Taifa_Kwanza
JF-Expert Member
- Sep 3, 2010
- 443
- 86
Mimi ni mzaliwa wa Mwanza, kutokana na mgawanyiko wa Majimbo ya uchaguzi, naweza kusema nimezaliwa katika Jimbo la Ilemela.
Wakati wa Kampeni za Uchaguzi habari nyingi kutoka Mwanza zilikuwa juu ya Jimbo la Nyamagana, sikusikia sana juu ya Ilemela, siku chache kabla ya uchaguzi nilipata bahati ya kukutana na rafiki yangu ambaye yeye anaishi Mwanza, tukazungumzia juu ya mchakato wa kampeni na matarajio ya matokeo.
Akaniambia Wenje anafanya kampeni nzuri, atatoa ushindani mzuri kwa Masha, lakini nilipomuuliza juu ya Ilemela, alisema Mbunge wa Kule ni Dialo, akadai Ilemela kumesinzia sana, bado hawajaamuka kabisa, nikamuuliza kwani Chadema hawajasimamisha Mgombea, akasema kuna mtu kamuambia kwamba wamesimamisha Mgombea lakini yeye hamjui hata kwa jina.
Hata mimi nilitegemea hilo, sababu hata nilipojaribu kupigapiga simu kwa ndugu jamaa na marafiki, sikuona mabadiliko yakitokea ILEMELA.
Hiyo ni TISA, Kumi ni kwamba Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ulikimbia Mwanza Kufanya utafiki wa maendeleo ya Kampeni, katika taarifa yao wakadai Dialo anamsaliti Masha Mwanza,sikumbuki kama walisema anafanya usaliti namna gani, pia hawakusema kama kumbe na Dialo kansa ya kushindwa ilikuwa ikimtafuna taratibu, Habari kuhusu Ilemela hazikusisikika kabisa.
Kauli ya kunistua niliipata siku moja kutoka kwa mama yangu mzazi, Kada wa CCM wa kuchanjiwa, Usiku wa jumamosi nilimpigia kumjulia hali, mwisho wa Maongezi nikamuuliza uchaguzi vipi, Akaniambia kesho Ilemela tutapaza sauti, nikamuuliza mtapaza vipi? akasema kura ni siri ya mtu, lakini kwa vile wewe ni Mtoto wangu nitakuambia, Kesho naipigia Kura VEMA.
Kilichobadilisha msimamo wa Mama yangu ni nini?
Hasa Kilichotokea Ilemela ni kitu gani jamani?
Wakati wa Kampeni za Uchaguzi habari nyingi kutoka Mwanza zilikuwa juu ya Jimbo la Nyamagana, sikusikia sana juu ya Ilemela, siku chache kabla ya uchaguzi nilipata bahati ya kukutana na rafiki yangu ambaye yeye anaishi Mwanza, tukazungumzia juu ya mchakato wa kampeni na matarajio ya matokeo.
Akaniambia Wenje anafanya kampeni nzuri, atatoa ushindani mzuri kwa Masha, lakini nilipomuuliza juu ya Ilemela, alisema Mbunge wa Kule ni Dialo, akadai Ilemela kumesinzia sana, bado hawajaamuka kabisa, nikamuuliza kwani Chadema hawajasimamisha Mgombea, akasema kuna mtu kamuambia kwamba wamesimamisha Mgombea lakini yeye hamjui hata kwa jina.
Hata mimi nilitegemea hilo, sababu hata nilipojaribu kupigapiga simu kwa ndugu jamaa na marafiki, sikuona mabadiliko yakitokea ILEMELA.
Hiyo ni TISA, Kumi ni kwamba Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi ulikimbia Mwanza Kufanya utafiki wa maendeleo ya Kampeni, katika taarifa yao wakadai Dialo anamsaliti Masha Mwanza,sikumbuki kama walisema anafanya usaliti namna gani, pia hawakusema kama kumbe na Dialo kansa ya kushindwa ilikuwa ikimtafuna taratibu, Habari kuhusu Ilemela hazikusisikika kabisa.
Kauli ya kunistua niliipata siku moja kutoka kwa mama yangu mzazi, Kada wa CCM wa kuchanjiwa, Usiku wa jumamosi nilimpigia kumjulia hali, mwisho wa Maongezi nikamuuliza uchaguzi vipi, Akaniambia kesho Ilemela tutapaza sauti, nikamuuliza mtapaza vipi? akasema kura ni siri ya mtu, lakini kwa vile wewe ni Mtoto wangu nitakuambia, Kesho naipigia Kura VEMA.
Kilichobadilisha msimamo wa Mama yangu ni nini?
Hasa Kilichotokea Ilemela ni kitu gani jamani?