GHOST RYDER
JF-Expert Member
- Jun 10, 2011
- 1,025
- 475
Taarifa zisizo rasmi kutoka chanzo chetu cha Uhakika mjini Dodoma zinatuaarifu ya kuwa mjadala wa kuinusuru Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini bado wajumbe wanakinzana kwa lipi hasa liwe azimio la jumla.
Kundi moja linaafiki kufumba macho kupitisha Bajeti hiyo kwa mabadilishano na Nafasi ya Ngeleja, Yaani Ondoka tupitishe Bajeti yako. Walau ukijiuzuru tutapoza hasira za watanzania.
Upande mwingine haukubaliani na Njia hii Mbadala ukiendelea kushikilia msimamo wa kutounga mkono Bajeti hiyo. Hatari ya kutopita kwa Bajeti ni kuvunjwa kwa Kikao cha Bunge linaloendelea kwa Mujibu wa Kanuni na kuandaliwa Bajeti mpya. Jambo ambalo kundi la awali linalitazama kama litakuwa matumizi mabaya ya fedha katika kipindi hiki ambacho Uchumi wa Taifa unazidi kudorora.
Yote haya yanaendelea huku shauku kubwa ya watanzania ni kuona nishati ya Umeme wa Uhakika unapatikana.
Tunapanga silaha zote mapema kufuatilia Mjadala LIVE kutoka Mjengoni.
Stay Online
ADIOS
Kundi moja linaafiki kufumba macho kupitisha Bajeti hiyo kwa mabadilishano na Nafasi ya Ngeleja, Yaani Ondoka tupitishe Bajeti yako. Walau ukijiuzuru tutapoza hasira za watanzania.
Upande mwingine haukubaliani na Njia hii Mbadala ukiendelea kushikilia msimamo wa kutounga mkono Bajeti hiyo. Hatari ya kutopita kwa Bajeti ni kuvunjwa kwa Kikao cha Bunge linaloendelea kwa Mujibu wa Kanuni na kuandaliwa Bajeti mpya. Jambo ambalo kundi la awali linalitazama kama litakuwa matumizi mabaya ya fedha katika kipindi hiki ambacho Uchumi wa Taifa unazidi kudorora.
Yote haya yanaendelea huku shauku kubwa ya watanzania ni kuona nishati ya Umeme wa Uhakika unapatikana.
Tunapanga silaha zote mapema kufuatilia Mjadala LIVE kutoka Mjengoni.
Stay Online
ADIOS