Double K
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 907
- 340
Mimi ni msichana nina 26 years, nina boyfriend wangu tumeanzana tokea chuo lakini huwa haonekani kunijali ananitafuta akiwa na shida zake za............, nilimsemaga akajirekebisha kidogo, badae tukawa tunaongelea mipango ya ndoa na akasema ataenda kuongea kwao, alirudi ananiambia kwamba mama yake anataka mtu wa kabila lake (mkurya) lakini anasema yeye ananipenda nisihofu nisubirie labda mama yake atabadilika. msimamo wake kutwa ni visingizio mama anaumwa, sijui kazi anatoka usiku, simu yenyewe napigiwa jumamosi akiwa na shida hata sielewi na ananigagania eti nisimwache na hataki hata niwe na mtu ananifatilia kweli. naombeni ushauri je huyu mtu ananipenda hajui kuonyesha mapenzi au ananipotezea mda, na suala la mama kweli anaweza kubadilika au changa la macho?