nisaidieni jinsi ya kumshauri:

Mrs Patrick

Member
Feb 2, 2012
13
0
nina rafiki yangu amekuja kuomba ushauri: ana mpenzi wake wana uhusiano wa mwaka mmoja. wanaishi mbalimbali, na tangu waanze uhusiano wameonana mara mbili tu ambayo ni mwezi wa kumi mwaka jana na mwezi wa kwanza mwaka huu.ila mwanzoni mwa uhusiano wao mkaka alikuwa anampigia simu sana, walikuwa wanachat pia. ila tatizo linakuja ni kwamba saiv yule mkaka kabadilika. mara ya mwisho wameonana ni january, na mpaka sasa hawajaonana. na hata walivyoonana alikuta message za wasichana wengine, ila huyo mkaka akasema hao wadada ndo wanamtaka.sasa rafiki yangu akimwambia waonane, mkaka anasema yupo busy na shule. saiv shule kamaliza lakini anatoa visingizio kibao. na pia mara nyingi hapatikani kwenye simu anasema sehemu aliyopo kuna shida ya umeme. sasa anashindwa kumuelewa mpenzi wake huyo, nimshauri vipi jamani.
 
Urafiki wa mwaka mmoja tena wa kuona mara mbili tu nao unahitaji ushauri? Ndoa za miaka 20 zinavunjika bila ushauri itakuwa urafiki? Kwangu mimi naona sio dhambi huu urafiki ukivunjika for good!! Aanze upya tu lakini awe makini asijekurupuka akakanyaga ****
 
hivi watu mbona bado wana ng'ang'ania mapenzi ya long distance wakati inaonekana kabisa kuwa haya dumu?
 
ukiona manyoya ujue imeliwa...kwa nini kujiumiza moyi kwa mtu ambaye sio baba, kaka wala ndugu...piga chini endelea na maisha mengine...wanawake bhana wanaume wengine huwa wanaamini mwanamke ukiona visa vinaanza kama hivyo utakuwa ushapata mustakabali wa nini kinaendelea lakini wadada huwa mnakuwa wagumu kuelewa
 
ushauri wa nini wakati lipo wazi, me najua kama unampenda mtu kila unapopumzika lazima umuwaze na lazima umpigie kila siku, ukishindwa kabisa haziwezi kupita siku mbili...othrwz no love...akate kona
 
Huyo alikuwa anataka kipapaa tu, keshapata anaendelea kutegua mitego mingine. Muambie aamini mtima wake. Hana hata majirani wa majirani zake jamani?
 
Ukiona manyoya ujue ......................? nafikiri kwa hapo utajaza mwenyewe, mwambie rafikiyo akimbie kungali mapema
 
Urafiki wa mwaka mmoja tena wa kuona mara mbili tu nao unahitaji ushauri? Ndoa za miaka 20 zinavunjika bila ushauri itakuwa urafiki? Kwangu mimi naona sio dhambi huu urafiki ukivunjika for good!! Aanze upya tu lakini awe makini asijekurupuka akakanyaga ****

Mwambie akae humu.
 
ushauri wa kufuatwa ni huu wa mkuu Gerrard tu!
Urafiki wa mwaka mmoja tena wa kuona mara mbili tu nao unahitaji ushauri? Ndoa za miaka 20 zinavunjika bila ushauri itakuwa urafiki? Kwangu mimi naona sio dhambi huu urafiki ukivunjika for good!! Aanze upya tu lakini awe makini asijekurupuka akakanyaga ****
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom