Nzowa Godat
JF-Expert Member
- Jun 15, 2011
- 2,783
- 819
Hivi ni kwa nini siku hizi watu wengi hasa vijana wa kike na kiume wamekuwa na mazoea ya kuishi kama mke na mume ilhali hawajaoana? Mara nyingi kisingizio ni 'mpenzi' wangu. Utasikia kijana anajitapa, huyu ni mpenzi wangu nimezaa naye watoto wawili. Ninachofamu mimi wanaozaa watoto ni wanandoa baada ya kufanya tendo la ndoa. Zamani tendo la ngono lilikuwa linapatikana kwa shida sana baada ya kusaga kiatu sana ndio maana watu walikuwa wanaona ni heri aoe mke lakini siku hizi ni bwerere hata vijana hawaoni haja ya kuoa oh! samahani! siku hizi ni kuoana gender balance.
Hivi taratibu za kidini hasa taratibu za kilokole zinakubaliana na wapenzi wa namna hii?
Nawasilisha.
Hivi taratibu za kidini hasa taratibu za kilokole zinakubaliana na wapenzi wa namna hii?
Nawasilisha.