Nionavyo maana ya shirika na ndege ya taifa..

broken ages

JF-Expert Member
Mar 23, 2012
235
84
Shirika la ndege la taifa pamoja na ndege inayobeba nembo ama bendera ya taifa ni namna mojawapo bora sana ya kutangaza taifa nje ya nchi,kwani ndege inaposafiri kwenda nje wenyeji na wasafiri wanaosafiri kupitia sehemu ilikofikia ndege wanaona alama ama nembo ya nchi husika kwa maana wanaiona ndege, ofisi za ndege airlines offices mara Nyingi kama siyo kwa ujumla hufunguliwa sehemu za kitovu cha miji(city central)hivyo wengi waonaopita sehemu hizi wanapoona majina ya hizo offices ndipo huzitambua ama kujikumbusha nchi husika,mashirika ya ndege huweka vipeperushi vya matangazo ya makampuni yao sehemu za faragha sana zikionekana maelezo yake nchi imetangaazwa tayari hili litasaidia sana hata sekta kama utalii na taifa kwa ujumla kujulikana inanisikitisha mtalii anayekuja Tanzania kwamba safari yake itamlazimu kupitia Nairobi kufanya connection ambayo itamchukua kama siyo siku kadhaa basi ni masaa kadhaa kunakosababishwa na taifa kukosa usafiri wa moja kwa moja kutoka huko atokako.kama serikali imeshindwa kuliendesha shirika ibinafsishe lakini ktk kusaini miktaba izingatie pamoja na mambo mengine ni nembo gani inastahili kutumika ktk hili.hapa hatutalalamika tena Kenya wanatuzidi kuutangaza utalii ikiwepo na mlima Kilimanjaro pamoja na serengeti
 
Back
Top Bottom