Nimewahi kuwa na mpenzii ambaye nilimkuta akiwa bado kigoli katka mahusiano yetu niligundua alikuwa mwongo sana na kila kitu yeye ni mbishi sana ukimkataza kitu atakubali kuacha ila siku hiyo hiyo unamkuta anfanya hilo hilo ulilokataa. nilikuwa nikimkataza kuhusu kutumia line ya tigo coz mimi nilikuwa natumia voda atakubali ila ndani ya dkk tu tayari tigo iko hewani tena iko busy ukimuuliza anabisha basi ikabidi niangalie ustaarabu wangu Mungu jaalia nikapata binti mwenye sifa zoote za kuwa mke wangu tukapendana sana na nikamweleza kila kitu kuhusu x g.f wangu akanielewa. Baada ya kama miezi miwili x.g.f akanieleza kuwa ana miezi miwili hajaenda siku zake alivyoenda kupima kweli akaonekana ana mimba ya miezi na kliniki kaandika jina langu kama Baba jukumu la mtoto nikaona ni langu nikakubali coz kwa mahesabu yangu niliona uwezekano ni mkubwa ila ikabidi nimweke wazi siwezi kumwoa yeye kutokana na tabia zake hasa ya uongo ila mtoto nitamlea mimii tatizo linakuja namna ya kumweleza mke wangu mtarajiwa kuhusu hili coz naona kama mwanzo wa kumpoteza,,,,,,,,, msaada wa mawazo jamani