Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Nimekuwa najiuliza nini maana ya kuitwa au kuwa Baba
Je, ni kuzaa mtoto au watoto na kuingia mitini na kumuacha Mama akitaabika?
Je, ni kuzaa mtoto au watoto na kuwalea kwa pamoja na Mama (Mke)?
Je, ni kuzaa uko mtaani kwa wanawake tofauti na kujitangaza kidume kwa kuwa umeweza kuzaa na wanawake tofauti?
Nimeweka hii mada hapa kwani nina mshikaji wangu ambaye Baba yake baada ya kuzaa na Mama yake walitengana na mshikaji kukulia kwa ndugu wa Mama na Mungu saidia amesoma mpaka chuo. Sasa ndugu wa Baba wanaanza kumfuata na kumwambia mjali Baba yako, maisha yake sio mazuri kwa sasa vinginevyo utapata laana kutoka kwa Baba yako. Halafu kumbuka mshikaji toka chekechea hadi anamaliza chuo mwaka jana hajawahi kukutana na Baba yake. Ila msimamo wa mshikaji yeye ni kuwa kwa mateso aliyopata kwa kuishi kwa ndugu mara uku mara kule halafu uishi kwa uhuru kama nyumbani vile kumemfanya amchukie Baba yake na anasema kamwe hamfikirii hata kidogo kwenye maisha yake. Ameamua ni yeye na Mama yake na ndugu za Mama yake Kwani ndio wanajua uchungu na mateso ya kumlelea mpaka hapa alipo leo.
Ndugu yangu sipo;kabla sijachangia mada hii naomba msaada yafuatayo:
nini chanzo cha kutengana na kutelekezwa kati ya wazazi wake?
Kibinadamu hali hiyo inaumiza moyo. Lakini hata hivyo ukweli unabaki palepale: kwamba mwingine kutotimiza wajibu kwako hakukuondolei wewe jukumu la kutimiza wajibu wako kwake. Baba alikuwa na wajibu wa kumtunza, lakini hakufanya hivyo. Akatunza wengine. Leo hii mtoto (kijana) amekuwa mtu mzima ana wajibu wa kumtunza (au kumsaidia) baba yake. Anapaswa kutimiza wajibu huo. Hawezi kusema kwa kuwa baba hakumtunza naye hatamsaidia. Ni makosa! Kwani wajibu wake kwa baba si malipo kwa mema alivyomfanyia. Ni wajibu wa kiutu na kimaadili. Tena kijana akifanya hivo atapata baraka tele kutoka kwa Mungu, na pia litakuwa somo chanya kwa wazazi wengine wanaotelekeza watoto waoNilishawahi kuongea na mshikaji sababu ya mafarakano ya familia yao akasema nachofahamu yeye ni kuwa baada ya kuzaliwa yeye dingi yake aliamua kuoa mwanamke kwa sababu ambazo hata kwa mujibu wa ndygu zake wengine zilisababishwa na huyo dingi kuamia DSM na kumpata mwanamama mwingine ndio akatoa go ahead kwa mama wa mshikaji. Kinachomuuma mshikaji ni kuwa hiyo familia nyingine aliyokwenda kuilelea baba yake ilikula raha sana watoto wakasoma raha mustarehe yeye akitupwatupwa huku na kule pasipo msaada mahususi