Nini hupelekea Wasomi wa Tanzania kukimbilia siasa?

Moja ya sababu inayotufanya tuende shule ni kupata pesa,so kwakuwa taaluma hazina pesa ya kutosha ndo maana wasomi wengi wanakimbilia bungeni ndo kwenye pesa.
 
  • Thanks
Reactions: DSN
Argument zako ni very flimsy. Umeandika thread hii bila kufanya utafiti wa kutosha. I can't do it for you for sure.Please go back to the drawing board.

Hint:
Wasomi wa kweli hawako kwenye siasa, kwasababu hawawezi siasa. Wao ni watu wa facts. Walioko kwenye siasa huku wakidai ni wasomi ni matapeli wa elimu, sio wasomi.

Hata wewe sikubaliani na wewe. Nitajie nchi moja tu duniani ambayo wanasiasa wake ni watu ambao hawajaenda shule! In fact ni Tanzania tu ambako idadi kubwa ya wanasiasa ni mbumbumbu wanaojua kusoma na kuandika tu: madiwani, wabunge n.k. Tunaendeshwa na semi-illiterates.

Cheki Spika wetu, ana elimu na uelewa stahili wa kuwa Spika? Just imagine akikutana na akina Lord Carrington kwenye vikao vya Maspika wa Commonwealth, Spika Makinda atajenga hoja gani?
 
Hata wewe sikubaliani na wewe. Nitajie nchi moja tu duniani ambayo wanasiasa wake ni watu ambao hawajaenda shule! In fact ni Tanzania tu ambako idadi kubwa ya wanasiasa ni mbumbumbu wanaojua kusoma na kuandika tu: madiwani, wabunge n.k. Tunaendeshwa na semi-illiterates.

Cheki Spika wetu, ana elimu na uelewa stahili wa kuwa Spika? Just imagine akikutana na akina Lord Carrington kwenye vikao vya Maspika wa Commonwealth, Spika Makinda atajenga hoja gani?
The Best Politiciana duniani ni wale waliokuwa na elimu ya chini ya chuo kikuu,watu kama Abraham Lincoln,Winston Chuchill na hata madikteta wakubwa kama Hitrel na Mussolin walikuwa na elimu ndogo sawa na innovators na kama Bill Gates na Marehemu Mac wote hao ni College dropout.Hivyo kitendo cha Maprofesa wetu kuingia kwenye siasa hakina tofauti na na Profesa Binaisa kuwa Rais Uganda.

Na hata linapokuja swala muhimu lenye kuitaji reality kwenye kureason na Kujudge ni vyema wenye elimu ndogo wakapewa kuongoza njia kwa kuwa wasomi wamekuwa too much theoretically kutathmini mambo kwa kuprove kwa Hypothesis na Synthesis kibao kwa jambo lenye kuitaji Logic na reasoning ya kiinadamu kwendana na wakati na nyakati husika.Fact ni kuwa siasa ni ubunifu wa akili ya kawaida na sio elimu ya Dalasani,nakama kuna wasomi wazuri waliofanya vizuri kwenye siasa duniani basi ni wanasheria kama Bill Clinton na Barack Obama sasa.
 
asungwilemwaifunga

Mkuu asante sana kwa uchambuzi mzuri. Wameamua kweli kupambana, lakini kinachosikitisha ni kuwa wengi wao wanaonekana wamenuwia kuwa viungo hatari vya ufisadi wa kuimaliza nchi.

Ningewaona wapiganaji mahiri kama wangejiunga wakaanzisha chama madhubuti zaidi ya CCM na Chadema, au wangejiunga na chama kimoja cha upinzani kwa wingi zaidi na kutekeleza yale yanayowashinda walioko kwenye hivyo vyama vilivyopo sasa, haswa chama tawala.

Kinachopatikana baada ya wengi wao kujiunga na chama tawala ni sumu ile ile hujazwa ndani ya chupa tofauti. NI JANGA KWA TAIFA LETU!!
 
Last edited by a moderator:
Nchi ilinayoendelea inatakiwa kuwa na wasomi WENGI kama si WOTE. Vinginevyo kama hii si ndoto yako basi nawe utakuwa umeanguka katika dimbwi lile lile la ku- arrogate ufahamu, uelewa, ujuzi na stadi za maisha katika medani mbalimbali kuendelea kuwa mikononi mwa wachache.

Hivyo Wanasiasa wanatakiwa kuwa seti ndogo (ya wasomi) toka seti kuu (Taifa lenye Wasomi wengi wa Taaluma mbalimbali).

KATIKA KARNE HII HATUWEZI KUKUBALI KUONGOZWA NA WATU WASIO NA ELIMU NZURI, wWASIO NA SIFA ZA KUONGOZA WALA WASIO NA MAADILI KATIKA DHAMANA ZAO WALIZOPEWA.

Tatizo si Wabunge / Mawaziri kuwa Wasomi bali ni kuwa na baadhi ya Wabunge wasio na sifa za kuongoza na pia bila kuwa na maadili ya nafasi (dhamana) zao. Tatizo hili linasababishwa na mimi na wewe ambao tunawachagua kwa sababu ya uroho wa vizawadi na pia unafiki wa kujifanya kuwa mgombea ni mzuri wakati tunamfahamu kuwa ni bomu toka utoto / ujana/ utu uzima wake!!
 
Siasa kwa Tanzania ndio biashara inayolipa sana, tena kwa muda mfupi tu, usomi bila pesa ni utumwa ,
 
Kwani siasa ni kwa ajili ya wajinga tu? wasomi hawahitajiki? unaposema wasomi wasiingie kwenye siasa unataka siasa iendeshwe na nani? tunahitaji wasomi kwenye siasa na kwenye utendaji kotekote tu.
 
Binafsi ninafahamu kwamba Maslahi ya walimu wa nchi hii ni duni mno , lakini nilijua ya kwamba walimu wa Sekondari wana nafuu kidogo kuliko wale wa Chekechea au hata wale wa shule za msingi , na hasa wale walimu ambao ni Graduate sikudhani kabisa kama maisha yao yanahitaji kudra za wanasiasa ! Sasa huwa najiuliza imekuwaje wajidhalilishe namna hii ? Kweli maisha ni Magumu kiasi hiki ? hakuna haja ya kutaja majina , Mifano ni mingi na inafahamika ? Naomba Tujadili .
 
Halafu hao wanasiasa siku ikifika wanashangaa matokeo yakiwa mabaya.
 
Unakusudia mwalimu Nyerere au Mzee Ali Hassan Mwinyi?

Prof. Baregu au Prof. Sarungi?

Dr. Mwakyembe? Prof. Mwandosya?
Prof. Kapuya? Prof. Mu..ongo? Dr. Kawambwa? Dr. Lamwai? Dr. Mirigo?

Sasa tujadili nini? Hivi mtu hana haki ya kubadili kazi? Unataka wafe katika kula na kuvuta hewa yenye vumbi la chaki?

Unawaonea hao graduate tu.. hao madaktari na maprofesa vipi?

Nani afanye kazi ya siasa?
 
Unakusudia mwalimu Nyerere au Mzee Ali Hassan Mwinyi?

Prof. Baregu au Prof. Sarungi?

Dr. Mwakyembe? Prof. Mwandosya?
Prof. Kapuya? Prof. Mu..ongo? Dr. Kawambwa? Dr. Lamwai? Dr. Mirigo?

Sasa tujadili nini? Hivi mtu hana haki ya kubadili kazi? Unataka wafe katika kula na kuvuta hewa yenye vumbi la chaki?

Unawaonea hao graduate tu.. hao madaktari na maprofesa vipi?

Nani afanye kazi ya siasa?

Umewataja wengi sana na ninakubaliana na wewe , lakini hukutaja sababu hasa za wao kuingia kwenye siasa ! Kwamba Profesa kweli anaingia kwenye siasa kwa ajili ya nini hasa ? Hujasema sababu .
 
Umewataja wengi sana na ninakubaliana na wewe , lakini hukutaja sababu hasa za wao kuingia kwenye siasa ! Kwamba Profesa kweli anaingia kwenye siasa kwa ajili ya nini hasa ? Hujasema sababu .

Wanaingia kwenye siasa kwa sababu huko ndio kwenye nafasi ya kugawana keki ya taifa, kaka!
Siasa kwa hapa Tz ndio kazi nyepesi lakini inayoleta tija kubwa.

Wanasiasa wanatafuna hela ya walalahoi(umma) kama mlevi anavyotafuna kitimoto kwa bia.

Ndio sababu kila anayepata upenyo anadandia usafiri wa siasa. Sasa imekuwa ni tabia kwa kila anaetaka kukimbia kugawiwa umasikini anajiunga katika timu ya kugawa umasikini.
Siasa kwa Tz inalipa, dugu.
 
Umewataja wengi sana na ninakubaliana na wewe , lakini hukutaja sababu hasa za wao kuingia kwenye siasa ! Kwamba Profesa kweli anaingia kwenye siasa kwa ajili ya nini hasa ? Hujasema sababu .

Wanaingia kwenye siasa kwa sababu huko ndio kwenye nafasi ya kugawana keki ya taifa, kaka!
Siasa kwa hapa Tz ndio kazi nyepesi lakini inayoleta tija kubwa.

Wanasiasa wanatafuna hela ya walalahoi(umma) kama mlevi anavyotafuna kitimoto kwa bia.

Ndio sababu kila anayepata upenyo anadandia usafiri wa siasa.

Sasa imekuwa ni tabia kwa kila anaetaka kukimbia kugawiwa umasikini anajiunga katika timu ya kugawa umasikini.
Siasa kwa Tz inalipa, dugu.

Haki haitolewi katika sinia,haki inapiganiwa.watanzania tumelala, hatudai haki zetu ndio sababu wanasiasa wanaendelea kutufanyia upuuzi. Tungelikuwa tunawawajibisha, wachache wangekimbilia katika siasa.

Ukitaka sababu nyengine, nitakuongezea.

Wewe hujui sababu hata moja kwa nini walimu wanakimbilia kwenye siasa? Lakini ujue sio walimu tu....ni kila aliyekata tamaa ya kupata maisha bora kwa njia halali.

Kuna wachungaji, kuna waimbaji,wasanii wenye majina ya wale wadudu wanaotembelea miti na migomba usiku au jina mbadala la toto tundu!! nk.
 
Wanaingia kwenye siasa kwa sababu huko ndiko kuliko na maslahi mazuri,hakuna stress, husumbuliwi na uhaba wa vifaa. Unajua tunafanya kazi ili tuwe na maisha mazuri ni wachache sana wanafanya kwa sababu ya wito. Wewe huoni jinsi tulivyo na uchache wa madactari lkn huacha kazi zao na kujiunga kwenye siasa. Ukiwa mwanasiasa maisha yanakua rahisi namaanisha ukiwa mbunge huna kazi kubwa. Kazi yako ni kuangalia watawala wanataka nini then ukiwa bungeni unaunga mkono hoja hata kama hukubaliani nayo ili mradi maisha yaende.
Sasa uking'ang'ania kufundisha wakati unaona kuna uwezekano wa kutoka kwa njia ya siasa si utajiona mjinga. Ule usemi wa uwalimu ni wito umepitwa na wakati. Waalimu walikua wavumilivu sana na bado wanavumilia mengi kwani kazi yao ni ngumu na imesahaulika. Wewe inaumaje unapoona mwanafunzi wako kawa mbunge na amenona kwa kula keki kisha hata elimu uliyo nayo hajakufikia na unajua jinsi alivyomaliza kwa taabu degree yake yaani kwa supp nyingiiiii. Siasa imepewa kipaumbele sana ndio maana watu muhimu sana kwenye proffession zao wanaacha na kuingia humo. Hebu ona mtu kama dactari wa moyo alivyo muhimu na walivyo wachache anaingia kwenye siasa tunatesekaje wagonjwaaa. Shida hii itaisha tu pale tutakapowathamini wasomi/wataalam na makundi mengine halafu siasa ikawa ya mwisho kuanzia maslahi nk.
 
Siyo walimu tu hata madaktari, watu wenye taaluma zao siasa inalipa.
 
Wakati serikali za wenzetu kama china zikiwathamini wasomi,sisi tunawadhalilisha na kuthamini siasa.bongo bwana!
 
unataka wasio wasomi ndo wajazane kwenye siasa? ndo watupangie na kutuamulia mambo yetu? bora wasomi wa ukweli wajazane kwenye siasa kuliko wasio wasomi. nafas za siasa si nyingi kihivo kuwa huku kwingine kutakuwa hamna wasomi. kwamba akiukwaa uwaziri atakuwa na majivuno hiyo hulka ya mtu. the last thing we need as a nation is to have uneducated people katika ngazi za kutupangia na kutuamulia mambo.
 
Taifa letu liko kwenye kipindi kizito sana kuvuka kwenye nyanja ya siasa na uchumi.Lakini tumefika hapa kivipi?Jibu langu kwa kujiuliza huko swali hilo na kujifunza kupitia kuona na kusoma tatizo la msingi na kubwa walilonalo watanzania ni la wasomi wengi wa Taifa hili kuwa ni majisifu, ufithuli, kujigamba, wenye kujitwalia bila haki ,jipachika hasa bila haki, jitwaza,jipachika utukufu wa Taifa kwa mgongo wa siasa kufaidi matunda ya uchumi.[Allogance and Arrogate]

Someone who is arrogant behaves in a proud, unpleasant way towards other people because they believe that they are more important than others.

If someone arrogates to themselves something such as a responsibility or privilege, they claim or take it even though they have no right to do so.

Leo hii Mtanzania aliyesomeshwa kwa mamilioni yapesa kwenye taaluma husika wamekimbilia kwenye siasa kwa kujua watakaa kwenye maamuzi na kuwa na kofia ya kujitwalia keki ya Taifa kimya kimya.Ni kwa wao kuingia kwenye kofia ya maamuzi leo Taifa halina watu wa kulishape [Think Tank],Wataalamu wa kilimo,maengineer,maprofesa, madaktari wa vyeo na madaktari wa Taaluma,walimuna wanasheria wote wamelundikana Bungeni na hatimae kuwa wana itikadi baada ya kuwa wanawataifa.

Kwa wenzetu taaluma pia umpelekea mtu kuwa ni aina gani ya mwanasiasa katika ulingo wa siasa,wasomi wa masomo ya political economy,mausiano ya kimataifa, wanasheria,watu wa masoko na wachumi ndio ambao kwa namna fulani wamejikuta kuwa wanasiasa.Leo hii kwa Tanzania sivyo.

Tumezalisha lundo la wasomi kila mwaka hawakai ofsini kuwa engineers wa kujenga Nchi kwa Taaluma zao bali wanatayarisha michakato ya kugombea ubunge ili atimae achaguliwe kuwa waziri hatimae kupata upofu wa si hasa.

Tuangalie vyanzo vya matatizo yetu,ebu pitieni CV za wabunge wa Taifa letu kila mmoja wekeni hapa,pimeni wahusika wangetumika sehemu husika pengine leo tusingekuwa na wanataaluma kwenye foleni queue ya kukusanya pesa ya umma kupitia miradi ya serikali ili kuwania ubunge na presidential appointment huku Taifa likiwa limesimama kwa kukosa watu wa kuengineer mambo ya kusogeza Taifa mbele kwa kuanda mikakati.

Je na wewe ni Mwanataaluma msomi?



The easiest way hapa Tanzania kuwa mjinga ni kukimbilia siasa kwani kule utakuwa unapiga kelele tu huku ukila posho na siku zinaendelea. Imagine eti mtu una masters degree yako labda ya business then unakimbilia siasa, are you serious? Kwa hapa Bongo ukisoma unakuwa tishio na kupata kazi nzuri mpaka upate referee wa kiukweli maana kazi za hapa ni za kupeana.
 
Back
Top Bottom