Kakende
JF-Expert Member
- Aug 18, 2012
- 2,741
- 1,231
Katika hali isiyo ya kawaida mchambuzi mashuhuri wa siasa bwana RENATUS MKINGA amekuja kwenye kipindi cha marumbano ya hoja kinachoendeshwa na kituo cha TV cha ITV akiwa amevalia nguo ya CCM. Kitendo cha kuvaa nguo hiyo wakati yeye anafahamu kwa undani madhambi yaliyotendwa na chama hicho kama alivyokuwa akiainisha kipindi cha nyuma kimeniogopesha mimi binafsi. Moja kati ya dhambi kubwa ni kuunga mkono jambo fulani wakati ukijua kuwa ni jambo la hatari.
Eti anasema chama pekee kinachounga mkono muungano ni CCM wakati kwa sasa Wazanzibari wanataka kujitenga wakiwa chini ya utawala wa CCM tangu muungano. Mkinga anafikiri kuunga mkono muungano ni maneno tu, kwanini CCM hawajatatua kero za muungano wakati wao muda wote ndiyo watawala, na wana uwezo wa kufanya hivyo?.
Mkinga ambaye jamii masikini ilimuheshimu sasa anaanza kupotea, kitendo cha kuvaa nguo ya CCM ni dalili za kufa kiakiri. Shujaa ufa akisema ukweli, mkinga umeanza kupotea na ndiyo maana mwendesha mada bwana DEOGRATIUS RWEYUNGA alikuponda hapohapo kuwa jadili maswala ya kauli ya nyerere kuhusu muungano na siyo jezi ya CCM
Eti anasema chama pekee kinachounga mkono muungano ni CCM wakati kwa sasa Wazanzibari wanataka kujitenga wakiwa chini ya utawala wa CCM tangu muungano. Mkinga anafikiri kuunga mkono muungano ni maneno tu, kwanini CCM hawajatatua kero za muungano wakati wao muda wote ndiyo watawala, na wana uwezo wa kufanya hivyo?.
Mkinga ambaye jamii masikini ilimuheshimu sasa anaanza kupotea, kitendo cha kuvaa nguo ya CCM ni dalili za kufa kiakiri. Shujaa ufa akisema ukweli, mkinga umeanza kupotea na ndiyo maana mwendesha mada bwana DEOGRATIUS RWEYUNGA alikuponda hapohapo kuwa jadili maswala ya kauli ya nyerere kuhusu muungano na siyo jezi ya CCM