Nisaidieni wapendwa

Brainiac

Senior Member
Jan 1, 2012
165
13
Shikamoo wakubwa, wenzangu na mm habari za saa hz bila kusahau wadogo hamjambo...mimi ni msichana ninae fanya kazi katika kampuni moja hv nina shida na natumai mtanisaidia ninaomba mniambie ni biashara gani ninaweza fanya kwa kutumia msingi mdogo?
 
salama dada! weka wazi msingi wako ni shilingi ngapi, upo wapi n.k. manake hata million 100 yaweza kuwa ndogo na pia laki 1 yaweza kuwa kubwa, ni kutegemea mazingira. hivyo ni vema ukaweka wazi mazingira as much as possible,
 
Msingi mdogo ni bei gani??
maana kwa miji kama dar es salaam hata million mia ni msingi mdogo........funguka zaidi tukupe mawazo....
 
mi msingi wangu ni sh. laki 3 na nusu je inawezekana?

Fungua banda la video kama unakaa uswazi litakulipa uoneshe movies zilizotafsiriwa kiswahili ili badae ufungue library ya kukodisha CDs. Kwa mabanda mengine yanayofanya biashara kama yako.
 
Fungua banda la video kama unakaa uswazi litakulipa uoneshe movies zilizotafsiriwa kiswahili ili badae ufungue library ya kukodisha CDs. Kwa mabanda mengine yanayofanya biashara kama yako.

inalipa sana?
 
Nashindwa nikusaidiaje maana hujajieleza vizuri na unaonekana hujiamini. yaani una wasiwasi sana. Biashara inataka ujiamini dada na uwe tayari kula hasara. Wazo langu kwako ni kwamba jaribu kufanya utafiti wa kina ili ujue huko unakoishi ni huduma gani watu wanaihitaji zaidi lakini inakosekana? Ukipata jibu angalia uwezekano wa kuanza kuitoa hiyo huduma ktk mazingira hayo.
 
Hivi ile thread iliyukuwa na heading Mtaji Milioni 10 modes waliipeleka wapi? kwanini hawakuifanya sticky? It was one of the best threads for business ideas?
 
Back
Top Bottom