Tatizo kwenye vyama vya upinzani ni ukosefu wa demokrasia ya ndani. Ni vema viongozi wakawapisha wengine na wao wakabakia wanachama waaminifu na wapiganaji.Kufanya hivyo watapata nafasi ya kuona matatizo wakiwa nje ya uongozi. Kwa sasa kukimbiwa na viongozi mbalimbali ni kutokana na hao kuona kuwa mbele kumezibwa. Tunawaheshimu viongozi hao waliokaa zaidi ya miaka kumi na historia itawajenga kama wakiachia ngazi badala ya kung'ang'ania madaraka. Si lazima tufuate, lakini nchi nyingi kiongozi hujudhuru iwapo ameshindwa kukiingiza chama chake madarakani..