Nini kiliibadirisha hali hii na nchi kuwa omba omba????

KakaKiiza

JF-Expert Member
Feb 16, 2010
11,578
8,600
Mwaka 1982
Nakumbuka nikiwa mdogo Baba aliumwa tukampeleka kituo cha afya Bunazi akalazwa lakini asubuhi madakitari wakasema huyu ni wakupelekwa Hosptali ya Mkoa ikachukuliwa Ambulance na kumpeleka Hospitali ya Mkoa Kagera, Bukoba (M)
Nakumbuka ilikuwa Land-Rover 109 Station wagon nasisi tukapanda baba akatibiwa akarudi!!

Hicho nikituo cha Afya Bunazi kwa wakati huo kina Ambulance serikali inahudumia,Kuna maji ya Bomba masafi,Kina Generator ya Umeme kwa wagonjwa wanao lazwa hapo!
Tarafani kulikuwa na Trakta 3 Ford kwa ajili ya wananchi kulimia!!
Kwamaana Tarafa ya Missenye tulikuwa na huduma zote za jamii!!

Swali langu ni nini haswa kilisababisha hivi vitu vyote vikapotea huduma zajamii hakuna mpaka dawa mahospitalini hakuna ambulence zimebaki kwenye Hospitali za wilaya pekee!
Na wakati ule uchumi wetu ulikuwa mchanga lakini tulimdu kuwawezesha wananchi!!Hatukuwa tuna machimbo ya madini zaidi ya yayale ya Mwadui shinyanga!
Likini sasa hivi tuna migodi mingi tu!!
Je ni utawala mmbovu au Nyerere alikuwa ana akili zaidi kuliko viongozi wa sasa??

Kuhusu viwanda hivyo naogopa kuviongelea kwani nasikia machungu kwani najua kila mmoja wetu anafahamu nini kilitokea!!
 
Back
Top Bottom