Mkulima wa Kuku
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 1,270
- 533
Tangu aingie madarakani moja ya malalamiko makubwa ya wananchi kwa JK ni woga wa kuchukua maamuzi magumu dhidi ya viongozi anaowateua yeye. Mifano ni mingi: Chenge-mpaka madhara yalipojitokeza ndipo mwenyewe akaamua: Dr. Mwinyi, Mwamunyange kwenye mabomu ya Mbagala na G/mboto -mpaka leo tumepoteza watu wengi lakini wanadunda tu: Jairo, Malima, Ngeleja na rushwa za wazi kwa wabunge -hawa usiseme, mpaka leo maazimio ya bunge hayafanyiwi kazi: Richmond na Dowans saga: Meremeta saga; Dr. Mponda na Dr. Nkya pamoja na madaktari: na mengine mengi. Nini faida na hasara za kushindwa kwake kuchukua maamuzi magumu kichama, kiserikali, kijamii, kirafiki? Je, anawatendea haki watanzania kwa kushindwa kwake kufanya hivyo? Wananchi tunaweza kuchukua hatua gani kumwonyesha kuwa haturidhiki na mambo yake? Nawasilisha