Shadow,
Mkuu shukran sana kwani umenipa somo zuri sana ulipotaja Patriotic Act. Hawa wenzetu wanakwenda na wakati na kama navyosisitiza siku zote kwamba ni muhimu kutambua uliposimama yaani Watu na Mazingira ni muhimu sana ktk utunzi wa kitu chochote ikiwa ni pamoja na sheria...Kila hatua ya maendeleo inahitaji kutazama vitu hivyo laa sivyo tutakuwa tunajikanyaga tu kila siku.
Kwa umaskini wetu sisi waafrika ni sawa na mafisi wenye njaa. sasa kama utawafuga fisi karibu na machinjioni inabidi uweke sheria ama vikwazo ambavyo unafahamu watu(fisi) hawa hawawezi kuvizia mifugo yako ktk mazingira yale (machinjioni). Na hata kama ukisema wale watu sio mafisi ila ni mbwa tu, basi malezi ya kuwapa nyama mbichi ya mifugio yako kila siku inaweza kuwafanya wakaanza kula hata mifugo yako pindi ukichelewa tu kuwalisha.
Tanzania leo hii tunapata matatizo yote haya sio kwa sababu ya demand and supply bali imekuwa ni mila na desturi ya Mdanganyika kutafuta utajiri kiujanja ujanja. Umaskini fedheha jamani!
Ukitazama mafisadi wote hawa ni matajiri wa kutupa, hao viongozi wetu wanapewa mishahara kuliko hata viongozi wa nchi za Ulaya lakini bado kila siku wanatafuta mbinu za kutuibia zaidi nje ya mishahara na marupurupu wanayopewa..
Ni lazima fagio la chuma lirudishwe!. Ni lazima Azimio la Zanzibar life haraka sana, laa sivyo hakuna kinachoendelea Tanzania. Tusidanganywe na siasa wala vyeti vikubwa ukutani kutuambia uchumi unatakiwa kuendeshwa hivi ama vile..
Binafsi nampongeza Kikwete kwa hatua zote alizokwisha chukua hadi sasa hivi na muhimu zaidi kauli yake aliposema viongozi wote wanaotaka kufanya biashara inabidi waachie madaraka... kauli hiyo naomba iwe ktk Kanuni na maadili ya viongozi Kitaifa.
Mkuu Mkandara, Asante pia kwa uchambuzi wako. Tatizo la rais wetu ni moja. Kuweka urafiki mbele sana kuliko masirahi ya taifa ( mfano issue ya wanamtandao) hao ndo wanayumbisha nchi hii kwa sababu karibu wengi wao ni wabaka uchumi.
Akiweza kuwachulia hatua tena kali hao wabaka uchumi, basi atakuwa ametuvusha kikwazo cha kwanza. Pili unafiki wa wabunge wetu ambao wengi ni rubber stamp za vyama vyao na wala hawasimami katika kupigania haki za mtanzania.
Tunasafari ndefu mzee. Kama ni hiyo safari basi tupo kwenye kilima kikali na gari alina break!