Kwame Nkrumah
JF-Expert Member
- Dec 2, 2008
- 886
- 376
Mara nyingi sana tunasikia viongozi wetu wakiwa wanazungumza na Watanzania nje ya nchi, Botswana, Afrika Kusini, Canada, UK na kwingineko wanashauri sana vijana warudi nyumbani kusaidia juhudi za kujenga Taifa.
Lakini mimi binafsi nimesikia tofauti kidogo kutoka kwa ndugu na jamaa waliofuata ushauri huu. Kwamba fursa hiyo ya kujenga taifa baada ya kurudi hawaipati !!!! Ndugu mmoja alisoma mambo ya computer nje na kufanya kazi hiyo kwa miaka 7 nje. [ ni mtaalamu wa kutisha wa IT } Akaamua kurudi nyumbani kusukuma gurudumu la maendeleo kama wakubwa walivyosihi, lakini baada ya muda alirudi tena na kusema ameshindwa kufanya kazi nyumbani na kwamba atarudi baada ya kustaafu !!
Mwingine alisoma mambo ya masoko, akapata kazi shirika la umma, lakini bosi wake alimnyanyapaa sana. Jamaa akitoa mawazo mapya bosi anasema anataka kumnyang'anya kazi au anafanya kazi kwa sifa. Sasa yeye hana uwezo wa kurudi nje alikokuwa. Inabidi awe hapohapo huku manung'uniko hayaishi. Na kutusihi sisi " jamani msirudi".
Jamaa mwingine akaniambia kama siku hizi nina lafudhi ya Ki-Kenya basi nirudi nyumbani !!!Maana hao ndio wana kazi zote nzuri.
Tupatie experience yako baada ya kurudi.
Lakini mimi binafsi nimesikia tofauti kidogo kutoka kwa ndugu na jamaa waliofuata ushauri huu. Kwamba fursa hiyo ya kujenga taifa baada ya kurudi hawaipati !!!! Ndugu mmoja alisoma mambo ya computer nje na kufanya kazi hiyo kwa miaka 7 nje. [ ni mtaalamu wa kutisha wa IT } Akaamua kurudi nyumbani kusukuma gurudumu la maendeleo kama wakubwa walivyosihi, lakini baada ya muda alirudi tena na kusema ameshindwa kufanya kazi nyumbani na kwamba atarudi baada ya kustaafu !!
Mwingine alisoma mambo ya masoko, akapata kazi shirika la umma, lakini bosi wake alimnyanyapaa sana. Jamaa akitoa mawazo mapya bosi anasema anataka kumnyang'anya kazi au anafanya kazi kwa sifa. Sasa yeye hana uwezo wa kurudi nje alikokuwa. Inabidi awe hapohapo huku manung'uniko hayaishi. Na kutusihi sisi " jamani msirudi".
Jamaa mwingine akaniambia kama siku hizi nina lafudhi ya Ki-Kenya basi nirudi nyumbani !!!Maana hao ndio wana kazi zote nzuri.
Tupatie experience yako baada ya kurudi.