Wapendwa wana JF naombeni msaada wenu katika hili;
Mimi nipo kwenye ndoa ni mwaka mmoja sasa lakini matatizo ndani ya hii ndoa hayaishi.Mimi na mme wangu wote tunafanya kazi ila kuna mambo nashindwa kuyaelewa na ninabaki njia panda!
Mwezi uliopita nilikwenda likizo nyumbani cha ajabu wakati najiandaa kuondoka asubuhi mme wangu akaninyang'anya card yangu ya benki eti akifikiria nitakwenda kuwapa pesa nyumbani kwetu!
Kwa kweli tulibishana sana hadi nikafanikiwa kuondoka na card yangu ila alikasirika sana hadi akasema nikirudi nije na wazazi wangu eti hanitaki tena!
Nimeenda likizo nimerudi yakawa yameisha cha ajabu tukawa tumetoka out na waliokuwa washenga wetu wa harusi acha aanze kusimulia yaliyotokea!
Mimi ninaamini katika kusamehe na kusahau lakini mwenzangu ukifanya kosa anakumbushia na makosa yaliyopita nashindwa kuelewa ni kwa nini?
Kwa kweli mimi inaniuma sana na kuna kipindi najiuliza hivi kweli huyu mme wangu ananipenda kweli?
Naombeni mnisaidie katika hili kutokana na hizi tabia za mme wangu mimi nifanye nini?
Amelie!
Mimi nipo kwenye ndoa ni mwaka mmoja sasa lakini matatizo ndani ya hii ndoa hayaishi.Mimi na mme wangu wote tunafanya kazi ila kuna mambo nashindwa kuyaelewa na ninabaki njia panda!
Mwezi uliopita nilikwenda likizo nyumbani cha ajabu wakati najiandaa kuondoka asubuhi mme wangu akaninyang'anya card yangu ya benki eti akifikiria nitakwenda kuwapa pesa nyumbani kwetu!
Kwa kweli tulibishana sana hadi nikafanikiwa kuondoka na card yangu ila alikasirika sana hadi akasema nikirudi nije na wazazi wangu eti hanitaki tena!
Nimeenda likizo nimerudi yakawa yameisha cha ajabu tukawa tumetoka out na waliokuwa washenga wetu wa harusi acha aanze kusimulia yaliyotokea!
Mimi ninaamini katika kusamehe na kusahau lakini mwenzangu ukifanya kosa anakumbushia na makosa yaliyopita nashindwa kuelewa ni kwa nini?
Kwa kweli mimi inaniuma sana na kuna kipindi najiuliza hivi kweli huyu mme wangu ananipenda kweli?
Naombeni mnisaidie katika hili kutokana na hizi tabia za mme wangu mimi nifanye nini?
Amelie!