Elections 2010 Niwaonavyo wagombea watatu wa urais

Kufikia hatua ya kuteuliwa kugombea uraisi si kipimo cha ubora wa mgombea.Mara nyingi hatua hiyo hufikiwa kutokana na kubebwa na vyama tu, ambavyo navyo si kipimo cha akili za wananchi bali matakwa ya kimfumo unaotawala ulimwengu kwa sasa.
Mbali na kampeni za uchaguzi zinazoelekea ukingoni kutoa mielekeo ya nani anafaa zaidi kukabidhiwa uongozi wa nchi.Ufuatao ni uelewa wangu kuhusiana na wagombea watatu wa nafasi hizo.Hao ni Ibrahim Lipumba,Jakaya Kikwete na Wilbroad Slaa.
Mimi binafsi kwa nafasi hii namuamini zaidi Ibrahim Haruna Lipumba.Namuona ana elimu ya mambo ya kiuchumi ambalo ndilo tatizo sugu la watanzania.Ana uchangamfu wa kiuraisi na huzungumza kwa hekima.Wale wanaompinga si kutokana na kukosa sifa bali sababu nyengine ambazo ikibidi nitazitaja baadae.
Jakaya Mrisho Kikwete ni mkweli katika utekelezaji wa ahadi zake.Hata hivyo amezungukwa na wajanja wengi wa hapa ndani ya nchi na wale wa nje ambao mara nyingi huwa wanaingilia maslahi ya watanzania na hata kumzonga ili asitekeleze baadhi ya ahadi ambazo ziko ndani ya uwezo wake.
Wilbroad Slaa.Nitakayoyasema juu yake hapa, najuwa si pahala muafaka.Lakini ukweli wa moyoni mwangu unanifanya nisiwe na chaguo jengine isipokuwa nimueleze kama nimuonavyo.CHADEMA kwa makusudi au kwa bahati mbaya wametuletea chagua ambalo lisingepaswa kuwa hivyo kwa wakati huu.Hana sifa za kuwa raisi.Fani ya elimu yake hachaguliki kwa kundi kubwa la wapiga kura.Si muadilifu kwa nafsi yake na hawaheshimu watu wanaomzunguka.Ni mpayukaji.
Katika siasa kuna kudanganya huku kwa undani mtu anafanya vyengine kama alivyofanikiwa raisi wa mwanzo wa Tanzania;Julius Nyerere.Hilo ni gumu kufanikiwa kwa dkt Slaa.Zaidi ya ubunge aliokwishakuupata hastahiki kupata cheo cha juu na hata kurudia huo ubunge.
Chaguo linabaki kwa wagombea wawili,yaani Kikwete na Lipumba.Ili kuzuia hatari ya kushinda kwa dkt Slaa ambaye hana elimu wala sifa,nawashauri wapiga kura waangalie nani kati ya hawa wawili anafaa zaidi kupewa kura.

Wewekama rais ukipangiwa mambo ya kufanya na walio nje ya nchi yako, wewe ni *****. ushawishi unaotoa ni pumba tupu, njoo kwa mara nyingine.
 
Wewekama rais ukipangiwa mambo ya kufanya na walio nje ya nchi yako, wewe ni *****. ushawishi unaotoa ni pumba tupu, njoo kwa mara nyingine.
Naona umekuja na hasira za kukurupuka kama za dkt Slaa.
Hueleweki.Hebu fafanua nukta yako.
 
Mimi nadhani Ami anasumbuliwa na udini, Uislam, ushahidi ni hiyo avatar yako. Pia hizo waraka waislam wamekuwa wakitoa nadhani kuna kitu.
Conclusion yangu yangu ni kuwa:
1. Waislamu wako tayari kumpigia kura JK si kwa sababau si mchapa kazi bali tu ni muislam
2. Waislam ni watu hatari sana kwa kudhania kuwa hii nchi ni yao peke yao. Wasisahahu madudu aliyofanya huyo Firauni JK yanawaathiri wao pia. pia wasisahau kuwa mazuri yote yatakayoletwa na Prezida wetu Dr Slaa nao watafaidi pia. Acheni ughaidi!
3. Unafiki, kutoeleza ukweli wa mambo inaonesha mtoa mada hana elimu ya kutosha, nashawishika kudhani kuwa huyu jamaa kasoma madrasat, akajifunza kutumia computer ndo anaanza kuchangia humu. kwa Taarifa yako, Dr Slaa ana Shahada ya UZAMIVU (Philosophia Doctorae au PhD) na kwa elimu yake, wanasiasa wote presha inapanda, presha inashuka.
4. Mwisho, hakikisha 31.10 kura yako unampa DR SLAA.
HATUDANGANYIKI. VOTE FOR DR SLAA
Sisi waislamu si watu wa kuchezewa kabisa katika kila hali.Kuanzia elimu,hekima mpaka kujitoa muhanga ikibidi.Tuna kanuni ya kupima ipi ni shari ndogo kati ya shari nyingi, pale inapokuwa hatuna mbadala kutokana na shari hizo.
Katika uchaguzi huu tumepima mengi.Kikwete katuudhi kwa mengi na ana mapungufu kama walivyo wengi wetu.Hata hivyo mbele ya dkt Slaa yeye ni nafuu.Huenda tukakata kura zetu kwa Lipumba na kumpa yeye Kikwete.
 
Dkt Slaa yuko taaban.Nasikia hajaweza kuyafikia maeneo mengi ya nchi huku siku za kampeni zikiwa zimebaki chache.Helkopta yake imemuangusha.
Kikwete na Lipumba wamekuwa na wakati mzuri hata kurudia baadhi ya maeneo waliyokwisha kuyapitia.
 
sikubaliana kabisa nawewe. Uwezo wa kuongoza si lazima uwe na kiwango cha juu sana kielimu. Kwa ujumla Tanzania inahitaji mabadliko. ni miaka 50 tangu tanzania ijitawale na wote walio ongoza nchi ni wasomi, mpaka sasa tuko wapi? na tuna kila kitu. Mafuta, Gas, Maji, Madini, Ardhi yenye rutuba, Je ninani anafaidika?. Skando kubwa zimeibuliwa na upinzani za ufisadi je ninani anaye faidika? Kikwete ambaye ni msomi unae mpigia debe ana madaraka ya kukemea na kutumia vyombo vya sheria alivyonavyo kuwaadhibu Mafisadi, zaidi tunasikia porojo Ina udhi!!!. Kura yako ni uwamuzi wako kama watanzania tunapenda mabadliko |hatuna haja ya kuogopa upinzani, ndio maana kunasheria ya vyama vingi, kwamba chama kinachoshindwa kutekeleza ahadi zake basi tuchague chama kingine tuone nao watatufikisha wapi katika kipindi cha miaka mitano.
 
sikubaliana kabisa nawewe. Uwezo wa kuongoza si lazima uwe na kiwango cha juu sana kielimu. Kwa ujumla Tanzania inahitaji mabadliko. ni miaka 50 tangu tanzania ijitawale na wote walio ongoza nchi ni wasomi, mpaka sasa tuko wapi? na tuna kila kitu. Mafuta, Gas, Maji, Madini, Ardhi yenye rutuba, Je ninani anafaidika?. Skando kubwa zimeibuliwa na upinzani za ufisadi je ninani anaye faidika? Kikwete ambaye ni msomi unae mpigia debe ana madaraka ya kukemea na kutumia vyombo vya sheria alivyonavyo kuwaadhibu Mafisadi, zaidi tunasikia porojo Ina udhi!!!. Kura yako ni uwamuzi wako kama watanzania tunapenda mabadliko |hatuna haja ya kuogopa upinzani, ndio maana kunasheria ya vyama vingi, kwamba chama kinachoshindwa kutekeleza ahadi zake basi tuchague chama kingine tuone nao watatufikisha wapi katika kipindi cha miaka mitano.
Mimi pia nakubaliana na wewe.Ndio maana hata mimi najiona nina uwezo wa kuongoza.Elilmu yangu ya madrasa inanifanya nifaae sana baadhi ya maeneo ambayo wagombea wengi hawayamudu.
Pamoja na hivyo elimu ya dkt Slaa ni kikwazo katika utumishi wa nafasi ya uraisi.
 
Hakuna hata mmoja anayefaa maana wote ni products za ccm-mafisadi. We are just desparate!
 
Sisi waislamu si watu wa kuchezewa kabisa katika kila hali.Kuanzia elimu,hekima mpaka kujitoa muhanga ikibidi.Tuna kanuni ya kupima ipi ni shari ndogo kati ya shari nyingi, pale inapokuwa hatuna mbadala kutokana na shari hizo.
Katika uchaguzi huu tumepima mengi.Kikwete katuudhi kwa mengi na ana mapungufu kama walivyo wengi wetu.Hata hivyo mbele ya dkt Slaa yeye ni nafuu.Huenda tukakata kura zetu kwa Lipumba na kumpa yeye Kikwete.

Mpeni Lipumba
 
:dance: mkuu post yako inashabihiana na tamko la kikundi cha wafuasi wa dini ya kiislamu waliolitoa hivi karibuni.
nina wasi wasi kama udini utaingia hadi jf hatutafika mbali kwa sababu sisi kama great thinkers tunatakiwa kutoa mfano wa fikra za kimantiki badala ya fikra za sokoni.

haiingi akilini kudai eti dr slaa hana elimu na wakati hiyo phd amepata darasani.
udini ni mbaya sana naulaani hapa jf. period.
 
Ami
Ayo ni mawazo yako na una uhuru nayo.
Ila kwa haraka haraka naona kama vile unasukumwa na udini katika kutoa maamuzi. Ni kigezo gani ulichotumia kuona elimu ya Dr Slaa ina mashaka na haifai kuendesha nchi? Kwa taarifa yako viongozi wengi unaowafahamu wamesoma Seminari za kanisa, na mpaka hivi sasa Seminari ndio zinaongoza kwa ubora wa waalimu, mazingira ya shule,na elimu kwa ujumla.
Achana na mambo ya kufikirika na kuweka udini mbele ni ushauri wa bure tu, Huwezi kuendelea kwa kukaa vibarazani na kunywa kahawa, jioni kupiga majungu na kusubiri misaada.
 
ndugu ami, sitaki kuamini hili lakini nadhani lina ukweli ndani yake, wewe unaongozwa na itikadi ya kidini ingawa hukutaja hapa moja kwa moja. Hivi unadhani elimu ya dr.slaa ni ya upadri peke yake? Je unajua viongozi wote wenye hekima duniani kuanzia karne ya 4 enzi za roman empire walikuwa wanasoma philosophy? Je, unajua watu wanaosoma philosophy tena kwa undani zaidi ni pamoja na mapadri? Je, unajua duniani hakuna chuo cha kusomea uraisi? Iweje useme elimu ya dr.slaa haiendani na cheo anachokitaka?! mi nafikiri elimu yako ndo haiendani na yale unayoyachambua.

fact!!!!!!
 
Ami
Ayo ni mawazo yako na una uhuru nayo.
Ila kwa haraka haraka naona kama vile unasukumwa na udini katika kutoa maamuzi. Ni kigezo gani ulichotumia kuona elimu ya Dr Slaa ina mashaka na haifai kuendesha nchi? Kwa taarifa yako viongozi wengi unaowafahamu wamesoma Seminari za kanisa, na mpaka hivi sasa Seminari ndio zinaongoza kwa ubora wa waalimu, mazingira ya shule,na elimu kwa ujumla.
Achana na mambo ya kufikirika na kuweka udini mbele ni ushauri wa bure tu, Huwezi kuendelea kwa kukaa vibarazani na kunywa kahawa, jioni kupiga majungu na kusubiri misaada.[/QUOTE]


Hatutaki mgombea atakayeendeleza ukiritimba wa kwamba shule za seminari ndizo zinazoongoza.Ubora huo umepatikanaje kwenye seminari hata ukosekane kwenye shule za serikali.Huoni kwamba ni kujipendelea kwa kuweka MOU na kukacha misamaha ya kodi.Tunachotaka ni kwamba huo ubora uhamie serikalini ili na sisi walalahoi tusiotayari kupoteza imani zetu za kidini nasi tufaidike.
Kingine ni kuwa huo ubora ni wa kufikirika tu au ni hewa ukweli ni kuwa wengi wanaomaliza seminari kama dkt Slaa ni vilaza.Angalia kashfa ya misamaha anayoahidi kuitekeleza!.Huo usomi uko wapi?.
Maendeleo gani yamepatikana kwa kuongozwa na nyinyi munaoshinda kwenye mabaa na kunywa vitu haramu.Hata nyakati za kazi za kiofisi za serikali tunawaona sehemu hizo.Ni afadhali sisi tunaokunywa kahawa na kula pilau.
 
post 318, thanks 12 !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Yaani inaonekana we ndo una matatizo. kwani hauungwi mkono na unayosema. inawezekana we ni yule uliye badili jina baada ya kupigwa madongo na vichwa vilivyoko JF
 
post 318, thanks 12 !!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!! Yaani inaonekana we ndo una matatizo. kwani hauungwi mkono na unayosema. inawezekana we ni yule uliye badili jina baada ya kupigwa madongo na vichwa vilivyoko JF
Hapo hujaeleweka.Weka vyema wazo lako tuone iwapo una jipya kuhusiana na dkt Slaa.
 
OH!Another lunatic person!Milembe Hospital is there to help you,do not undermine the capacity of the hospital,you never know!,you might be healed!
 
:whistle: Mweshimiwa, nadhani wewe una ka-upungufu kidogo ka mawazo. Si Slaa asiye kuwa na elimu ya kutosha. Labda wewe ndo std 7 ya 2000. Jitahidi kuendelea kusoma zaidi ili uweze pevuka kimawazo. Huna strong evidence ya kusema hayo kwa kadamnasi hii.... Kawaulize wenzio kijiweni wakupe wasifu wa wote then come again.............:A S 103:
 
Ami
Ayo ni mawazo yako na una uhuru nayo.
Ila kwa haraka haraka naona kama vile unasukumwa na udini katika kutoa maamuzi. Ni kigezo gani ulichotumia kuona elimu ya Dr Slaa ina mashaka na haifai kuendesha nchi? Kwa taarifa yako viongozi wengi unaowafahamu wamesoma Seminari za kanisa, na mpaka hivi sasa Seminari ndio zinaongoza kwa ubora wa waalimu, mazingira ya shule,na elimu kwa ujumla.
Achana na mambo ya kufikirika na kuweka udini mbele ni ushauri wa bure tu, Huwezi kuendelea kwa kukaa vibarazani na kunywa kahawa, jioni kupiga majungu na kusubiri misaada.[/QUOTE]


Hatutaki mgombea atakayeendeleza ukiritimba wa kwamba shule za seminari ndizo zinazoongoza.Ubora huo umepatikanaje kwenye seminari hata ukosekane kwenye shule za serikali.Huoni kwamba ni kujipendelea kwa kuweka MOU na kukacha misamaha ya kodi.Tunachotaka ni kwamba huo ubora uhamie serikalini ili na sisi walalahoi tusiotayari kupoteza imani zetu za kidini nasi tufaidike.
Kingine ni kuwa huo ubora ni wa kufikirika tu au ni hewa ukweli ni kuwa wengi wanaomaliza seminari kama dkt Slaa ni vilaza.Angalia kashfa ya misamaha anayoahidi kuitekeleza!.Huo usomi uko wapi?.
Maendeleo gani yamepatikana kwa kuongozwa na nyinyi munaoshinda kwenye mabaa na kunywa vitu haramu.Hata nyakati za kazi za kiofisi za serikali tunawaona sehemu hizo.Ni afadhali sisi tunaokunywa kahawa na kula pilau.

Mkuu tofauti yetu na wewe ni kubwa sana, huwezi kuiona kwa mtizamo ulionao.
Ukitaka shule za Serikali zilingane na status ya Seminari wambie hao viongozi wako waache ufisadi na wawekeze kwenye elimu ya kweli na sio shule za kata. Sitaki kuongea mengi kwa kuwa unaujua ubovu wa system yenu na nakushangaa unapomshambulia mtu kwa dini yake. Wewe upo uislaam kwa matakwa yako au umejikuta upo huko baada ya kuzaliwa na wazazi waislaamu? Fikiri zaidi ya dini, ni ushauri wa bure tu. Ningependa nikufahamishe zaidi lakini kwa mtizamo wa machapisho yako haupo tayari kujifunza ya wengine, nafikiri sitokujibu tena manake kuendelea kufanya hivyo ni sawa na kupoteza muda wangu.
 
Back
Top Bottom