Ningependa JK Atuambie Yafuatayo Kwenye Hotuba Yake

WaMzizima

Senior Member
Jun 25, 2009
152
41
Baada ya kuahirisha hotuba yake na apparently kwenda Kigali kwenye sherehe yao ya miaka 50 ya uhuru (ilhali Kagame hakuja hapa, anyhow...), ningependa atueleze wananchi wake yafuatayo kwa kina :

1. Mgomo wa madaktari na muelekeo wake wote, anafanya nini kumaliza huo mgomo?
2. Usajili wa meli za Iran Zanzibar na tishio la kuwekewa vikwazo na USA
3. Mustakabali mzima wa vuguvugu linaloendelea Zanzibar kuhusu muungano
4. Dr Ulimboka na nani hasa waliohusika na unyama huo
5. Kwa nini yupo Kigali, wakati Kagame hakuja hapa na kuna mambo ya muhimu kushughulikia? hivi rais wetu anakamdudu ka safari au ni kitu gani, kwa nini hakumtuma Membe kwenda huko...


Kwa nini anakua mkimya kwa muda mrefu wakati kuna mambo mengi wananchi wake tunakuwa na dukuduku nayo na kuruhusu majungu kupamba moto nchini ilhali yeye kama kiongozi yupo kimya.

Na badala ya mpango wake wa kuongea na wazee na Dsm, safari hii akaongee na vijana wa Zanzibar...

Na mengine ongezeeni hapa
 
Back
Top Bottom