Nisaidieni

mmmh changa la macho hilo mpenz, tena wanaume wanaofatilia huwa ni nomaaa, anakupumbaza akili yako ili ujue anakupenda kumbe looo! mmh (Moyo wa mtu kichaka) sepa zake mdada asikupotezee muda huyo. tena unaweza achana nae mungu akakufungulia mlango ukampata mwenye malengo sawa na ww! believe that my dia GOD IS ABLE.
 
Let him go..
Coz atakutumia sana then will dump U.. Take care
 
Dada, unataka akwambieje?
kesha kuchenjia huyo na hataki kukuoa,
kama anakupenda angekuoa tu na mama yake angemuweka sawa lakini kilichobaki kwake hapo ni tamaa tu.
mchenjie uone reaction yake, angalia ustaarabu wako before its too late
kwa kawaida watuwengi (i call them weak) wakikaa na mchumba muda mrefu inakuwa ngumu kumuacha
 
Duuh wanawake...kila siku nikisoma story kama hizi huwa zinanipa hasira. Ushajua kama hana mapenzi ya kweli na wewe, halafu kinachokuweka ni nini. Baba, mama, shangazi hawaweki ndoa kama anakupenda atafanya juu chini awe nawe. Huyo in simple terms ni time waster na kama unataka usubiri mama abadilishe mawazo, haya subiri mpaka yesu atakaporudi.
 
pia inawezekana wala jamaa hajaongea na mama yake, hapo anataka kukuziba mdomo ili aendelee kufaidi tunda kwako...dada, hapa utapata ushauri wa aina mbalimbali lakini mwisho wa siku mwenye maamuzi ya mwisho ni wewe mwenyewe...fuata moyo wako ila ukae ukijua kuwa jamaa hana mpango na wewe na huenda ana mtu mwingine aliyepo katika plans zake za maisha...chezea play boy!!! KIMBIA ACHANA NA HUYO ANAKUPOTEZEA MUDA NA KUKULETEA KAUZIBE!!!pole sana!
 
hakupendi hata kidogo mwache kabla haujaingia kwenye ndoa ya majuto na masikitiko,kama angekuwa anakupenda asingekuwa anakaa kimya mda mrefu mpaka atake vitu ndio akupigia!halafu mama yake hajamwambia. amekudanganya,
 
binti huyo kijana ulizaliwa nae? au mlikutana wote mna meno 32?

hebu mwache hakupendi anakutumia.....
 
Dadangu chapa lapa huyo jamaa wala hana mpango nawe kabisa.
 
Na-declare interest............ Nilishaishi kanda ya ziwa, hivyo nawafahamu kidogo.

Ushauri wangu dada, kwa kuwa amekuwa mkweli sikiliza moyo wako kwa makini sana. Kiwango chake cha msimamo kikoje? Je, unashawishika kwamba ataweza kubadili fikra za mama yake?

Kusema kweli, kama huyo mama amekulia na kuishi huko huko ukuryani, (kwamba hana exposure) binafsi, sidhani kama kijana wake/your boy ataweza kumbadili!

Vile vile, kuna uwezekano mkubwa hataki kukupoteza, labda unamridhisha sana kimapenzi, unam-care vyakutosha Etc. Hivyo kinachomfanya abaki kwenye dilema ni wivu/watakachofaidi wengine.

Ushauri; Anza taratiiiiiiiiiiiibu kuruhusu hewa safi iingie ndani ya moyo wako. Epuka kutumiwa, anza kujiheshimu......... Inawezekana yupo ambaye hatawekewa vigezo vya kabila na mama yake!
 
mimi ni msichana nina 26
years, nina boyfriend wangu tumeanzana tokea chuo lakini huwa haonekani
kunijali ananitafuta akiwa na shida zake za............, nilimsemaga
akajirekebisha kidogo, badae tukawa tunaongelea mipango ya ndoa na
akasema ataenda kuongea kwao, alirudi ananiambia kwamba mama yake
anataka mtu wa kabila lake (mkurya) lakini anasema yeye ananipenda
nisihofu nisubirie labda mama yake atabadilika. Msimamo wake kutwa ni
visingizio mama anaumwa, sijui kazi anatoka usiku, simu yenyewe napigiwa
jumamosi akiwa na shida hata sielewi na ananigagania eti nisimwache na
hataki hata niwe na mtu ananifatilia kweli. Naombeni ushauri je huyu mtu
ananipenda hajui kuonyesha mapenzi au ananipotezea mda, na suala la
mama kweli anaweza kubadilika au changa la macho?

"dada angu mwanaume anaekupenda kwa dhati na mwenye maandalizi mema km mke haiwezi pita cku hajakujulia hali,leave him alone"
 
Back
Top Bottom