Nini kimempata Nassari?

Amavubi

JF-Expert Member
Dec 9, 2010
30,140
13,215
Joshua Nasari hayupo bungeni leo kuapishwa....

Hapana mkuu, ataapishwa kesho kutwa.

Kulikuwa na kutoelewana baina ya viongozi wa Chadema waliopo hapa Dodoma na Uongozi wa bunge. Chadema waliomba wabunge Hao waapishwe kesho, lakini kanuni zinasema wabunge wapya wataapishwa siku ya kikao cha kwanza na shughuli hiyo itakuwa ya kwanza. Lakini katibu wa bunge hakuwaeleza hivyo Chadema na ndio maana hata matangazo yaliyotolewa awali yalionyesha kuwa hawataapishwa Leo. Lakini kikao Kilipoanza asubuhi ikaonekana kwenye order paper kuwa uapishwaji unapaswa kuwepo. Lakini Chadema na bunge wameelewana na sasa Nassari na mwenzake wataapishwa Alhamis. Kesho Nassari atafanyiwa orientation.

Msafara wake, ukiongozwa na Mbowe na magari zaidi ya kumi ndio umeingia Dodoma kwa mbwembwe kama nusu saa iliyopita
 
Spika hana sababu ya kutokuwepo kwa wabunge hao wawili lakini ametoa mwongozo kwamba kamati ya uongozi itapanga tarehe nyingine ya kuwaapisha
 
Kuna wabunge wangapi leo wa cdm au wote wapo kwenye msiba wa kanumba?
 
amecite bonge la precedent, nahisi itatungiwa kanuni.........liwaahidi wapiga kura wake kwamba vumbi litaanza kutimka leo...au ndio anamsaidia Halima Mdee kumtoa Lulu???
 
Sio lzm aapishwe siku hyo hyo,hana misifa's camp,nassari yupo juu sana ajalewa sifa kua mb kwani ana uhakika ameshinda kihalali ndio maana hana wasiwasi hata sipika akisema sio mb atashinda tena.
 
Kuna wabunge wangapi leo wa cdm au wote wapo kwenye msiba wa kanumba?
Serikali yote ipo Leaders Club wanamzika kanumba!!

Rais
Waziri mkuu
Makamu rais
Waziri wa habari na michezo
waziri wa akina mama na watoto
waziri wa afya
mwanasheria mkuu wa serikali
Makamu wa Spika - ndugai


Sasa hapo unataka nini tena kujua serikali hii ni hovyohovyo!!
 
Wabunge wa chama cha demokrasia hawajakuwepo bungeni kwa kuapishwa kikao cha mwanzo.sababu hatujui.je taarifa ya kuapishwa kwao haikuwafikia au la?
Mwenye neno kuhusu kutoapiapishwa kwao aseme.
 
Mbunge mteule wa arumeru mashariki Joshua Nassary na mbunge mwingine wa viti maalum wote wa chadema hawakuwepo bungeni hivi punde kuapishwa!Spika wa bunge mama Anna makinda amesema hali hiyo sio ya kawaida kwa kuwa inajulikana kuwa ratiba ya kwanza ya leo kama ilivyopangwa na kamati ya uongozi wa bunge ni kuwaapisha wabunge wapya!Spika amesema ratiba za bunge zitaendelea kama zilivyopangwa kwa kuwa hana taarifa zozote za udhuru kutoka kwa wateule hao.Kamati ya uongozi wa bunge itakaa tena kupanga ratiba nyingine ya kuapisha wabunge hao.

My take:I didn't like it.
 
Back
Top Bottom