Nishati na Madini wanarejea Bungeni Jumamosi hii: Tutegemee muujiza Gani?

GHOST RYDER

JF-Expert Member
Jun 10, 2011
1,025
475

Nishati na Madini siku 21 zimekwisha

Huku Jairo akisukumiwa Tuhuma nyingine jana kama njia na kamtego hivi kupoteza lengo na kuwasahaulisha Watanzania uozo katika Bajeti ya Awali ya Wizara hiyo iliyogonga mwamba mwezi uliopita, siku zao 21 zimekwisha na Jumamosi wanarejea tena Bungeni kuwasilisha Bajeti yao itakayosomwa kwa siku moja na kisha kuputishwa ama kutopitishwa.

My Take:
  • Unafiki wa wabunge na makundi utaona yanavyofanya kazi Jumamosi.
  • Sina shaka semina zimeshapigwa vya kutosha kama ilivyookolewa Bajeti ya Wizara ya Uchukuzi
  • Mie binafsi sitegemei muujiza wowote kesho wala jipya zaidi ya Bajeti kupita katikati ya Giza
  • Ahadi zitajaa zenye ladha saafi kama asali na wingi wa hoja za kinafiki kama mkia wa kondoo
Yetu macho na masikio, sijui mnalitazamaje hili hapo Jumamosi

ADIOS
 
Generator zinadaiwa kuwa zinaweza kusababisha ongezeko la Hewa ya Ukaa kutokana na kuwashwa kwa Wingi bila mpangilio, Thanks to maamuzi mazito ya Serikali kuwabana wamiliki wa mabohari ya Mafuta baada ya shinikizo zito la CDM
 
Naona katika hii bajeti haitakua na jipya zaidi zaidi hongo ndo itatumika zaidi ili ipite kwa upigajikura wao wakiwenda wazimu wa ndio au hapana makinda hakukosea kulifananisha bunge na kariakoo
 
Itakuwa muujiza kama watakuja na muujiza lakini knowing them business as usual will prevail
 
Mie naungana na Mwanakijiji kutoa rai kuwa bila ya Wizara ya Nishati kutenga pesa za Stieglers gorge project hiyo bajeti isipitishwe!!!!! Tumechoka na umeme wa hadithi za megawati hatutaki tunataka a fixed solution na wapunguze matumizi ya serikali kulipia mradi huo.
 
Bunge tangu lini likafanya kazi Jumamosi? Mbona kama vile inataka kupitishwa kwa nguvu hii bajeti? Maana hakutakuwa na muda wa kutosha kuijadili. Na pia, siku hiyo kuna mechi ya Simba na Yanga na Ligi Kuu ya England inaanza...Si unawajua Watanzania ilivyo rahisi ku-divert attention yao?

Tusubiri tuone! Ila hakutakuwa na jipya. Zitapigwa blah blah kisha wabunge wa magamba watagonga meza na bajeti itapita!
 
Bunge tangu lini likafanya kazi Jumamosi? Mbona kama vile inataka kupitishwa kwa nguvu hii bajeti? Maana hakutakuwa na muda wa kutosha kuijadili. Na pia, siku hiyo kuna mechi ya Simba na Yanga na Ligi Kuu ya England inaanza...Si unawajua Watanzania ilivyo rahisi ku-divert attention yao?

Tusubiri tuone! Ila hakutakuwa na jipya. Zitapigwa blah blah kisha wabunge wa magamba watagonga meza na bajeti itapita!

Ligi Kuu ya England ndo chambo hapo, Simba na Yanga wanakipiga Jumatano ijayo Tarehe 17 August 2011.

Kiukweli Jumamosi ni siku ambayo wabunge wengi huipenda kwenda Mnadani kula nyama na mvinyo, bila shaka hapa ni game la kuwafanya wajadili kwa kukosa umakini wakiwazia weekend, ila kama nilivyotahadharisha hapo juu tutayaona na kuyasikia mengi hapo kesho
 
Mie naungana na Mwanakijiji kutoa rai kuwa bila ya Wizara ya Nishati kutenga pesa za Stieglers gorge project hiyo bajeti isipitishwe!!!!! Tumechoka na umeme wa hadithi za megawati hatutaki tunataka a fixed solution na wapunguze matumizi ya serikali kulipia mradi huo.

Tatizo Mwanakijiji washamwona kama Adui hata awashauri jema lipi ni kama hawaoni licha ya Mdau huyu mwenye ufahamu mkubwa kuchukua muda mwingi kuchambua vitu vizito vyenye masilahi ya Umma.
 
Mh. William Lukuvi katoa ufafanuzi tayari kanuni ya 28 kifungu kidogo cha 25 kwa kuwa Bunge haliwezi kukutana siku za Jumamosi Jumapili na siku za Sikukuu, kaomba Bunge kutengua Kanuni hiyo ili kuruhusu Hoja hiyo kujadiliwa siku ya Jumamosi kwa kuwaruhusu Wizara ya Nishati na Madini kuweza kutoa marekebisho yao katika kipengele cha MATUMIZI YA WIZARA na ni KIPENGELE cha UMEME tu.

Mnyika anaomba muongozo kuhusu kutengua kanuni muda kuongezwa na kutoa nafasi ya kujadiliwa vema kwa Hoja hiyo ambayo inadaiwa kuwa haitarejewa Hotuba yote ila kipengele nilichokitaja hapo juu na hapatakuwa na maswali.

Spika anasema muda utatosha kwa kuwa hatasoma tena Hotuba yote kama hofu ya Mnyika ilivyojitokeza
 
Generator zinadaiwa kuwa zinaweza kusababisha ongezeko la Hewa ya Ukaa kutokana na kuwashwa kwa Wingi bila mpangilio, Thanks to maamuzi mazito ya Serikali kuwabana wamiliki wa mabohari ya Mafuta baada ya shinikizo zito la CDM

Sio hewa chafu peke yake pia ni "NOISE POLLUTION"
 
Bunge tangu lini likafanya kazi Jumamosi? Mbona kama vile inataka kupitishwa kwa nguvu hii bajeti? Maana hakutakuwa na muda wa kutosha kuijadili. Na pia, siku hiyo kuna mechi ya Simba na Yanga na Ligi Kuu ya England inaanza...Si unawajua Watanzania ilivyo rahisi ku-divert attention yao?

Tusubiri tuone! Ila hakutakuwa na jipya. Zitapigwa blah blah kisha wabunge wa magamba watagonga meza na bajeti itapita!

Masaki umeongea Point kamanda wangu.................. That's TZ
 
Ligi Kuu ya England ndo chambo hapo, Simba na Yanga wanakipiga Jumatano ijayo Tarehe 17 August 2011.

Kiukweli Jumamosi ni siku ambayo wabunge wengi huipenda kwenda Mnadani kula nyama na mvinyo, bila shaka hapa ni game la kuwafanya wajadili kwa kukosa umakini wakiwazia weekend, ila kama nilivyotahadharisha hapo juu tutayaona na kuyasikia mengi hapo kesho

Wangetaka ipite kiurahisi wangepanga tarehe ya jana Majembe ya CHADEMA yakiwa Arusha
 
Bajeti imepita, na marekebisho yanatia matumaini. Mlikuwa wapi sasa kuja na mikakati kama Hii

Hongera Wizara na Wataalam mliofanya marekebisho haya
 
Back
Top Bottom