili ya kupiga vita ufisadi hadharani na wanastahili kupewa pongezi ingawa bado vita inaendelea! Inasikitisha watz tumechelewa sana kujua adhali ya ufisadi katika maisha na uchumi wetu na hivyo kuendelea kuwakumbatia mafisadi na mbaya zaidi kutotoa support ya kutosha kwa watu wanaojitokeza kupinga ufisadi.
Nasema haya wote tukijua mambo yanawayopata hawa mashujaa wetu kwa kujitokeza kwao kupinga ufisadi! Dr. Slaa wote tunajua matusi anayotukanwa na mpaka wanasema hana akili timamu, kesi nk. Ndugu Mengi amefunguliwa kesi na mtuhumiwa wa ufisadi bwana menji.
Mafisadi wamekuwa very strategic ktk kufanya kazi yao na kwa njia hiyo kujificha wasijulikane/wasifatiliwe, mojawapo ya njia hizo ni
· kwa kujua shida za watz za umasikini na uelewa mdogo, wametumia mwanya huo kugombea nafasi za kisiasa ilikuonyesha wanajali lkn kumbe ili kupata mwanya mzuri wa kuwaibia watz
· Wamejua watz wana-mind mambo yasiyo ya msingi na mambo hayo kuwachukulia nafasi kubwa kiulewa na mtazamo; mfano mambo ushabiki wa Simba na Yanga. Hivyo kuchukua cover ktk mambo hayo kwa kufadhili timu!
· Kuweka urafiki wa karibu na viongozi wakuu wa nchi ilikurinda maslahi yao
· N.k
Katika kipindi hiki watati watz tunatakiwa kuilipa dowans pesa ambayo hatujui ni kwa nini tuilipe na tunamlipa nani hasa? Wakati ambapo wazalendo wenzetu wanabuluzwa mahakani kwa kosa la kujitoa kukemea ufisadi! Wakati ambapo watz wenzetu wanapoteza maisha directly na indirectly kwa sababu ya ufisadi! Wakati ambapo raisi, chama tawala na serikali wanaongea/wanamtizamo kama kichwa cha mwenda wazimu kuhusiana na ufisadi! Naona hiki ni kipindi ukomavu wa ufisadi umefika kileleni kabisa!
Swala linalobaki ni nini la kufanya? Je ni kuendelea kumwangalia Rais wetu ambaye anasema hajui/hana undani na masuala ambayo ni pekee tulitegemea awe na undani nayo atupatie effective mwelekeo?
Yapo mengi yakuwaza na kusema kuhusu nini la kufanya…lakini ebu tukumbuke (naamini wengi tunatoka vijijini) twachukua hatua gani inapotokea kuna mtu anahatarisha maisha; mfano kwa ndugu zetu wasukuma wanapogundua mtu mmoja anamaliza watu kwa uchawi! Ndugu zetu wahaya wao uweka chini migomba yote na mibuni shambani! Ama hapa town watu wakigundua kijana fulani ndiye anahatarisha maisha na hata ukampeleka polisi haisaidii wanafanyaje?
Haya ni baadhi ya mambo yanafanyika wakati watu wamekosa msaada wa kisiasa, kipolisi, kisheria na kimahakama na maisha yao kuendelea kuathilika kwa sababu ya bad governace.
Lkn naomab nirudi nyuma kdg na kuulize kwani majumba, magari, mashamba n.k ya hawa mafisadi hayajulikani ilituanze kwa kutumia njia zetu za asili! ....... kwa kuchoma au woga unatusumbua? Wakowapi wakurwa siku hizi jamani?
Naamini ikitokea tokea angalau gari la fisadi likachomwa moto itakuwa message kubwa kwa mafisadi na hawatakuwa tena na ujasili wakutuburuza mahakani!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom