Domy
JF-Expert Member
- Dec 12, 2011
- 4,700
- 1,084
Salaam wana JF
Nasikitishwa sana, na watanzania wanasikitika sana na jinsi mambo yanavyokwenda ndani ya nchi yetu,
Sasa hivi Tz imekuwa siyo nchi salama tena kwa kuishi binadamu na kufanya mambo yako kwa uhuru ingawa nchi inadai kwamba ina katiba.
Hii siyo nchi iliyoachwa na Baba wa Taifa Mwl Nyerere, ambayo ilikuwa tanzania ni kwa ajili ya watanzania, leo imekuwa ni nchi tofauti kabisa na matarajio,imekuwa ni nchi ya mafisadi na wauaji.
Takwimu zinaonyesha Tanzania ni miongoni mwa nchi kumi zinazoongoza kwa ukatili wa polisi duniani,watawala hakuna wanalofanya kutunusuru na hilo bali wamegeuka miungu watu wanaotamani kuabudiwa kuliko hata MUNGU mwenyewe,
Watu wanauwawa ovyo hatusikii hata kauli ya mkuu nchi, hii maana yake nini? Tulimchagua atumike kwetu lakini amekuwa ni mtu wa masafa kila kukicha huku tukikosa majibu ya maswali yetu.
Rais anatakiwa na wananchi wake kuunda tume huru kuchunguza mauaji ya watu,utekaji wa watu wanaodai haki matokeo yake anaweka pamba masikioni na kuvaa miwani ya mbao huku wasaidizi wake wakituambia LIWALO NA LIWE tunapelekwa wapi watanzania,
Maisha ni magumu sana mtaani,hali ni mbaya,kuishi Tanzania sasa ni adhabu wakati tuliahidiwa maisha bora kwa kila mtanzania inawekana,matokeo ni maisha bora kwa kila kiongozi na watoto wao imewezekana,
Tuna viongozi kama Paul chagonja huyu nae anaitwa kiongozi sijui kwa vigezo vipi,akina Kamuhanda wanaua mkoa mmoja wanahamishiwa mkoa mwingine nako wanaua wanaachia wanastarehe uraiani,tunapelekwa wapi,
Watu wanapigwa risasi na mabomu na kufa tunaambiwa wanarushiwa vitu vizito kweli!! Damu ya kijana yule muuza magazeti ALY ZONA nani ataitetea? Damu ya MWANGOSI inatulilia ardhini tufanye nini? Watawala wanatudanganya
mwana JF toa maoni yako nini kifanyike uwatetee watanzania wenzako wanaouwawa ovyo,Leo kwao kesho kwetu.
Naomba kuwasilisha.
Nasikitishwa sana, na watanzania wanasikitika sana na jinsi mambo yanavyokwenda ndani ya nchi yetu,
Sasa hivi Tz imekuwa siyo nchi salama tena kwa kuishi binadamu na kufanya mambo yako kwa uhuru ingawa nchi inadai kwamba ina katiba.
Hii siyo nchi iliyoachwa na Baba wa Taifa Mwl Nyerere, ambayo ilikuwa tanzania ni kwa ajili ya watanzania, leo imekuwa ni nchi tofauti kabisa na matarajio,imekuwa ni nchi ya mafisadi na wauaji.
Takwimu zinaonyesha Tanzania ni miongoni mwa nchi kumi zinazoongoza kwa ukatili wa polisi duniani,watawala hakuna wanalofanya kutunusuru na hilo bali wamegeuka miungu watu wanaotamani kuabudiwa kuliko hata MUNGU mwenyewe,
Watu wanauwawa ovyo hatusikii hata kauli ya mkuu nchi, hii maana yake nini? Tulimchagua atumike kwetu lakini amekuwa ni mtu wa masafa kila kukicha huku tukikosa majibu ya maswali yetu.
Rais anatakiwa na wananchi wake kuunda tume huru kuchunguza mauaji ya watu,utekaji wa watu wanaodai haki matokeo yake anaweka pamba masikioni na kuvaa miwani ya mbao huku wasaidizi wake wakituambia LIWALO NA LIWE tunapelekwa wapi watanzania,
Maisha ni magumu sana mtaani,hali ni mbaya,kuishi Tanzania sasa ni adhabu wakati tuliahidiwa maisha bora kwa kila mtanzania inawekana,matokeo ni maisha bora kwa kila kiongozi na watoto wao imewezekana,
Tuna viongozi kama Paul chagonja huyu nae anaitwa kiongozi sijui kwa vigezo vipi,akina Kamuhanda wanaua mkoa mmoja wanahamishiwa mkoa mwingine nako wanaua wanaachia wanastarehe uraiani,tunapelekwa wapi,
Watu wanapigwa risasi na mabomu na kufa tunaambiwa wanarushiwa vitu vizito kweli!! Damu ya kijana yule muuza magazeti ALY ZONA nani ataitetea? Damu ya MWANGOSI inatulilia ardhini tufanye nini? Watawala wanatudanganya
mwana JF toa maoni yako nini kifanyike uwatetee watanzania wenzako wanaouwawa ovyo,Leo kwao kesho kwetu.
Naomba kuwasilisha.