Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,460
- 39,927
Nimeivuta manati, kumlenga ndege huyu,
Nikasikia sauti, siyo yake mbayuwayu,
Kutoka tawi la mti, si mbuyu ni mkuyu
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki
Nimwite nani?
Kwanza nipe hilo jina, ndege huyo katamka
Bila jina mimi huna, msituni nitaruka,
Niwe mlo wa mchana, jina langu ninataka
Ndege anataka jina bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Karuka karukaruka, mtini akiringia,
Huku anacheka cheka, mbawa akinipungia,
Manyoya yakitimka, manati nimeshikia
Ndege anataka jina bila jina hatunguki,
Nimwite nani?
Katunisha na kifua, na wimbo kaniimbia,
Hamu ikanichukua, jiwe nikaachilia,
Ndege akajichepua, mbali likapitilia,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Huamini wa kijiji, bila jina mimi siji,
Hata ukinipa mji, Wa Dar au Ujiji,
Na univishe na taji, unipe togwa na maji,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Njaa imenizidia, ndege namtamania,
Jina naliulizia, wawindaji saidia,
Mwingine atajilia, huyo akiniwahia,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Nawauliza malenga, mabingwa wa kutungia
Mnaotoka Karenga, Wa Pwani nawaitia,
Ndege bado namlenga, jibu nalisubiria,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Na: M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)
Nikasikia sauti, siyo yake mbayuwayu,
Kutoka tawi la mti, si mbuyu ni mkuyu
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki
Nimwite nani?
Kwanza nipe hilo jina, ndege huyo katamka
Bila jina mimi huna, msituni nitaruka,
Niwe mlo wa mchana, jina langu ninataka
Ndege anataka jina bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Karuka karukaruka, mtini akiringia,
Huku anacheka cheka, mbawa akinipungia,
Manyoya yakitimka, manati nimeshikia
Ndege anataka jina bila jina hatunguki,
Nimwite nani?
Katunisha na kifua, na wimbo kaniimbia,
Hamu ikanichukua, jiwe nikaachilia,
Ndege akajichepua, mbali likapitilia,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Huamini wa kijiji, bila jina mimi siji,
Hata ukinipa mji, Wa Dar au Ujiji,
Na univishe na taji, unipe togwa na maji,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Njaa imenizidia, ndege namtamania,
Jina naliulizia, wawindaji saidia,
Mwingine atajilia, huyo akiniwahia,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Nawauliza malenga, mabingwa wa kutungia
Mnaotoka Karenga, Wa Pwani nawaitia,
Ndege bado namlenga, jibu nalisubiria,
Ndege anataka jina, bila jina hatunguki!
Nimwite nani?
Na: M. M. Mwanakijiji (Sauti ya Kijiji)