Asprin
JF-Expert Member
- Mar 8, 2008
- 68,012
- 95,352
Hii kwangu ilikaa vibaya. Mwanzoni nilidhani masihara mpaka niliposhuhudia makonde na chupa zikirushwa. Kisa? bar maid.
Ni kwamba kuna ka baameid kamoja ka kimbulu kameleta zahma kwenye bar moja mitaa ya kwetu (lazima nikiri ni kazuri, kwakuwa hata mzee mzima nilikuwa napanga kukasarandia). Njemba moja kumbe ndio inakaweka mjini; imekapangia chumba na inakapa fedha za matumizi. Kumbe swahiba wake njemba ambaye anajua uhusiano ule akawa anakaiba kisirisiri. Siri ikafichuka jana, baada ya mabaameidi wenye wivu kumtonya mwenye mali.
Njemba yenye mali, ikapandisha na kushusha presha. Ikamsubiri swahiba wake anayemwibia. Kama masihara vile, njemba mwizi ilipotinga kaunta na kuagiza ka valeur kake ikashangaa inakwidwa kwa nyuma. Wadau kwakuwa tunaujua uswahiba wao, tukadhani masihara mpaka ulipoibuka mtiti wa kufa mtu.
Kibaya zaidi hizi njemba zote zimeoa, na zinaishi maeneo ya jirani. Nadhani mpaka mida hii, habari zitakuwa zimefika kwa wake zao. (Labda na kwa wife wangu pia, huwezi jua. Nasubiria nipigiwe simu kuulizwa kulikoni kwakuwa njemba zenyewe ni washkaji zangu pia.)
Kutandikana kwa sababu ya penzi la baameidi imenishangaza sana. Na kumgharamia baameidi kiasi kile wakati wale ni watu wa kumegwa na kila mtu atakaye ndilo limenishangaza zaidi. Ni mimi tu nimebakia, ni mimi tu kuwaletea habari.
Wasalaam.
Ni kwamba kuna ka baameid kamoja ka kimbulu kameleta zahma kwenye bar moja mitaa ya kwetu (lazima nikiri ni kazuri, kwakuwa hata mzee mzima nilikuwa napanga kukasarandia). Njemba moja kumbe ndio inakaweka mjini; imekapangia chumba na inakapa fedha za matumizi. Kumbe swahiba wake njemba ambaye anajua uhusiano ule akawa anakaiba kisirisiri. Siri ikafichuka jana, baada ya mabaameidi wenye wivu kumtonya mwenye mali.
Njemba yenye mali, ikapandisha na kushusha presha. Ikamsubiri swahiba wake anayemwibia. Kama masihara vile, njemba mwizi ilipotinga kaunta na kuagiza ka valeur kake ikashangaa inakwidwa kwa nyuma. Wadau kwakuwa tunaujua uswahiba wao, tukadhani masihara mpaka ulipoibuka mtiti wa kufa mtu.
Kibaya zaidi hizi njemba zote zimeoa, na zinaishi maeneo ya jirani. Nadhani mpaka mida hii, habari zitakuwa zimefika kwa wake zao. (Labda na kwa wife wangu pia, huwezi jua. Nasubiria nipigiwe simu kuulizwa kulikoni kwakuwa njemba zenyewe ni washkaji zangu pia.)
Kutandikana kwa sababu ya penzi la baameidi imenishangaza sana. Na kumgharamia baameidi kiasi kile wakati wale ni watu wa kumegwa na kila mtu atakaye ndilo limenishangaza zaidi. Ni mimi tu nimebakia, ni mimi tu kuwaletea habari.
Wasalaam.