Mlimazunzu
JF-Expert Member
- Dec 14, 2010
- 415
- 52
Ndugu zangu naombeni msaada kwenye kisa hiki cha kweli . nina mke tuliyefunga ndoa yapata miaka 11 iliyopita, mke wangu tulikutana kazini kwenye kiwanda cha kutengeneza biscuits ambapo yeye alikuwa teller mimi ni mwendesha mashine.
Baada ya kuoana nilimwendeleza kimasomo kwakuwa yeye alikuwa wa form IV nami ni darasa la saba, kwakuwa alifanya vizuri katika kozi zake alifanikiwa kupata kazi kwenye shirika moja la kimataifa kama administrative secretary.
Sisi huku kiwanda kilifungwa kutokana na biscuits kukosa masoko kutokana na ushindani uliopo hivyo
nikalazimika kukaa nyumbani huku nikijitahidi kutafuta vibarua vya hapa na pale.
Issue ni kwamba mke wangu sasa amekuwa mbogo hataki kusaidia kitu chochote hapa nyumbani na ikitokea akatoa hela basi masimango yanatisha, tutaitwa majina ya kila aina mara poyoyo, mara Mario nk.
Wakati tunaoana kila mmoja alikuwa na mtoto na wote tulikuwa tunawalea kwa mapenzi bila ubaguzi, cha kushangaza yeye mtoto wake kampeleka international school wa kwangu amemwacha aendelee na hizi za kayumba!
Kinachonipa taabu sana ni kurudi usiku wa manane wakati mwingine akiwa amelewa nikimuuliza anasema walikuwa na kazi nyingi na mikutano inayoambatana na vinywaji, pia ana safari nyingi za kikazi na akifika huko huwa hataki nimpigie simu eti namsumbua!
Sasa je huyu bado anastahili kuwa mke wangu? Si kawa wa mataifa sasa niachane naye nikaoe mwingine?
Vikao vya wazee vimeshindwa kutoa ufumbuzi wanamuogopa au sijui ni kwamba anawakatia mkwanja mrefu?!
Nawasilisha
Hiyo red acha kuwa tegemezi hataki kusaidia maana yake nini??
Hiyo blue wewe huna msimamo wakati anampeleka wakwake international kulikuwa hakuna makubaliano? Mawasiliano kati yako na yeye ni ziro
Hiyo zambarau mikutano gani hiyo inayoambatana na vinywaji sijawahi sikia (wewe ni mlalamishi sana)
Ki ukweli ni hoja nzito mkuu, lakini imekuwa bahati kuwa umekwisha ijibu kwamba
nimekwishaanza maandalizi ya QT, na ninachokazania ni lugha hiyo ambayo wameniambia kuwa it is a ladder to all higher learnings. Pia kutokana na michango yenu ilinihamasisha nikajitutumua kukaweka kakizungu kadogo ako nionekane nami nimo kwenye social class ya wasomi. Au nimekosea jamani?!
Acha uongo juzi QT mara ushajua lugha ngumu hivyo?
Nashukuru sana kwa michango yenu, imekuwa ya manufaa sana kwangu.
Nimeamua kusubiri sitakurupuka kuoa tena nitajitahidi kutafuta kazi japokuwa si kazi rahisi kupata kazi, kuhusu yeye nadhani aendelee na maisha yake nami niwe peke yangu na mwnangu, pengine itanisaidia kupunguza mawazo yanayosababishwa na kumuona akiwa katika hali ya kunikataa na masimango pia.
Ahsanteni sana na Mungu awabariki awazidishie hekima, akili, maharifa na busara ili muweze kuwasaidia na wengine, tuzingatie kuwa haya ni matatizo ya kijamii katika ulimwengu wa sasa tunaouishi, hivyo ni vyema tukapeana ushauri, mwongozo na maelekezi bora ya kuyatatua.
Na kwa kufanya hivi tutapunguza uwezekano wa e.t.c, yaani end of thinking capacity ambayo upelekea mtu kuamua kujinyonga!
Lugha gongana hapa
Ni kweli usemayo lakini jamani hivi kweli mimi sina haki ya kuliwazwa katika magumu haya?!,
mwenzangu ana ponda life yaani kanisahau kabisa, pia kuna suala la kimwili ambalo sijalisema hapa namimi ni mtu mzima niliyekamilika sana kijinsia navumilia kutopata haki hii kwa muda mrefu wakati nahisi mwenzangu anapata ndio maana hana tena shida na mimi.
Nakula kwa kufanya vibarua vya kazi ndogo ndogo si kama mimi na mtoto tunamtegemea yeye keshatubwaga kabisa! hasa ukizingatia kuwa wa kwake yuko boarding.
Pia tusisahau kuwa ajira zenyewe ni taabu siku hizi hata kwa wasomi wenye shahada zao kwangu nikisubiri kujijenga si nitazeeka manake inabidi nirudi shule ili nipate kazi.
uamuzi wa kutafuta mwingine nimeufanya kwa mpangilio kwa mfano nilipojiunga na jf ilikuwa njia mojawapo ya kutafuta faraja kwa kubadilishana mawazo kama hivi, ndio maana utaona sikulisema hili mwanzo mpaka nilipoelewa utaratibu wa mada zinavyowasilishwa.
kwa hiyo nitakayempata atajua nimekosa nini huko kwa awari na tutazungumzia uwezekano wa mapenzi ya dhati kabla ya kupiga hatua zaidi.
Malalamiko again and again
Ahsante sana kwa mchango wako na ushauri wako mzuri,
lakini suala la kukimbilia uhusiano mwingine huoni kama ni muhimu kwa kipindi hiki kwakuwa niko desperate na wakati huo yeye ana good time, think of mimi ndio nafanya kila kitu nyumbani (house boy) yeye anarudi muda anaotaka. Kwa sasa mtotot wake yuko boarding mimi wa kwangu yupo tunaishi naye nisipohangaika hali ni kweli niendelee kuvumilia? ya chumbani naogopa kusema nisijemvunjia heshima hapa mbele za watu.
Umeshatoa uamuzi na inaonyesha tayari una mahusiano mengine
Ahasanteni sana kwa michango yenu mizuri, pia na wale ambao hawakunielewa nawashukuru sana kwakuwa nao wamewakilisha mawazo yao vizuri tu. Hakika nimeona umuhimu wa kujiunga na jf, naomba nitoea ufafanuzi wa ujumla kama ifuatavyo;
Wakati namsomesha ilikuwa ni kwa makubaliano kama mke na mume na kama ujuavyo maagizo yanasema mnakuwa mwili mmoja, hivyo sikuona taabu kwa yeye ambaye amenizidi
darasa kidogo japokuwa division ilikuwa ni IV ya point 28 niliona badala ya mimi kwenda qt bora nimjengee uwezo yeye kwani ni kitu kimoja.
Sina pesa kwa sasa kwakuwa wakati nafanya kazi nilikuwa nawekeza kwenye masomo yake, nimekwishamshauri anipe mtaji wa biashara lakini ananiambia mimi sikusoma hesabu za kibiashara nitazijuaje!
Ubaguzi kwa mtoto wangu unakuwa dhairi sasa kiasi kwamba mtoto ameanza kuuliza kama huyu ni mamake mzazi au kuna mwingine ( mamake alishafariki) hii inanipa shida kwakuwa muda wote sikuzaa naye kwa kile alichokuwa anadai mimba hazishiki, japokuwa hivi karibuni katoa mimba akidai yuko busy hawezi kupata muda wa kulea mtoto kwa sasa!
Ninaposema nafikiria kuoa manake ni kuachana kabisa na huyu na kuanza upya, kama nimempa elimu anayoringia na kuninyanyasa nayo kwa sasa, kwani mimi siwezi kupata mwanamke mwenye upendo wa kweli nami akaniinua kimaisha au ni dhambi mwanamke kumuinua mwanaume?
Kiukweli ni visa vingi naweza kujaza kitabu
Upewe mtaji wa biashara na mwanamke?? Na unalalamika hadharani aibu gani hii.
Wewe umeshaamua kuoa ndo maana unataafuta attention hapa jamvini
BTW: Uamuzi ni wako.
Kwa ushauri wangu ni kwamba stand as a man na acha kucomplain kama mtoto mdogo eti mwanamke anakunyanyasa mara anakunyima mtaji mara anasomesha wakwake international mara anarudi usiku yaani yote haya naona ni malalamiko matupu na wewe unaonyesha dhahiri ni MARIOO acha hiyo tabia kuwa mwanaume mtimilifu unalalamika kutotunzwa na mwanamke nimeshangaa sana. Im sory to say that.
Good day my brother