Ninauliza Nani Kaiweka Nchi Rehani?

Ninauliza Nani Kaiweka Nchi ya TANZANIA Rehani?

Jibu:
-Wananchi wenyewe kwa kutoonyesha msimamo mkali dhidi ya viongozi wanaowachagua kuchukua majukumu kwa niaba yao.

-Viongozi wakiwa 'mwangwi/kivuli'(reflection) ya jamii waliyomo kwa kutoonyesha kuwa wanaweza kuja na mbinu endelevu na madhubuti katika kulinasua Taifa lao.

-Vyombo vya sheria na mihimili kuu ya nchi isiyofanya kazi au kutekeleza majukumu yake iliyojiwekea yenyewe, pia kutoendeleza mbinu au kanuni mpya ili Taifa zilizomo liendelee.

-

-

SteveD.
 
Ulichosema ni kweli Steve. Lakini CCM ndio hasa walioweka Tanzania rehani. Wananchi wakijaribu kufurukuta tu kupinga maamuzi mbali mbali kwa mfano mikataba ya madini, wizi wa kura na maamuzi mbali mbali yasiyokuwa na maslahi kwa Tanzania basi polisi, FFU na hata jeshi vinaweza kutumika katika kuhakikisha wananchi 'mafedhuli' wanapata mkong'oto wa uhakika. Kwa hiyo jibu langu ni CCM ndiyo iliyoiweka Tanzania rehani.
 
1. Most Tz are igronant na maskini na ukiwapa tu wali na kanga unapata kula- sasa unategemea nini?

2. CCM exploit such ignorance- sasa nani wa kumlaumu?
 
Kuna uhusiano mkubwa sana kati ya umasikini wa watanzania na ujinga wao.Wengi wao wanajua kuwa umasikini wao ni maamuzi ya mungu na siyo sera na utendaji kazi wa CCM.
Pili wao wanadhani kuwa umasikini wao pia umetokana na sababu kuwa wao si watoto wa viongozi au hawana uhusiano wa karibu au kujulikana na viongozi.
Ni mpaka hapo watakapoona kuwa kuna uwezekano wa kuwa na maisha bora na mazuri bila ya kuwa mtoto wa kingunge au malechela...very sad!..

-Wembe
 
Tatizo letu kubwa kwa maoni yangu ni vyombo vya dola mahakama, polisi, FFU TPDF n.k. Hawa jamaa watapofumbua macho, kubwaga manyanga na kuungana na watanzania katika vilio vinavyohusu maamuzi mbali mbali ambayo hayana maslahi na Tanzania, basi hapo ndio utakuwa mwanzo wa mabadiliko makubwa katika nchi yetu. Lakini sasa hivi watawala wanahakikisha 'kuwalea' vizuri hawa jamaa. Wakinung'unika kidogo tu wameshasikilizwa. Kwa sasa hivi wamewekwa mifukoni mwa CCM hivyo CCM itaendelea kuiweka Tanzania rehani kwa sababu wanajua vyombo vya dola vimo mifukoni mwao.
 
Tatizo letu kubwa kwa maoni yangu ni vyombo vya dola mahakama, polisi, FFU TPDF n.k. Hawa jamaa watapofumbua macho, kubwaga manyanga na kuungana na watanzania katika vilio vinavyohusu maamuzi mbali mbali ambayo hayana maslahi na Tanzania, basi hapo ndio utakuwa mwanzo wa mabadiliko makubwa katika nchi yetu. Lakini sasa hivi watawala wanahakikisha 'kuwalea' vizuri hawa jamaa. Wakinung'unika kidogo tu wameshasikilizwa. Kwa sasa hivi wamewekwa mifukoni mwa CCM hivyo CCM itaendelea kuiweka Tanzania rehani kwa sababu wanajua vyombo vya dola vimo mifukoni mwao.

Ni kweli, lakini kuna haki moja ambayo imoanishwa kwenye katiba na kumbuka nilifundishwa kwenye Civics.

Haki ya kwanza ni kupiga kura,......kuchaguliwa kuwa kiongozi...
lakin kuna haki.
Ya kumwondoa madarakani kiongozi ambaye hafai


Ni lini au wakati gani tunatekeleza haki hiiii
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom