Ndachuwa
JF-Expert Member
- Mar 8, 2006
- 6,269
- 4,569
Mpenzi wangu amechanganyikiwa,
anahitaji msaada wangu wa mawazo.
Nimeshindwa kumpa kwa kuwa hata mie nimechanganyikiwa.
Juzi kapata barua ya kufukuzwa kazi.
Kaenda nssf kufuatilia mafao yake, akaambiwa arudi na barua ya mwajiri.
Mwajiri kagoma kumsainia, kasema kwa kuwa alikuwa na mkopo kazini basi mafao yake yanachukuliwa na mwajiri.
Amekuwa akilia tu tangu asubuhi mpaka sasa, kila baada ya dakika tatu ananipigia.
Sina hata maneno mazuri ya kumpa moyo.
Naomba mnisaidie ushauri ili mama watoto apunguze maumivu.
Nampenda sana, akilia yeye na mimi naumia sana rohoni.
Hata kama kazi imeisha, ni jambo la kheri kumalizana na mwajiri wako kwa uzuri. Kama ulikopa si budi ulipe? Kuna leo na kesho. Ukiondoka vibaya watakapohitaji reference zako zitajazwa hivyo hivyo. Swala la kujaziwa fomu za NSSF, mwajiri hawezi kujaza hizo fomu kabla ya kufanya "Clearance" si kwa ubaya au chuki binafsi, kuna auditors wakija kuta Ex-employee anadaiwa hiyo ni Query. Sorry kwa hilo mimi ni mkaguzi huwa tunauliza sana jambo la Clearance kwa mfanyakazi aliyeondoka hasa pale ambapo bado anadaiwa.