Rejao
JF-Expert Member
- May 4, 2010
- 9,220
- 4,056
Devi kamwona mwenzie waliesoma nae siku nyingi akiwa amejiinamia kwa masikitiko kwenye baa. Akamsogelea,
Devi: Aise Abuu, habari za siku nyingi?
Abuu: Safi japo si safi sana, nina mawazo sana, maisha yamekuwa magumu sana ndugu yangu.
Devi: Nini tatizo unaonekana uko hovyo sana
Abuu: Niko hovyo ndugu yangu. Unajua Mzee wangu alifariki mwaka jana Januari, akaniachia urithi wa shilingi milioni sita. Miezi mitano baadae, mama akafariki akaniachia nyumba nikauza nikapata milioni 22,
Devi: Duh aise pole sana kupoteza wazazi wote mfululizo lazima ikupe mtu mawazo.
Abuu: Mjomba nae baada ya miezi mitano kafariki akaniachia milioni4
Devi: E bwanaee mbona mikosi? Kila miezi mitano unapoteza mtu?
Abuu: Mikosi kweli sasa imeshapita karibu miezi minane kimya na hela imeshaisha ndugu yangu
Devi: Aise Abuu, habari za siku nyingi?
Abuu: Safi japo si safi sana, nina mawazo sana, maisha yamekuwa magumu sana ndugu yangu.
Devi: Nini tatizo unaonekana uko hovyo sana
Abuu: Niko hovyo ndugu yangu. Unajua Mzee wangu alifariki mwaka jana Januari, akaniachia urithi wa shilingi milioni sita. Miezi mitano baadae, mama akafariki akaniachia nyumba nikauza nikapata milioni 22,
Devi: Duh aise pole sana kupoteza wazazi wote mfululizo lazima ikupe mtu mawazo.
Abuu: Mjomba nae baada ya miezi mitano kafariki akaniachia milioni4
Devi: E bwanaee mbona mikosi? Kila miezi mitano unapoteza mtu?
Abuu: Mikosi kweli sasa imeshapita karibu miezi minane kimya na hela imeshaisha ndugu yangu