OSOKONI
JF-Expert Member
- Oct 20, 2011
- 10,965
- 5,336
Wakuu HEmedi baba yake amewahi kuwa rpc Arusha HEMEDI mwenyewe alianzia kazi ya polisi Arusha akaenda kusema diploma ya sheria aliporudi alipelekwa kituo cha Usariver sehemu yenye kituo na vifaa maalum vya kutesea wahalifu. Yeyote anaekamatwa na anatakiwa kuhojiwa aliekwa anapelekewa ni HEMEDI kuna wahalifu wengi wamekufa wakiwa wanahojiwa nae. Huyu jamaa baadae alihamisiwa Morogoro.
Hiki sio kituo cha polisi kinatakiwa kiitwe SOBIBOR, kambi ya mateso! Watu wanaopelekwa kwenye hichi kituo wanapata mateso makubwa mno, wanawake wanabakwa, wanaume wanalawitiwa na polisi, wanabanwa sehemu za siri na kufanyiwa unyama mwingine usio na wa kibinadamu,naweza kusema kuwa ni kituo ambacho pia kinaongoza kwa Kupokea Rushwa askari wote wa kituo hiki wana magari HIACE zaidi ya mbili wamejenga majumba ya kifahari na wanaishi maisha y anasa sana, Je mshahara wao kweli ndio unawatosha kufanya hivo? Wanaharakati na wapenda mageuzi hebu mulikeni kituo hiki cha polisi ili kuwaondolea wananchi mateso, manyanyaso na kuvuliwa utu ndani ya nchi yao!!Huyu Msangi alikuwepo hapa akitesa watu kupokea rushwa,kubaka, kulawiti na kuwafanyia wakazi wa Arusha kila ukatili!!