Kurzweil
JF-Expert Member
- May 25, 2011
- 6,622
- 8,397
[h=6]Nitaishitaki CCM Mahakamani, Bado najadiliana na wakili wangu kuhusu hilo.
Nia ninayo, Uwezo ninao, na Sababu ninazo.
... Baadhi ya mashitaka yatakayoainishwa ni:
Kupigwa kibao nikiwa mtoto mdogo (1985) na kada wa CCM, pale nilipouliza swali la msingi baada ya kuiona karatasi ya kupigia kura hasa ukizingatia wakati ule hakukuwa na haja ya kujiandikisha kupiga kura, unaenda tu kituoni unachukua karatasi na kuijaza. Msingi wa swali langu ni hoja, nilimuuliza msimamizi wa kituo " hivi hakuna mgombea mwingine hapa ili tumchague?"
Ile karatasi ilikuwa nyembamba na ndefu kidogo, halafu ilikuwa na sehemu mbili za picha, upande wa kulia ilikuwa picha ya baba aliyejaa mashavu, mwenye tabasamu na mvi moja moja kwa mbali,na chini yake kuna alama ya V au ndio. Upande wa kushoto kulikuwa na sehemu ya picha yenye kivuli (giza) na chini yake alama ya X. Hapo ndipo nikauliza swali langu la msingi na kupigwa, sasa basi kwanini nipigwe badala ya kujibiwa na kama ilivyo kawaida kwa watoto kuuliza maswali hata 200 ikibidi.
Pili niliona watoto wakipiga kura kwa maelekezo kwamba"njoo jaza hapa"ulikuwa ni utani wa kweli.
Sababu nyingine ni kubakwa : Uhuru wangu ulibakwa mwaka 1987, pale nilipolazimishwa kuimba nyimbo zenye hamasa ya chama cha mapinduzi bila idhini yangu. Shuleni mimi nilikuwa mtafsiri wa lugha ya kiingereza kwa wenzangu, M/kiti wa kamati ya "maadili lugha " ila kila siku asubuhi niliamriwa kuimbisha wenzangu nyimbo za CCM" Chama chetu cha mapinduzi chajenga nchi", Aaaah TANU na CCM vyajenga nchi, na nyinginezo nyingi, nilipokataa nilipewa adhabu mbaya sana, Kwanza mwalimu mkuu, (Mwl Daudi Minja soma hii)aliniingiza ofisini kwake, akanichapa viboko ambavyo havina idadi....
Kulazimishwa kutoa Sh 5, kama mchango wa mafuta ya mwenge hata kama hakukuwa na mwenge, mwalimu wa uhamasishaji alikuwa kada wa CCM (Bibiana Tarimo)..jamani wote hawa wapo tena bado ni waalimu na wanaendelea kufundisha (Naomba nisizitaje shule wanazofundisha,na waliopandishwa vyeo kuwa waratibu wa elimu hadi nitakapo wasiliana na mwanasheria wangu).
Jina langu kupewa mtu mwingine na akasoma kwa jina langu katika shule moja kule Arusha huku mimi nikisoma shule ya bei mbaya kwa kujishughulisha na kuombaomba mitaani hadi kufikia hatua ya kusaidiwa na kanisa (Naomba nisiitaje kwa sasa kutokana na taratibu za kesi kutokamilika) kwa kutumia majina yangu matatu..huyu niliwahi kutana naye nikamuuliza na kumdadisi akanieleza ukweli wote...huyu ni key person kwani atakuwa mmoja kati ya mashahidi. Baba yake ni kada wa CCM, hivyo naamini atatupa ushirikiano wa kutosha. Yote haya yalifanyika kwa kauli mbiu ya kuwaandaa vijana wa kakamavu wa CCM....tupewa mifano mingi ya jinsi Lord Powel, mwanzilishi wa Scout huko Uingereza!
Hayo ni baadhi ya yale yatakayoainishwa na kujumuishwa katika hati ya mashitaka.
Naomba mwongozo!!![/h]
Nia ninayo, Uwezo ninao, na Sababu ninazo.
... Baadhi ya mashitaka yatakayoainishwa ni:
Kupigwa kibao nikiwa mtoto mdogo (1985) na kada wa CCM, pale nilipouliza swali la msingi baada ya kuiona karatasi ya kupigia kura hasa ukizingatia wakati ule hakukuwa na haja ya kujiandikisha kupiga kura, unaenda tu kituoni unachukua karatasi na kuijaza. Msingi wa swali langu ni hoja, nilimuuliza msimamizi wa kituo " hivi hakuna mgombea mwingine hapa ili tumchague?"
Ile karatasi ilikuwa nyembamba na ndefu kidogo, halafu ilikuwa na sehemu mbili za picha, upande wa kulia ilikuwa picha ya baba aliyejaa mashavu, mwenye tabasamu na mvi moja moja kwa mbali,na chini yake kuna alama ya V au ndio. Upande wa kushoto kulikuwa na sehemu ya picha yenye kivuli (giza) na chini yake alama ya X. Hapo ndipo nikauliza swali langu la msingi na kupigwa, sasa basi kwanini nipigwe badala ya kujibiwa na kama ilivyo kawaida kwa watoto kuuliza maswali hata 200 ikibidi.
Pili niliona watoto wakipiga kura kwa maelekezo kwamba"njoo jaza hapa"ulikuwa ni utani wa kweli.
Sababu nyingine ni kubakwa : Uhuru wangu ulibakwa mwaka 1987, pale nilipolazimishwa kuimba nyimbo zenye hamasa ya chama cha mapinduzi bila idhini yangu. Shuleni mimi nilikuwa mtafsiri wa lugha ya kiingereza kwa wenzangu, M/kiti wa kamati ya "maadili lugha " ila kila siku asubuhi niliamriwa kuimbisha wenzangu nyimbo za CCM" Chama chetu cha mapinduzi chajenga nchi", Aaaah TANU na CCM vyajenga nchi, na nyinginezo nyingi, nilipokataa nilipewa adhabu mbaya sana, Kwanza mwalimu mkuu, (Mwl Daudi Minja soma hii)aliniingiza ofisini kwake, akanichapa viboko ambavyo havina idadi....
Kulazimishwa kutoa Sh 5, kama mchango wa mafuta ya mwenge hata kama hakukuwa na mwenge, mwalimu wa uhamasishaji alikuwa kada wa CCM (Bibiana Tarimo)..jamani wote hawa wapo tena bado ni waalimu na wanaendelea kufundisha (Naomba nisizitaje shule wanazofundisha,na waliopandishwa vyeo kuwa waratibu wa elimu hadi nitakapo wasiliana na mwanasheria wangu).
Jina langu kupewa mtu mwingine na akasoma kwa jina langu katika shule moja kule Arusha huku mimi nikisoma shule ya bei mbaya kwa kujishughulisha na kuombaomba mitaani hadi kufikia hatua ya kusaidiwa na kanisa (Naomba nisiitaje kwa sasa kutokana na taratibu za kesi kutokamilika) kwa kutumia majina yangu matatu..huyu niliwahi kutana naye nikamuuliza na kumdadisi akanieleza ukweli wote...huyu ni key person kwani atakuwa mmoja kati ya mashahidi. Baba yake ni kada wa CCM, hivyo naamini atatupa ushirikiano wa kutosha. Yote haya yalifanyika kwa kauli mbiu ya kuwaandaa vijana wa kakamavu wa CCM....tupewa mifano mingi ya jinsi Lord Powel, mwanzilishi wa Scout huko Uingereza!
Hayo ni baadhi ya yale yatakayoainishwa na kujumuishwa katika hati ya mashitaka.
Naomba mwongozo!!![/h]