Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Wakuu, mimi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 25, kwa sasa ninavirusi vya ukimwi, ninatamani sana kuolewa na kuzaa watoto, nifanye nini? je ntapata mwanaume wa kunioa? na tukitaka kuzaa salama tutafanyaje?
naombeni msaada wenu wana jamvi.
Pole sana mpendwa.....
Nakushauri tembelea vituo vya ushauri nasaha kuna watu wengi wanaoishi kwa matumaini wanatafuta wenzi wa kuishi nao. Kuwa na VVU siyo mwisho wa maisha. Usikate tamaa, kaza moyo... Kama vipi nenda pale PASADA uonane na washauri nasaha... kuna dada yangu mmoja alijipatia mchumba pale, wameoana na wana mtoto ambaye hajaathirika.
Mungu aliye mbinguni akubariki na kukuongoza.
Mdogo wangu haupo peke yako watu wengi sana wameathirika.Na wengi hawajijui Hongera wewe unaejitambua.
Inawezekana sana tena kwa asilimia 100% wewe kuolewa na mwanaume utakae pendana nae.Na kupata watoto.Tena kwa umri wako jihesabie Miaka 15 ya kuishi bila ARV.
Hivyo Vyama ni uzushii Mtupu achana nao Wengi wao wapo kimaslahi yao zaidi.Ww jiangalie wewe kama wewe nenda Hospital angalia afya yako yote kwa ujumla.
Kumbuka wagonjwa wazamani hawakuwa na ARvs wala kinga dhidi ya mtoto alie tumboni lakini siku hizi vitu hivyo vipo.Usikate tamaa.Na imani baada ya miaka kadhaa TIBA itapatikana.Matokea yanaonesha hivyo.Kikubwa Jitunze.
Nitumie Private mail.nikuelekezee zaidi na kukupatia msaada zaidi
Wengi wanampa pole sijajua wanampa pole kwa ajili gani? Kwani amesema anaumwa? Dada usiwe na wasiwasi kuhusu kuolewa na kupata mtoto,vyote hivyo vinawezekana kwa 100% pale TACAIDS wapo watu ambao ni HIV+ wanatafuta wa kuwaoa cha msingi nenda pale utapata mtu.
King Katika watu niliokuwa nawaheshimu wewe ni mmoja wapo lakini leo nimekushusha thamani kabisa.
Una hakika kuwa wafanyakazi wa TACAIDS wapo HIV+ (Ninabisha na ninauthibitisho wa hilo ukitaka)
Sidhani kama unajua hata kazi wala majukumu yake. For your infomation TACAIDS hakuna mtu ambaye hajaoa wala kuolewa. Muwe mnazungumza vitu mlivyo na uhakika sio kuropoka hovyo hovyo tu.
Ushauri kwa mdada:
Wengi wamekwambia hapo juu nenda pima magonjwa yote moyo, sukari nk ili ujue uko katika hali gani ikiwamo kuangalia CD4 zako ziko kiasi gani kwa sasa usije kuchelewa ukakuta zimeshuka sana ukapata magonjwa nyemelezi kwa maelezo zaidi NI PM
we we mletata mada mbona umekula kona au ndio unasoma ushauri we nenda maeneo waliokushauri utapata tu mtu mwenye wazo kama lako amini nakuambia hilo bibie enjoy and feel your expressional