wiseboy
JF-Expert Member
- Mar 22, 2011
- 2,931
- 3,299
Mimi ni mkazi wa kijiji cha ujamaa Bumangi kilichopo wilaya ya musoma vijijini, ambalo ni jimbo la nimrod mkono na ni kijiji cha tatu toka nyumbani kwa mbunge wangu nimrod mkono.
Nimezaliwa, nimekulia na kupata elimu ya msingi na upili hapo kijijini kwetu ,kabla ya kukiacha kwa kwenda kujiunga na masomo ya advance na badae chuo kikuu mikoa mingine.
Niende moja kwa moja kwenye mada
toka nikiwa mdogo kijiji changu kinakabiliwa na ukosefu mkubwa wa maji, japokuwa ukiwa kijijini kwetu ukinyanyua macho upande wa kaskazini utaona maji ya mto mara yakitiririka kuingia ziwa victoria, nikikumbuka siku moja tulitolewa darasani nikiwa kidato cha tatu, huko kisimani kulitokea ugomvi wa maji ya kwenye vidimbwi kati yetu wanafunzi na wanakijiji, nakumbuka nilimwagiwa tope shati langu la shule.......nikikumbuka adha hii ya maji kwa sasa natokwa machozi.
juhudi nilizofanya binafsi kulitatua tatizo hili
1:nikiwa mwaka wa kwanza nilifika kwa mkono jijini dar es salaam ili nimuone na kumfikishia kilio hiki cha shida ya maji wanayopata wazazi, ndugu, na wanajamii kwa ujumla pale kijijini lakini kwa bahati mbaya walinzi hawakuniruhusu niingie pale kwake, na hata nilipojaribu kumsubiri nje ya geti, alinipita bila kusimama akiwa ndani ya gari lake.
2.nikiwa mwaka wa pili nilijaribu kutafuta ushauri kwa baadhi ya maprofesa pale chuoni kuona kama nitapata msaada wa kupata wadhamini wa kusambaza maji kijijni kwetu, japo sikufanikiwa kwani walinishauri niconcetrate na masomo kwanza there after ndo nideal na hili suala
facilities zilizopo kijijini kwetu
miaka ya huko nyuma kulikuwa na huduma ya maji, japo miundo mbinu haikufanyiwa matengenezo hivyo kushindwa kufanya kazi......kwa kigezo hicho kijijini kwetu kuna matank makubwa ya kuhifadhi maji, na pia kuna steel pipeline ambazo bado zipo connected, na pia umbali wa kilomita 20 kuna chemi chemi yenye maji mengi yanaweza kuvunwa na kujazwa kwenye matank.
DHUMUNI LA KULETA HII MADA HAPA
1. Kama kuna mtu ana email ya nimrod mkono humu naomba amforwadie hii thread yangu
2:sitaki kukata tamaa, naomba wana jf kama kuna mtu anajua funders wanaoweza kudhamini mradi wa maji kijini anisaidie link yao
3:kama kuna mtu ana proposal format ya jinsi ya kuandika project proposal juu ya maji, please anitumie kupitia mmattuh@gmail.com
please toka moyo mwangu naumia sana na hili tatizo la kijiji changu, naombeni mawazo yenu na msaada wenu kulifanikisha hili suala, nifanyeje? karibuni wakuu
Nimezaliwa, nimekulia na kupata elimu ya msingi na upili hapo kijijini kwetu ,kabla ya kukiacha kwa kwenda kujiunga na masomo ya advance na badae chuo kikuu mikoa mingine.
Niende moja kwa moja kwenye mada
toka nikiwa mdogo kijiji changu kinakabiliwa na ukosefu mkubwa wa maji, japokuwa ukiwa kijijini kwetu ukinyanyua macho upande wa kaskazini utaona maji ya mto mara yakitiririka kuingia ziwa victoria, nikikumbuka siku moja tulitolewa darasani nikiwa kidato cha tatu, huko kisimani kulitokea ugomvi wa maji ya kwenye vidimbwi kati yetu wanafunzi na wanakijiji, nakumbuka nilimwagiwa tope shati langu la shule.......nikikumbuka adha hii ya maji kwa sasa natokwa machozi.
juhudi nilizofanya binafsi kulitatua tatizo hili
1:nikiwa mwaka wa kwanza nilifika kwa mkono jijini dar es salaam ili nimuone na kumfikishia kilio hiki cha shida ya maji wanayopata wazazi, ndugu, na wanajamii kwa ujumla pale kijijini lakini kwa bahati mbaya walinzi hawakuniruhusu niingie pale kwake, na hata nilipojaribu kumsubiri nje ya geti, alinipita bila kusimama akiwa ndani ya gari lake.
2.nikiwa mwaka wa pili nilijaribu kutafuta ushauri kwa baadhi ya maprofesa pale chuoni kuona kama nitapata msaada wa kupata wadhamini wa kusambaza maji kijijni kwetu, japo sikufanikiwa kwani walinishauri niconcetrate na masomo kwanza there after ndo nideal na hili suala
facilities zilizopo kijijini kwetu
miaka ya huko nyuma kulikuwa na huduma ya maji, japo miundo mbinu haikufanyiwa matengenezo hivyo kushindwa kufanya kazi......kwa kigezo hicho kijijini kwetu kuna matank makubwa ya kuhifadhi maji, na pia kuna steel pipeline ambazo bado zipo connected, na pia umbali wa kilomita 20 kuna chemi chemi yenye maji mengi yanaweza kuvunwa na kujazwa kwenye matank.
DHUMUNI LA KULETA HII MADA HAPA
1. Kama kuna mtu ana email ya nimrod mkono humu naomba amforwadie hii thread yangu
2:sitaki kukata tamaa, naomba wana jf kama kuna mtu anajua funders wanaoweza kudhamini mradi wa maji kijini anisaidie link yao
3:kama kuna mtu ana proposal format ya jinsi ya kuandika project proposal juu ya maji, please anitumie kupitia mmattuh@gmail.com
please toka moyo mwangu naumia sana na hili tatizo la kijiji changu, naombeni mawazo yenu na msaada wenu kulifanikisha hili suala, nifanyeje? karibuni wakuu