Tegelezeni
JF-Expert Member
- Dec 31, 2009
- 268
- 124
Hata sijui sababu ni nini, maana kama ni kula nakula vizuri tu na mke wangu anajitahidi kunipikia mapochopocho mpaka basi lakini mwili wangu hauridhiki sijui kwanini, yaani nimekuwa na maumbile madogo wala sinenepi kabisaa mpaka ndugu zangu wanahisi kwamba huenda mke wangu hanipi chakula na ndio maana sinenepi kumbe binti wa watu anajitahidi kukalangiza lakini mwili wangu huu hauna shukurani.
Hebu nisaidieani, sababu hasa ya kukosa kwangu siha ni nini?
Hebu nisaidieani, sababu hasa ya kukosa kwangu siha ni nini?