Nisaidieni kumpata huyu mchumba

habari zenu wana jf natumaini wengi wenu hamjambo . jamani kuna msichana tuko naye course moja nampenda sana nataka awe mchumba wangu, leo tukiwa darasani niliamua kukaa naye karibu alivyoniona akatabasamu huku akiniangalia machoni hapo ndipo moyo wangu ulinasa kama sumako nikahisi kuchanganyikiwa sijamtokea nipeni njia za kumpata

Kumpata msichana umpendaye inahitaji mbinu zako za kiume. Mtu hakufundishi namna ya kumpata msichana.
 
Namba ya watu niliowatabasamia. . .
Wakati mwingine hua mtu anatabasamu kwa aibu baada ya kugundua mtu anamkodolea macho au just to be nice. Ngoja ukute mupenzi yupo humo humo darasani. .

Maisha ni shule dearest, ndo atakuwa amejifunza namna ya kutongoza kwa siri....hata hiyo kutabasamiana inaweza mleteaa kesi...!
 
step ya kwanza mwambie mambo..
step ya pili mwambie nimefurahi kukusalimia..
step ya tatu mwambie akupe jina la FB au ID ya JF ili muwezekusocialize...
step ya nne utaongea nae kwenye inbox au PM kwa kuwa wewe ni domo zege

kila la kheli mtongozaji..

We balaa kaka....nimeipenda ila mbavu sinaaa!
Ume mpatia mpaka basi....
 
Jenga naye urafiki, kama mna Group Discussions tafuta namna ya kujiunga katika GD lake, jitahidi kumfahamu lkabla ya kumweleza hisia zako au kumwingiza ndani ya hisia zako may be she isn't available halafu umeshajiwekea matumaini unaweza unakutana na kibuti cha ugoko!!!..
 
Jenga naye urafiki, kama mna Group Discussions tafuta namna ya kujiunga katika GD lake, jitahidi kumfahamu lkabla ya kumweleza hisia zako au kumwingiza ndani ya hisia zako may be she isn't available halafu umeshajiwekea matumaini unaweza unakutana na kibuti cha ugoko!!!..

Asante
 
We hua unafuata watu wakiwa na pesa?

Mie nimempata aliweza kujieleza mpaka nikashawishika na tungo zake za kiume,huyu hawezi kuongea asubiri wasichana wanaoshobokea pesa atawapata bila kutongoza!mwanamke km mm anakua tayari anajua kuitafuta hela na kuizoea,so hababaiki na wenye pesa.
 
dogo zingatia elimu kwanza
ukishaanza mapenzi ukiwa chuo tena na mate wa darasa moja jihesabu kupata gpa ya 2.1
ni hatari sana tena sana omba Mungu lecturer nae asimtongoze utajuta kuwa chuo
elimu muhimu kwanza mapenzi baadae,ukimaliza utawakuta wamejaa tele
siku ukimwona akiongea na mtu mwingine darasani hutaelewa kituenzi zetu tukiwa chuo tungekuwa na mawazo kama yako tusingefika tulipo
kwa ushauri zingatia masomo achana na mapenzi chuoni.
 
Mimi naweza kukushauri kama unataka awe msebule wako, hiyo ya mchumba siwezi. Sijui upo rede.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom