Crucifix
JF-Expert Member
- Feb 20, 2011
- 1,651
- 588
Watu waishio kwa chini ya dola 1 kwa siku ndio husemekana maskini sana. Hii nimeisikia tangu dola 1 ikiwa sawa na shilingi 800. Leo hii dola 1 ni sawa na sh 1600, je kuishi chini ya dola 1 bado ni kipimo cha umaskini uliokithiri? Au pengine kama watanzania tunapaswa kuja na kigezo kingine ili tunapopambana na umaskini tuweze kujipima kwa kipimo chetu wenyewe.