Nimfanye nini huyu dada jamani?

jaman poleh sna la msingi chukua maamuzi magum ya kutimua dada wa salun... Yu wil safa for a moment haina tabu cuz wen yo in biznes risks are inevitable...
 
Ukiwafukuza utapata wengine (wapo wadada wengi tu wanaohangaika kupata kazi), ukiwaacha next time wanaweza wakafanya kitu kikubwa zaidi.

Unaweza ukaamua kukaa kimya wiki iishe bila kuwauliza chochote ila ukawa unatafuta wafanyakazi wengine, ukishapata unawatimua. Hamna haja ya kuwasema maana wenyewe wanajua walichokifanya.

Leo kwa kua natoka kazini mapema nitakachofanya ni kuanza kutafuta wengine.
Nikiprint matangazo yangu nikabandika uswahili ninaamini hadi j4 nitapata wa kuhojiana nao kwa kufanya kazi.
Nawaambia wasije kazini kuanzia jumatatu hadi nitakapowajulisha
 
pole sana dada na pia uwashukuru sana hao madereva tax
siku zote huwezi kukaa na adui yako hata cku moja
jipange kwa kutafuta wafanyakazi wengine kisha hao fukuza
 
Hongereni kwa kuingia mwaka mpya.
Nina jambo limetokea leo ambalo ni mfululizo wa mambo mengi yaliyokua yakitendeka siku zilizopita.
Ni story ndefu ntajitahidi kuifupisha.
Ninaishi kwenye nyumba ndogo na mdogoangu mwanafunzi na mtoto wa 4yrs ambaye ni mtoto mdogoangu mwingine na msichana wa kusaidia kazi ukizingatia nina huyu mtoto mdogo nami ni mfanyakazi.
Leo nikiwa kazini nimepigiwa simu na tax driver wa pale jirani na kwetu kua msichana wangu ameonekana na begi anaondoka,na ameenda kuchukua tax pale ndio wakawa wanamuhoji maana kuna wanaomfahamu(mara nyingi nikiwa kazini kama kuna kinachotakiwa nyumbani nawaomba hao madereva wanifikishie hivyo humkuta yeye).
Nikawaambia wamzuie,nikamtuma mdogoangu aende akaongee na huyo binti amuulize kwanini alitoroka badala ya kuaga?
Binti akahojiwa,hakutoa jibu lolote,akasachiwa eti kabeba laptop,camera na perfume(nimeshangaa,nilitegemea atabeba nguo na labda simu!) akasemwa pale,akanyang'anywa alivyochukua nikawaambia wamruhusu aende maana nisingeweza kukaa nae tena,akaruhusiwa akaenda.
Sasa jioni hii narudi nyumbani nikapita kwa wale madereva waliyoniambia yamenichosha!!
Wanasema walipomuuliza anaenda wapi akasema kuna dada anafanya kazi salon kwangu,anaishi kinyerezi ndio waliongea kua aondoke atamsubiri tabata asubuhi ile (hajataja tbt ipi) ni kweli nina salon hapa jirani na ninapoishi na kuna mfanyakazi anaishi kinyerezi(naamini hawa madereva hawamfahamu) nae anatafuta housegirl.
Nimeshindwa kuelewa namfanyaje huyu dada wa salon.
Na siku za nyuma nilikua na binti ambae alikuja kwangu akiwa mjamzito nikampokea vizuri,
haohao wafanyakazi wa salon kwangu (wa kinyerezi)wakaanza kumzonga na maneno akawa ananiambia hadi tumbo limekua ndio wakawa wanashangaa eti ana mimba nimuondoe atanitia mzigo(wakati nilijua mapema) binti kaenda kwao kujifungua,huyu kaja tar 30 Dec washamchukua.
Hivi niwafanyeje hawa wafanyakazi wa salon kwangu??

yafukuye kazi hayo majununi
 
Wa uswazi si ndio wale wale jamani au huko kwenu ni tofauti na huku kwetu.

Ni kweli JB,
lakini kupata wafanyakazi wazuri inahitaji muda na gharama...
Kwa sasa sina muda wa kushughulikia hilo kikamilifu. Nachukua mmoja uswazi mwingine VETA.
 
Back
Top Bottom