Nimekupata mkuu...hata mimi nlivyoisoma hiyo article niliona haipo balanced....lakini nimeiweka ili tu watu watoe changamoto zao...kama kuna source nyengine watu waiweke....kilichonivutia kuhusu hiyo article ni mpangilio wake pamoja na Historia ya watekaji...nlikuwa sijui kuwa watekaji wote walikuwa na uhusiano wa kifamilia
Nini hujaelewa?Wenge tupu
Ingawa Waziri wa Mawasiliano na Uchukuzi wa Tanzania, John Malecela, aliwaambia waandishi wa habari mjini Nairobi kuwa watekaji hao walitaka kujiuzulu kwa Mwalimu Julius Nyerere, aliporudi Dar es Salaam alisema watekaji hao hawakutoa madai yoyote. Akiwa kama kiongozi wa kushughulikia utekaji nyara huo, Waziri Malecela alitoa taarifa hizo hizo kwa Rais Nyerere;
........Baadaye ilikuja kujulikana kuwa majina ya watekaji wale ni Musa Memba (25), Mohamed Ali Abdallah (26) na ndugu yake Abdallah Ali Abdallah (22), Mohamed Tahir Ahmed (21) na Yassin Memba (21). Kiongozi wao alikuwa Musa Memba............
Haya majina haya, mmmmmh ila coz ilikuwa serikali ya jembe basi waliipata fresh
Nini hujaelewa?
Linatajwa kuwa moja ya majaribio yenye kustua vyombo vya dola vya nchi hii,
Japokuwa hadithi hubadilika badilika kila mtu akikusimulia, lakini kisa kinaelezwa hivi:
Vijana wanne wakizanzibar waliovamia safari kutoka Zanzibar kuelekea Arusha, waliamua kuiteka ndege hiyo kabla ya kutua Arusha na kumwamuru rubani wa ndege hiyo awapeleke Ulaya,
Kutokana na kipigo, rubani alikubali na kuanza safari ya Ulaya,
Kinyume chake rubani aliwaleta Dar, akawaambia wapo nchi ya Ulaya huko na mafuta wameishiwa hivyo anatua ili wajaze mafuta,
Baada ya ndege kutua uwanja wa ndege Dar ulikuwa tayari upo chini ya ulinzi mkali, na wale vijana walikamatwa kama kuku kwani hawakuwa na silaha yoyote zaidi ya kisu, maembe dodo ambayo waliyatumia kama mambomu na bastola za bandia
Kiasi kwamba vijana walifanikiwa kuwatisha abiria wote nao wakaamini kuwa vijana wale walikuwa na mabomu na bastola kumbe matoi tu!
Hili linarudisha fikra zetu tujiulize kuwa viwanja vyetu vya ndege vinausalama wakutosha?