kwa kweli sioni tabu sana kama kikwete atamteua lowasa. Ingawa lowasa amamekutwa na kashfa hizo ukichunguza kwa makini utagundua kuwa ni mtu anayeipenda sana nchi yake, ni jassiri na anachapa kazi. Kwa lowasa naona ni kitu. Pia naye ameshajifunza kutokana na upepo wa mabadiliko. Tuache kuhukumu kwanza maana nasi tutahukumiwa
Bora Lowassa Mwizi mchapakazi kuliko mtoto wa mkulima mr Pinda muadilifu lakini muoga si jasiri.Fisadi mchapakazi ni bora kuliko muadilifu mzembe.
Wana JF na watu wote wenye mapenzi mema na Tanzania, naomba mnijulishe ni nini tunaweza kufanya kama week ijayo Rais akimteua mshikaji wake E Lowasa kuwa Waziri Mkuu. Au je katiba ya nchi hairuhusu Waziri Mkuu aliyejiuzuru kwa manufaa ya umma kurudi tena kuwa waziri mkuu?
Kama katiba inaruhusu sitashangaa kusikia jina la Lowasa au Rostam linatoka kama waziri mkuu au Waziri katika wizara ya fedha. CCM hawana haibu............
Jamani kwani katiba ya nchi inamzuia Lowasa kuwa waziri mkuu?. Kujiuzulu nafasi hiyo kipindi cha nyuma bado si kigezo cha yeye kutochukua tena nafasi hiyo. Mbona Mwinyi alijiuzulu uwaziri wa mambo ya ndani tokana na kashfa lakini baadaye akaja kuwa raisi wa Tanzania?.
Na kwa kifupi Lowasa kama Lowasa hakuwa na kosa katika sakata la Richmond, kujiuzulu kwake ni kwa ajili ya kuwajibika kwa maana kwamba waliokuwa chini yake hakutenda kilichopaswa kutendwa kwa wakati ule.
Kwa mtazamo wangu mimi Lowasa ni kiongozi mzuri sana. Anafuatilia maagizo aliyotoa, anawapelekesha mawaziri walio chini yake kufanya kazi na wala si kuleta longolongo. Lowasa haoni haya kumfukuza mtu mzembe kazi hadharani. Mawaziri na watendaji wavivu serikalini hawampendi Lowasa kwa sababu ni kiboko yao. Na ndiyo hao wavivu wameweza kumpikia majungu kwa lengo la kumwangusha ili kuendeleza uzembe na longolongo serikalini.
Jakaya tafadhali nakuomba mrudishe Lowasa katika nafasi ya uwaziri mkuu na Pinda mpe wizara nyingine.
hahahhahahhahahha kazikwelikweli!!:bowl::bowl::bowl:nitaacha kazi serikalini nikalime bangi Tarime!
:thinkingDDuuuuuu???? itawashangaza wengi wasio mjua wahite hair, ila nawaambieni wana JF wenzangu, Lowassa ni shoka la chuma cha pua kwa maana ya utendaji kazi na kuleta maendeleo halisi yenye tija. Ni bhati mbaya tu alikuwa mbuzi wa kafara wakati ule ila JK akimrudisha tutajionea maendeleo ya ajabu na hata hao mafisadi pia watamkoma. wanaomfahamu watakuwa wamenielewa hapa
Wana JF na watu wote wenye mapenzi mema na Tanzania, naomba mnijulishe ni nini tunaweza kufanya kama week ijayo Rais akimteua mshikaji wake E Lowasa kuwa Waziri Mkuu. Au je katiba ya nchi hairuhusu Waziri Mkuu aliyejiuzuru kwa manufaa ya umma kurudi tena kuwa waziri mkuu?
Kama katiba inaruhusu sitashangaa kusikia jina la Lowasa au Rostam linatoka kama waziri mkuu au Waziri katika wizara ya fedha. CCM hawana haibu............
Wana JF na watu wote wenye mapenzi mema na Tanzania, naomba mnijulishe ni nini tunaweza kufanya kama week ijayo Rais akimteua mshikaji wake E Lowasa kuwa Waziri Mkuu. Au je katiba ya nchi hairuhusu Waziri Mkuu aliyejiuzuru kwa manufaa ya umma kurudi tena kuwa waziri mkuu?
Kama katiba inaruhusu sitashangaa kusikia jina la Lowasa au Rostam linatoka kama waziri mkuu au Waziri katika wizara ya fedha. CCM hawana haibu............
- Wakuu ninaomba kuuliza kama Mh. Lowassa leo akiamua amechoshwa na CCM na akaitosa in the public kwamba ni chama ambacho hakifai na kwamba sasa anahamia Chadema, maana ni chama kinachofaaa zaidi, je Chadema watamkataa?
William.