Kwanza unatakiwa ujue maana halisi ya mahusiano.kila mtu anaweza akawa na maana yake, lakin maana yangu fupi inasema; mahusiano ni ukaribu kati ya mtu,kikundi au nchi moja na nyingine ambao una lengo la kutimiza jambo fulani. Jambo hilo linaweza likawa la kibiashara, kisiasa, kimapenzi au jambo lolote lilokusudiwa kufanywa baina ya watu hao. Katika mapenzi mahusiano ni stage miongoni mwa stage ili kuyafikia mapenzi. Sasa tukija kwenye mada yako, mtu anapokwambia unatumia nguvu katika mahusiano, ana maana unalazimisha kuwa karibu naye! Na kama mtu hataki kuwa karibu nawe mana yake hana haja nawe. Nawasilisha
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.